Wednesday, August 19, 2020

WATEJA WA ZAMANI NI LULU ?? WEKA KUMBUKUMBU ZAO . !!!

 Nguzo muhimu katika biashara yoyote duniani ni wateja. Ninaweza kusema kwamba biashara inafanikishwa na watu wawili; yaani mfanyabiashara ambaye ndiye anauza bidhaa au huduma na wa pili ni mteja ambaye ananunua bidhaa. Kama unafanya biashara ambayo wateja wapo, tunasema biashara hiyo inalipa lakini kama wateja hawapo tunasema biashara yako hailipi. Kwahiyo, kuendelea kwa biashara yako ni
wateja. Kwenye biashara kuna aina mbili za wateja, ambao ni wateja wa zamani na wateja wapya. 

Kwa jinsi hali ilivyo huku mitaani kwetu, ni kwamba wafanyabiashara wengi wanajali zaidi wateja mpya. 

Mteja mpya anaonyeshwa kila aina ya upendo kiasi cha kumkatishatamaa mteja wa zamani endapo ikitokea wote wawili wakawepo pamoja eneo la biashara. 

Hali hii ya kutengwa kama mteja wa zamani imenitokea mara nyingi na kunifanya niamini kwamba kadiri unavyozidi kununua bidhaa mara nyingi kutoka kwa mfanyabiashara fulani ndivyo anavyoacha kukujali. 

Kiashiria mojawapo ni wakati mwingine mteja wa zamani anapouziwa vitu kwa bei tofauti na Yule mteja mpya. Yaani ni ajabu wateja wapya wanapunguziwa wakati wale wa zamani wanaonunua vitu mara kwa mara wanapandishiwa bei. 

Wakati mwingine baadhi ya wafanyabiashara wanakupunja wewe mteja wao wa zamani kupitia vipimo hasa kwa bidhaa kama sukari, nyama, mchele n.k. 

Ukweli ni kwamba, mteja wa zamani ni LULU. Unapashwa kumtengenezea mazingira rafiki kwa kuhakikisha unampatia unafuu kadiri mtakavyozidi kukaa pamoja kibiashara. Ikiwa utazidi kumjali na yeye atazidi kuwa na sababu ya kuendelea kuwa mteja wako daima. 

Kwanini mteja wa zamani? 

Ukizidi kuwajali wateja wa zamani inakusaidia wewe kupata wateja wapya kwa gharama kidogo sana; kuliko ambavyo ungewatafuta wewe mwenyewe moja kwa moja. 

Mteja wa zamani ni mtaji mkubwa” endapo utakaanaye vizuri, na hii nikutokana na ukweli kwamba, anaouwezo wa kukuletea wateja wapya kila mara. 

Mteja wa zamani ni rahisi kumtunza kuliko kupata mteja mpya. 

Sisi wataalamu wa masuala ya masoko tunasema kuwa gharama za kumpata mteja mpya ni mara saba zaidi ya gharama za kukaa na mteja wako wa zamani. 

Mteja wa zamani tayari anakufahamu kwahiyo, akiambiwa juu ya mali mpya hana mud sana wa kuhoji kwasababu tayari anakuamini na hivyo ataweza kuitikia haraka. 

Uzoefu wangu unaonyesha kuwa inachukua muda na nguvu nyingi kumshawishi mteja mpya kukubali bidhaa yako kuliko wa mteja zamani. 

Tayari wewe unafahamu vizuri tabia na mahitaji ya wateja wako wa zamani, kwahiyo inakuwa rahisi kujua namna nzuri ya kutengeneza mkakati wa kuongeza mauzo yako bila kusahau kuwapa kilicho bora. 

Nifanye nini kukuza uhusiano na wateja wangu wa zamani? 
Unachotakiwa kufanya ni kujifunza jinsi ya kujenga na kuimalisha mahusiano na watu hasa wale wanaokuja kununua bidhaa na huduma mbalimbali kutoka kwako. 

Ni muhimu sana kujenga mahusiano ya karibu na kila mteja mpya wakiwemo wale walioletwa na mteja wako wa zamani, lakini jenga uhusiano na kila mmoja peke yake siyo kama kikundi. 

Katika mchakato wa kujenga uhusiano na wateja fanya yafuatayo; 

Badili tabia yako juu ya mahusiano: Tabia yako ya mahusiano na watu wengine ni muhimu sana. Usidhani suala zima la kujali watu litatokea tu siku moja, lazima uzame ndani kwenye tabia yako kwanza. 

Andaa orodha ya majina na namba za simu: Jiwekee utaratibu wa kuwa na orodha ya majina pamoja na namba zao za simu. Ukiwa na orodha ya majina ni rahisi kuwa na kumbukumbu ya nani kanunua nini na kiasi gani mwaka mwezi au mwaka huu. 

Inapofika sikukuu maalum kama Krismas hawa ndio wa kuwapa kipaumbele unapotuma salam za pongezi. Sijui wewe kama uliwahi kumtumia mtu heri ya krismas kwasababu tu ni mteja wako mzuri..kama hujafanya hivyo basi jitafakari na uchukue hatua. 

Toa elimu juu ya bidhaa/huduma: Hakikisha wateja wako wanapata elimu bora juu ya matumizi sahihi ya bidhaa zako, ili waweze siyo tu kununua bali kueneza habari njema kwa wateja wengine. Kadiri utakavyozidi kuwaelimisha ndivyo utakavyozidi kuzalisha wateja wengi ambao ni waaminifu. 

Shirikiana nao shughuli za kijamii: Jaribu kuwa nao karibu kwenye shughuli za kijamii; kama ni kuchangia harusi fanya hivyo, hawa ndio unatakiwa kuwachangia, kama ni misiba hawa unalazimika kuwatembelea na kuwafariji. 

Kwahiyo, kupitia mahusiano yako na wateja, unajikuta umejenga kundi kubwa la marafiki na ndugu mlioshibana. 

Bahati mbaya sana wengi tunashiriki zaidi shughuli za kijamii kwa watu ambao hawana uhusiano wowote na biashara zetu. 

Unahitaji kuwaongeza kwenye orodha wateja wako, ili linapofika suala zima la kushirikiana katika shughuli za kijamii, nao wawe ni sehemu ya watu unaowakumbuka. 

Toa tuzo kwa wateja: Kama unachukua kumbukumbu za wateja vizuri ni rahisi kwako kuona nani amechukua pesa zake kwa wingi kwa katika kipindi cha mwezi, robo, nusu mwaka au mwaka mzima. 

Hapa utakuwa na nafasi ya kujua ni nani umpe tuzo. Tuzo hiyo siyo lazima uwambie, unaweza ukatafuta utaratibu wa kumpongeza au kumpa tuzo. 

Mafano; kutoa mwaliko wa chakula cha jioni au kinywaji nyumbani au hoterini; unaweza kutuma salam za pongezi mfano kupata mtoto, kumaliza shule kwa watoto n.k. 

Wewe uliye na biashara yoyote tambua kuwa unahitaji kuendelea kujifunza mpaka ufike sehemu uone kwamba wateja ndio ndugu namba moja. 
 
KWA   KUJIFUNZA   KWA  MAPANA  NA   MAREFU    JIUNGE  NA   "  DARASA   ONLINE "   KWA  KUWA  MWANACHAMA.
Tuwasiliane  kwa  WhatsApp  + 255 716924136  /   + 255 755  400128  + 255  688  361  539

Ndimi  RAFIKI   NA   KOCHA   MWL.  JAPHET  MASATU , 
DAR  ES  SALAAM , TANZANIA.

 

No comments:

Post a Comment