Sunday, August 30, 2020

JINSI YA KUJIJENGEA NIDHAMU NA UDHIBITI WA FEDHA.

Kila pesa inayopita kwenye mikono yako ni mbegu, ambayo ukiitumia vizuri itakuwa na manufaa kwako. Lakini wengi wamekuwa hawana nidhamu na udhibiti mzuri wa fedha zao. Hapa kuna hatua za kuchukua kwenye kujijengea nidhamu na udhibiti wa fedha zako.

1. Nenda kwenye benki unayotumia sasa na fungua akaunti maalumu ambayo unaweza kuweka fedha lakini kutoa siyo rahisi au kuna ukomo. Karibu kila benki ina akaunti ya aina hii.

2. Omba huduma ya fedha kuhamishwa kwenye akaunti yako ya sasa ambayo ndiyo inaingiza kipato chako kikuu, iwe ni mshahara au fedha unazoweka akiba. Kwamba kila mwezi kuna kiasi watakikata kwenye akaunti yako ya akiba kwenda kwenye akaunti yako maalumu.

3. Weka akiba kwenye akaunti hiyo maalumu kila mwezi, bila kuigusa kwa angalau mwaka mmoja. Jiwekee kiwango cha kipato chako ambacho kitaenda kwenye akaunti yako, unaweza kuanza na asilimia 10 au nyingine itakayokufaa wewe.

4. Hakikisha kipato chako kinakatwa kabla ya matumizi, kama unafanya shughuli zako binafsi basi unapolipwa, kabla hujaanza kutumia weka kwanza pembeni kiasi cha akiba na kiweke kwenye akaunti hiyo.

5. Pesa iliyo kwenye akaunti hiyo maalumu isahau kabisa, chukulia kama ulinunua kitu fulani na hivyo usiiweke kwenye mahesabu. Ni mpaka mwaka uishe ndiyo utarudi kwenye fedha hiyo na kuchagua ufanye nayo kitu gani cha kuzalisha zaidi.

Zoezi hili linakulazimisha kujiwekea akiba na baadaye kuiwekeza, kitu ambacho kitakuweka vizuri kwenye eneo la fedha.



 

No comments:

Post a Comment