Saturday, July 18, 2020

NO GAINS WITHOUT PAINS---HAKUNA FARAJA / FURAHA / FAIDA BILA MAUMIVU

Mpendwa msomaji wa MAISHA NA  MAFANIKIO  BLOG (  LIFE  AND YOU) , napenda nianze kwa kusimulia jinsi nilivyokosa FARAJA kwa kuandika makala hii: 
“Leo nimeamka usiku saa tisa na nusu, na tayari nimeanza kuandika makala hii ambayo upo unaisoma. Lakini NIMEKOSA FARAJA kutokana na uwepo wa mbu wengi wanaonisumbua sana, achilia mbali hatari ya kuambukizwa ugonjwa wa malaria. Niko tayari KUKOSA FARAJA, kwasababu ni kwa njia hii nitaweza KUPATA FARAJA kama ambavyo imekuwa ikitokea pale wasomaji wa mtandao wa MAISHA  NA  MAFANIKIO BLOG ( LIFE  AND  YOU ) wanaponitumia ujumbe kuwa makala zangu zina mchango mkubwa kwenye maisha yao”. . 
Kisa hiki cha mbu walionisumbua kinatuonyesha kwamba, FARAJA ni kitu kizuri sana kwa binadamu na kwa wengine ni kichocheo kikubwa kwao kufanya kile wanachokifanya. 

Niseme tu, FARAJA ni ile hali ya kujisikia vizuri na huru kutoka kwenye maumivu, matatizo au msongo wa mawazo. 

Ukweli ni kwmba watu wengi wanapenda FARAJA. Matokeo yake FARAJA imekuwa ni kizingiti kikubwa katika kuyafikia maisha ya mafanikio na utajiri. 

Watu wengi wemejikuta wakishindwa kuchangamkia fursa kwasababu fursa nyingi ambazo ni kubwa zinakutaka huwe tayari kukosa FARAJA kwa muda Fulani ndio upate tena. 

Kutokana na tabia hiyo ya kupenda sana FARAJA, wengi wamejikuta wakifanya vitu vidogo vidogo sana na vya kawaida ILIMRADI tu haviwaondoi kwenye FARAJA yao ya awali. 

Ni vizuri kutambua kwamba FARAJA endelevu itapatikana kwa wale ambao wako tayari kukosa FARAJA kwa muda. 

Ukweli ni kwamba, vitu vingi vyenye kuleta FARAJA ENDELEVU vinafanyika katika mazingira ya kukosa FARAJA. 

Mfano ukitaka kuwa na afya nzuri, lazima uwe tayari kuacha kula vyakula Fulani hata kama ni vitamu sana, lazima uwe tayari kupunguza sukari, lazima kuamka mapema na kufanya mazoezi—hapa lazima uwe tayari kukosa raha ya usingizi wa asubuhi n.k, 

Wengi wetu katika kusaka mafanikio huwa tunapenda njia iliyonyooka. Martin Luther King aliwahi kusema kuwa;
“Kipimo kizuri cha binadamu siyo mahali aliposimamia wakati wa FARAJA, bali pale anaposimamia wakati wa changamoto na ubishani.”
Binadamu tuna tabia ya asili ya kuegemea zaidi kwenye HADHI tuliyonayo na tunapinga kile tusichokijua, ili tuweze kuendelea kukaa na FARAJA yetu. 

Tabia ya kupenda FARAJA inafungamana na tabia ya mababu zetu ya kuhofia kuhatarisha maisha. Tunaogopa kujaribu vitu vipya. Tunataka tukwepe mabadiliko. 

Kwahiyo, hatujisukumi mbele kwenda katika kiwango kingine cha maisha mazuri. Katika dunia ya sasa ya usumbufu na inayobadilika kwa kasi, inasaidia wewe kubadilisha mahusiano yako na mabadiliko na kuwa tayari kufurahia KUKOSA FARAJA. 

Wengi tunafikiri maisha ni kutafuta ulinzi na usalama na FARAJA peke yake. 

Hivi vitu ni muhimu na ni sehemu ya maisha ya kila siku, LAKINI maisha yamejaa RAHA na MAUMIVU, KURIDHIKA na KUTESEKA, URAHISI na UGUMU. 

Kwa kuangalia tu! upande mmoja wa sura ya FARAJA, tunajitenga na safu kamili ya uzoefu wa maisha ya binadamu—na maarifa, ujuzi na huruma itokanayo na upande mwingine wa (KUKOSA FARAJA). 

Kama haujisikii vizuri KUKOSA FARAJA, bilashaka huwa unakaimbia mabadiliko. Katika dunia ya sasa, huwezi kukimbia mabadiliko! 

Kila kitu kiko katika hali ya kubadilika mara kwa mara. Ngozi yetu ubadilika, majani ubadilika, watu ubadilika. Kwahiyo suala la kubadilika linatokea kila mahali muda wowote. 

Kuishi kikamilifu, lazima uwe tayari kukanyaga kwenye visivyojulikana, sasa hivi kuliko siku zote. Mfumo wetu wa kufanyakazi kidigitali na utandawazi unakuhitaji kufanyiakazi hata vile usivyojulikana pale unapoanza. 

Lazima uwe tayari kujipa changamoto ili kukua na kubadilika. Na mabadiliko huwa yana harufu ya KUKOSA FARAJA kwa wengi wetu. Woga na wasiwasi na kukosa FARAJA ni asili ya mapambano ya kimaisha kwa binadamu. 

Kujifunza namna ya kuwa na FARAJA kwa KUKOSA FARAJA, pengine ni mojawapo ya somo muhimu sana ambalo nimejifunza kama mjasiriamali. 

Anza leo kujiandaa na uzoee wakati Fulani KUKOSA FARAJA ili kupata FARAJA ENDELEVU hasa wakati huu unapoanza safari yako ya mafanikio. 

Kuendelea kujipatia ujuzi na maarifa juu ya pesa, kazi, biashara, ujasiriamali, afya, uongozi na suala zima la uchumi wa kaya; jaribu kuendelea  kusoma  na  kujifunza  katika  MAISHA  NA  MAFANIKIO  BLOG ( LIFE  AND  YOU )

No comments:

Post a Comment