Monday, August 31, 2020

KUJIJENGEA NIDHAMU NA UDHIBITI WA MUDA.

Tambua muda ndiyo rasilimali yenye uhaba, ambayo ukishapoteza hairudi tena. Katika kujijengea nidhamu na udhibiti wa muda, fanya yafuatayo;

1. Chukua kalamu na karatasi, gawa karatasi yako katika pande mbili, A na B.

2. Upande A orodhesha mambo yote ambayo umefanya kwenye wiki moja iliyopita, kila ulichofanya kiorodheshe, uliingia mtandaoni, orodhesha, uliangalia mpira, weka, ulibishana na watu weka.

3. Upande B orodhesha malengo na mipango uliyonayo, kile unachotaka kufikia ndani ya mwaka mmoja, miaka 5, 10 na mpaka 20 ijayo.

4. Linganisha orodha A na B, piga mstari kile ulichofanya upande A ambacho kinakusaidia kufikia upande B.

5. Baada ya hapo, chukua yale ya upande A ambayo yana mchango kwenye upande B na hayo tu ndiyo utakayoanza kuyafanya kuanzia sasa. Yale mengine uliyokuwa unafanya na hayana mchango kwenye kufikia malengo na mipango yako, achana nayo mara moja.

Yaani jiambie tu kuanzia leo sifanyi tena haya, na acha mara moja. Vitu kama kufuatilia habari, kubishana, mitandao ya kijamii na mengine utapaswa kuachana nayo mara moja.

Manufaa ya zoezi hili ni wewe kupata muda mwingi zaidi wa kufanya yale ambayo ni muhimu zaidi kwako. Na hapo hutakuwa tena na tatizo la muda.


 

No comments:

Post a Comment