Thursday, July 9, 2020

JINSI YA KUENDANA NA MABADILIKO YA KIDUNIA YANAYOTOKEA KILA SIKU.


Wakati mwingine unapaswa kuelewa kwamba kile ambacho unakijua leo baada ya miaka mitano ijayo kinaweza kisiwe na faida tena au kinaweza kisilete matokeo yale ambayo mwenyewe unayapata kwa sasa. Nimesema hayo kwa sababu kwa hivi sasa mambo yanabadilika sana.

Ile dunia ya jana si dunia ya leo. Mambo kila kukiacha yanabadilika sana, watalamu nao hawalali kutwa wanaumizwa vichwa vyao kuweza kugundua mbinu mpya ambazo ni rahisi kwa mwanadamu kuweza kumrahisishia kazi mbalimbali.
Kama nilivyosema hapo awali kwamba dunia inakwenda kasi hivyo  ili kuendana sawa na mabadiliko hayo ni kwamba hata wewe unapaswa kubadilika pia. Na njia pekee ambayo itakayokusaidia kwa namna moja ama nyingine kuwa bora zaidi kwenye kila eneo unalofanyia kazi ni kwamba unatakiwa kujiimarisha wewe mwenyewe kila siku.

Na njia pekee itakayokusaidia kuweza kujiimarisha ni kwamba unatakiwa kuhakikisha kwamba unaenda na mabadiliko yanayotokea kila siku, ni  kujifunza mambo mapya kila wakati kwa sababu usipojifunza mambo mapya ni kwamba utapitwa na vingi.

Ni muhimu kuelewa kwamba kwenye kila sekta unayoifanyika kazi unapaswa kujifunza namna ambavyo utakuwa bora  kila wakati.  Kumbuka kujifunza hakuna mipaka hivyo ni muhimu sana kwako kuweza kujifunza mambo mbalimbali yatakayokusaidia kwa namna moja ama nyingine kuwa bora zaidi kwenye kile unachokifanya kila wakati kwani pindi utakaposhindwa kufanya hivyo ni kwamba hata wewe utapitwa na utashindwa kuendana na kasi ya mabadiliko ya kidunia yanayotokea.

Kwa muktadha huo, unapaswa kila wakati uwekeze muda mwingi kwenye kujifunza vitu vipya kila siku. Kama wewe ni mkulima basi ni  jifunze mbinu mpya kila siku zitakazokuwezesha kufanikiwa zaidi katika kilimo hicho, kama wewe ni mtalamu wa jambo fulani basi yakupasa kuweza kujipambanua zaidi kwa kujiwekeza kwenye kupata maarifa sahihi juu ya jambo hilo.
Ni muhimu kupata maarifa fulani kila  wakati  kwa sababu kwa sasa dunia inakwenda kasi sana hivyo bila kuwa na maarifa mapya ni kwamba utazidi kuwa mtu wazamani kila siku , kwani kila kitu ambacho kitakuwa kinafanywa na watu wengine kwako kitakuwa kigeni.

Mwisho naomba nitamatishe kwa kusema ya kwamba kila wakati ongeza ubobezi kwenye kila eneo unalofanyia kazi kwa sababu ubobezi humsaidia mtu kuweza kufanya jambo lililo bora zaidi, pia kila wakati unapaswa kuelewa kwamba ubobezi hupatikana kwa kuweza katika kujifunza vitu vipya kila siku ili uweze kuendana na mabadiliko ya kidunia.

No comments:

Post a Comment