Thursday, July 9, 2020

JE , WAHITAJI KUFIKIA NDOTO ZAKO ? FANYIA KAZI MAMBO HAYA :--


Kila mtu anatamani kuzifikia ndoto za maisha yake ya mafanikio. Kwa sababu hiyo kila mtu huchukua hatua anazoziona yeye zinamfaa ili kutimiza malengo hayo. Je, ni wangapi wanajua kuwa huwa wanachukua hatua sahihi au la.?
Katika makala haya, ni lengo langu ni kukumbusha wewe, mambo ya msingi na kama utayazingatia mambo haya yatakusaidia wewe kuweza kukufikisjha kwenye ndoto zako za mafanikio. Je mambo hayo ni yapi?


1. Andika malengo yako.
Najua malengo yako unayajua vizuri tu, lakini kuna sababu muhimu sana kwa wewe kuyaandika malengo yako tena. Chukua kalamu na karatasi, na andika vitu vyote unavyotaka kuvifikia kwenye maisha yako.
Fikiria juu ya kitu ambacho unataka kufanya au unahitaji kukifanya. Inaweza kuwa kitu chochote kama malengo ya afya au malengo ya biashara yako. Orodhesha vitu vingi iwezekanavyo, lakini viwe vile unavyotaka kuvifanikisha.

2. Weka vipaumbele vya malengo yako.
Ndio, najua umeandika malengo mengi, lakini ukweli ni kwamba huwezi kuyatimiza yote. Ili uweze kuyafikia malengo hayo,  yagawawe kwa kuzingatia vipaumbele. Unapaswa kujua, malengo yapi uanze nayo na yapi uyaache.
Kwa kuweka vipaumbele itakupa nguvu wewe, ya kuweza kuyafikia malengo yako kwa urahisi. Na ukishaweka vipaumbele, usibabaishwe na malengo mengine yatakayotokea hapa katikati, vipaumbele vyako vinatosha, vitekeleze kwanza.

3. Vunja vunja malengo yako.
Vunja kila lengo kuwa dogo ambapo unajua unaweza kutimiza kwa urahisi. Hakikisha pia unajipa muda wa wewe kutekeleza malengo yako kulingana na wakati uliokadiriwa wa mradi huo uliojiwekea.
Kwa mfano, ikiwa lengo lako ni kusoma kitabu. Usijilazimishe kusoma kurasa mia moja, kwa mara moja, soma kurasa chache na zielewe. Fikiri kama unataka kujifunza kuogelea, je! Ungeingia ndani ya bahari au ungeanza kwanza kujifunza katika dimbwi?

4. Amua kuwajibika.
Lengo kuu ni kuishi maisha bora ya kufikia malengo yetu na kufanya hivyo lazima tuchukue hatua moja kwa wakati mmoja na kwa hiyo tunahitaji msimamo thabiti. Je! Unahakikisha vipi malengo yako yanatimia?
Hapa hakuna ujanja, unatakiwa kuwajibika. Fanya kila linalowezekana kwa wewe kuamua kuwajibika ili kuhakikisha malengo yako yanatimia. Ukikubali kuwajibika nakupa uhakika unaweza kufanikiwa na kufika mbali kimafanikio.
Fanyia kazi mambo hayo na hakikisha unachukua hatua kuona ndoto zako zinatimia.

No comments:

Post a Comment