BADILI FIKRA.FIKIRI TOFAUTI .BADILI MAISHA.JITAMBUE .JIFUNZE ELIMU YA SAIKOLOJIA,TEOLOJIA , FEDHA ,UTAMBUZI(SELF HELP EDUCATION),FALSAFA YA MAISHA,MAISHA NA MAFANIKIO,BIASHARA / UJASIRIAMALI.FURAHIA WASAA WAKO NA MAISHA NA MAFANIKIO BLOGU.THIS IS THE COMMUNITY CAPACITY BUILDING BLOG.ENJOY THE BLOG.STRETCH YOUR MIND. YOU CAN CHANGE YOUR LIFE FOR EVER. YOU CAN ACHIEVE EXCELLENCE.YOU CAN MAKE A DIFFERENCE.
Yapo maswali mawili muhimu sana kwa kila mtu kujiuliza kabla ya kuingia
kwenye biashara yoyote ile. Kwa kujiuliza maswali haya, utaingia kwenye
biashara ukiwa na uelewa sahihi, na ukijua ni hatua zipi sahihi kwako
kuchukua ili kufanikiwa zaidi kwenye biashara unayofanya.
(1). NI NANI MWENYE FEDHA ZANGU?
Nilishakuambia siku za nyuma kwamba hutafuti fedha bali unakusanya
fedha. Fedha unayoitaka sasa, ipo kwenye mikono ya mtu mwingine. Hivyo
hatua ya kwanza kabisa kwenye kufikiria biashara yako ni kujiuliza nani
mwenye fedha zako. Hapa unahitaji kuwajua wateja halisi wa biashara yako, watu ambao
wana shida, wana changamoto, wana uhitaji ambao unaweza kuutimiza. Pia
watu hao wana fedha ya kuweza kukulipa wewe kwa kile ambacho unawapa. Kama hujawajua watu wenye fedha zako, ukianzisha biashara utakuwa
unapoteza muda wako. Kwa sababu hata kama unaona wengine wanauza sana,
utashangaa unakaa kwenye biashara na hupati mauzo makubwa kama wengine. Kwa sababu unakua hujajua nani mwenye fedha zako na kumfuatilia huyo zaidi. Kama uliingia kwenye biashara bila kujiuliza swali hili, kaa chini
sasa hivi na jiulize nani mwenye fedha zako? Orodhesha sifa za watu
ambao wanaweza kunufaika na aina ya biashara unayofanya, na wenye uwezo
wa kulipia kile unachouza. Ukishajua kwa hakika nani mwenye fedha zako, ni rahisi kumlenga huyo na ukaweza kumhudumia vizuri na wote mkanufaika sana.
(2).JUA NI KITU GANI UNABADILISHANA NAO ILI WAKUPE FEDHA. Baada ya kuwajua wenye fedha zako, unahitaji kujua kitu gani
unahitaji kuwapa ili nao wakupe fedha walizonazo. Kwa sababu kila mtu
amepata fedha yake ka uchungu, na hivyo hataki kuipoteza. Lazima uwe na
sababu kubwa ya kumshawishi mtu akupe fedha zako. Kumbuka akishakupa
fedha wewe, hawezi tena kuitumia kwa mambo yake mengine. Hapa unahitaji kujua kwa hakika ni thamani gani unatoa kwa wateja wa
biashara yako. Hapa unahitaji kujua kwa hakika ni mahitaji gani
waliyonayo wateja wako ambayo unayatimiza, ni maumivu gani ambayo
unayatuliza. Kama huna sababu ya kutosha, ya kumshawishi mteja akupe fedha yake
aliyoipata kwa shida, hutaweza kufanikiwa kwenye biashara yako. Kwa sababu kumbuka mteja hanunui kwa sababu wewe unauza, wala hanunui
kwa sababu anakuonea huruma. Bali mteja ananunua kwa sababu ana
uhitaji, ana maumivu ndani yake ambayo hawezi kuendelea nayo na kuna mtu
amemshawishi kwamba ana kitu cha kutimiza mahitaji yake au kutuliza
maumivu yake. Hivyo baada ya wewe kujua ni nani mwenye fedha zako, jua maumivu yake
ni yapi, kisha mweleze jinsi kile unachouza kinavyoweza kutuliza
maumivu aliyonayo.
Ili kufanikiwa huhitaji kufanya kila kitu au kujua kila kitu. Badala
yake chagua eneo lako ambalo unaweza kufanya vizuri, kisha kazana
kufanya vizuri, kuwa bora kuliko wengine wote na utaweza kufanikiwa
zaidi. Kadiri unavyochagua vizuri eneo lako na kuweka juhudi kubwa,
ndivyo unavyotumia nguvu zako na umakini wako vizuri.
Jifunze kutofautisha kati ya mawazo na mawazo mazuri, bidhaa na bidhaa
bora, uwekezaji na uwekezaji mzuri. Asilimia 90 ya vitu vyote
unavyokutana navyo, siyo muhimu, yaani ukiachana navyo hutakosa
chochote. Ni asilimia 10 tu ndiyo muhimu, jua hiyo asilimia kumi na
ukazane nayo huku ukipuuza mengine yote.
Kuwa na kiasi, haijalishi umefanikiwa kiasi gani, miaka 200 ijayo,
huenda hakuna atakayejua hata kama uliishi hapa duniani. Kila unapoanza
kujiona wewe ni muhimu kuliko wengine, kumbuka kitakachotokea miaka 200
ijayo, dunia itakuwa imekusahau kabisa. Ishi maisha yenye maana kwako na
siyo maisha ya kujionesha na kutaka wengine waone wewe ni muhimu kuliko
wao.
Kuna orodha nyingi za watu waliofanikiwa, kuanzia ndani ya nchi mpaka
dunia nzima. Lakini jinsi mafanikio hayo yanavyopimwa inaweza isiwe
sahihi kwako. Mafanikio ya kweli kwako ni mafanikio ya ndani yako,
ambayo siyo rahisi kupimwa kwa nje. Mafanikio ya ndani utayapata kwa
kuweka juhudi kwenye yale maeneo uliyochagua, kuweka umakini wako kwenye
mambo yaliyo ndani ya uwezo wako na kuachana na mengine yote. fedha,
madaraka na umaarufu ni vitu vya nje, ambavyo huwezi kuvidhibiti,
unachoweza kudhibiti ni hatua unazochukua. Kazana kuwa bora kila siku na
weka juhudi zaidi kwenye kile ulichochagua kufanya.
Mzazi ana nafasi kubwa sana katika kuendeleza kipaji cha mtoto
Kipaji ni uwezo wa
kuzaliwa nao wa kufanya jambo fulani kwa ngazi ya juu bila kufundishwa
au baada ya kufundishwa kidogo tu. Kipaji kinaweza kuwa cha kimwili au
cha kiakili lakini pia kinaweza kuendelezwa au kudumazwa.
Mzazi ni
mtu wa kwanza anayeweza kutambua uwezo ama kipaji cha mtoto wake. Hata
hivyo ana fursa ya kuendeleza au kutokukiendeleza kipaji cha mtoto.
Baadhi
ya wazazi hutambua vipaji vya watoto mapema na kuanza kuviendeleza kwa
kuwapatia nyenzo mbali mbali ambazo huwasaidia katika kuboresha uwezo
walio nao.
Lakini pia wapo wazazi ambao wanamalengo yao juu ya ni
kitu gani wanapenda watoto wao wafanye. Ama yamkini hawana ufahamu wa
nini cha kufanya ili kumwendeleza mtoto mwenye kipaji .Hata hivyo vipo
baadhi ya vipaji ambavyo wazazi huona ni upotevu tu wa maadili mfano
kuimba na kucheza mziki.
BBC imezungumza na mama Ritha, mama mwenye watoto wanne. Anasema
kwa kiasi kikubwa baadhi ya wazazi na hata yeye mwenyewe kipindi cha
nyuma walikwamisha sana watoto sababu walikuwa hawatambui kama kipaji
pia ni njia salama ya kumwezesha mtoto kimaisha. "Wazazi wengi
huwa hawajuagi tena zamani tulikuwa tunaona watoto wanapotea kabisa. Mi
binti yangu wa kike alikua anapenda kuandika nyimbo za wasanii wa
marekani na hata za kwake mwenyewe kwenye daftari lake afu kukiwa na
sherehe yeye ndo mwimbaji. Nikaona anapotea nlikua na mchapa na
nlimwambia akifika chuo kikuu ndo afanye uo mziki lakini si nyumbani
kwangu maana hata baba yake alikuwa hapendi kabisa," Mama Ritha
anaiambia BBC Hata hivyo ameongeza kuwa wazazi pia huwanyima fursa
za kujifunza watoto kwani kila akishika kitu mzazi hupiga kelele mtoto
aache kwa madai kwamba ataumia. Hata hivyo wapo baadhi ya watoto ambao wamepewa msaada mkubwa na wazazi wao katika kuboresha na kuendeleza vipaji vyao.
BBC imezungumza na mwanadada mpambaji Plaxeder Jumanne au baby
precious kama anavyojulikana katika kazi zake za upambaji, anasema mama
yake ndio mtu wa kwanza kumshauri ageuze kipaji chake kuwa biashara huku
akimnunulia vifaa orijino vya urembo.
"Mie nlikuwa nawachukua
watoto wenzangu nawapamba nlikua napenda sana urembo kama mama yangu.
Hata nilipo kuwa nikaanza kuwapamba watu. Nilikuwa natumia vifaa feki
hivi vya bei rahisi lakini mama yangu alianza kwa kuninunulia vifaa
orijino kabisa. Na huwezi amini nilikua nampamba yeye na kumfuta kabla
sijapata wateja tena nimejifunza kufunga maremba ya kinaijeria kichwani
kwa mama na alikuwa ananisaidia sana, sasa hivi nasafiri hadi mikoani na
kupamba watu mbali mbali hadi watu maarufu na nimepata pesa nikanunua
vifaa vingi sana Orijino," Plaxeda anaiambia BBC.
Hata hivyo
manadada huyo anasema kwa sasa mama yake ametangulia mbele za haki tangu
mwaka jana ila bado anamshukuru kwa sababu hivi sasa kazi ya upambaji
inampa pesa kuliko ajira yake na imemwezesha kufungua biashara zingine.
"Mimi
sijajitangaza sana ila kupitia vifaa alivyonianzishia navyo mama yangu
nikawa napamba hadi maharusi na wasimamizi wao. Na kipaji hiki kimenipa
pesa ninafanya biashara ya kutengeneza nywele hasa mawigi na pia
kufungua biashara ya nguo. Mama yangu angekuwepo angefurahi sana ila
naamini anaona. Nimewaremba baadhi ya wasanii wa Tanzania. Safari ndo
inaanza," Plaxeder anaiambia BBC.
Mwanaharakati wa masuala mbali mbali ya kibinadamu Shahista Alidina
maarufu kama Shaykaa, anasema baadhi ya wazazi hupenda kutimiza ndoto
zao kupitia watoto na mwishowe huwakwamisha.
"Unakuta mzazi kama
alishindwa kuwa mwanasheria au daktari kama alivyotaka huko nyuma
atataka mtoto wake afuate ndoto hiyo. Hawataki kuwapa uhuru watoto
wafuate wanavyopenda. Unakuta kipaji cha mtoto kinaweza mletea kipato
cha kutosha tu ila mzazi anampa mtoto shinikizo la kufaulu tu shule awe
namba moja, mbili au tatu na ndiomaana unaona watoto wengine hadi
wanajiua. Wanawanyima fursa watoto kufanya vitu wanavyovipenda," Shaykaa
anaiambia BBC.
Hata hivyo anaongeza kuwa kunachangamoto nyingine
kwa wazazi kupangia kazi watoto kuwa hii ni ya wanawake au hii ni ya
wanaumena kujenga uoga kwa watoto na kuwanyima fursa ya kujituma zaidi.
"Kusoma
kwa mtoto ni muhimu ila kuna muda wa ziada na kuna maisha nje ya
darasa. Unakuta mtoto wa kike anapenda kucheza mpira, lakini mzazi
atapinga kuwa huu ni mchezo wa wanaume mwanamke hatakiwi, sasa hapo moja
kwa moja mzazi atakuwa ameua kabisa kipaji cha mtoto kama mtoto atakosa
fursa ya kujiendeleza huko mbele," anasema Shaykaa Mwanaharakati huyo pia amewaasa wazazi kuhakikisha wanawasaidia watoto kujiendeleza kijamii.
"Mtoto
ni muhimu awe na maisha yake pia, na tutambue kuwa na wao ni binadamu
wala si wafungwa. Ni muhimu ndio kufuata dini na misingi bora ya maisha
pamoja na mila na desturi lakini tusisahau kuwa mtoto anapofikia umri wa
kujielewa anahaki ya kufanya maamuzi kuwa anapenda nini ilimradi ni
jambo jema kisheria, kidini, kiafya na kijamii. Tuwe marafiki kwao
lakini tusiwapotoshe watoto wetu, Shaykaa anaiambia BBC.
Simu yaweza kumsaidia mtoto kujifunza lakini bado nimuhimu kwa mzazi kuwa makini
Hivi karibuni
imekuwa kawaida sana kumkuta mtoto anatumia simu ya mkononi ya mzazi
wake na mara nyingine wanatumia bila hata kupata ridhaa ya mzazi
mwenyewe.
Baadhi ya watoto huonyesha utaalamu wa hali ya juu katika kufungua kurasa mbalimbali za simu hizo.
Na inadaiwa kuwa kuna watoto ambao huwa wanajifunza mambo mengi kupitia simu za mkononi. Hata
hivyo si wazazi wote ambao hukubali simu zao zitumiwe na watoto, baadhi
huwa wakali na kuweka kila aina ya nywila ingawa wengine huwa hawaoni
shida kuwapatia watoto wao simu punde tu wanaporejea kutoka kwenye
majukumu yao ya kila siku.
Baadhi ya wazazi huwa wanaona kuwa simu ndio njia pekee inayoweza
kuwafanya watoto wao watulie na wao wapate muda wa kupumzika ama hata
kufanya shughuli zao za nyumbani.
Je,kuna faida yeyote endapo mtoto atatumia simu? BBC
imezungumza na baadhi ya wazazi ili kufahamu ni kwa kiasi gani watoto
wao hutumia simu zao na wanawadhibiti vipi vitu anavyoangalia mtoto?
"Kwa
kweli simu yangu hata sina uhuru nayo huwa nikifika tu nyumbani wanangu
huwa wananipokea kwa mbwembwe zote na cha kwanza kubeba ni simu na
nikihitaji lazima niwaombe wao. Simu ikiita utakuta wao ndio
wanapokea,mara nyingi wanaangalia video za kartoon au za watoto wenzao
zilizopo you tube," Mama Brian anaeleza
Baadhi ya watoto hutambua hadi nywila za simu za wazazi wao
Alex Kayetta ambaye ni baba wa mtoto mmoja, anasema simu yake huwa haimiliki punde tu anapofika nyumbani , "Mwanangu
akishashika simu yangu yani kuipata lazima nimbembeleze, na akichukua
mara nyingine huwa lazima nimtafute alipo ,kuna siku nilimkuta amejificha
ndani ya beseni akicheza michezo ya kwenye simu'game' nikampiga
picha".
Freddie Kyara ni mwanasaikolojia kutoka nchini Tanzania
ambaye anaeleza kuwa hali hii huwa inafanana na jinsi mzazi anapokua
kwenye simu muda mrefu na hupoteza fursa ya kuwa karibu jamii na ndivyo
hivyo inavyotokea kwa mtoto.
Na kwa upande wa mtoto kutumia simu huwa kuna madhara pia "Kukua kwa
mtoto kunahitaji awe na mbinu za kijamii, kama vile kucheza na watoto
wenzake na kujifunza mambo mbalimbali kutoka kwa wenzake, lakini siku
hizi unaweza kukuta mtoto anashindwa kucheza na watoto wengine kwa
sababu amezoea yeye rafiki yake ni simu tu.
Ubunifu wa mtoto
unaweza kupungua. Sisi wakati tunakuwa hatukuwa tunajua habari za simu,
ilikuwa ni kucheza mpira na kujishughulisha na shughuli mbalimbali za
nyumbani na hali hiyo ilitufanya tuweze kujenga urafiki na watu na kujua
tabia za watu tofautitofauti.
Mtoto anaweza kujifunza pia kwenye
simu lakini lazima uthibiti uwepo kwa sababu sio kila kilichopo kwenye
simu kina maudhui mazuri kwa watoto na wanapaswa kutengewa muda" Kyara
,mtaalamu wa saikolojia alieleza.
Hata hivyo jumbe mbalimbali zimekuwa zikisambaa kuonya madhara ya
mionzi ya simu kwa watoto wadogo na kudai kuwa umri sahihi wa kupewa
simu ni kuanzia miaka kumi na sita. Jambo ambalo Daktari Fredrick
Mashili anasema madhara ya namna hiyo huwa inategemeana zaidi na umri wa
mtoto japo kwa upande mwingine macho yanaweza kupata shida ingawa
hakuna ushahidi wa kutosha kuthibitisha madhara hayo ya mionzi.
"Kuna
wasiwasi kwamba mtu akianza kutumia simu mapema anaongeza muda wa
kuyashughulisha macho yake katika mionzi kwa muda mrefu zaidi kitu
ambacho si kizuri kwa afya ya macho," Dkt.Mashili alieleza.
Linapokuja swala la fedha, kila mtu ana namba na viwango vyake. Kwa
sababu tunatofautiana ndoto, kazi/biashara, kipato, mitindo ya maisha na
hata mazingira, matokeo yetu ya kifedha hayawezi kulingana.
Hivyo kujipima hatua ulizopiga kifedha kwa kuwatumia wengine ni
kujiumiza na hata kujirudisha nyuma, kwa sababu kuna namba nyingi ambazo
utakuwa huzijui kuhusu wengine. Kwa mfano unaweza kumwona mtu kwa nje
anaonekana kuwa na vitu vinavyoashiria ana fedha nyingi, lakini kumbe
vitu vyote hivyo amepata kwa mkopo ambao ataulipa maisha yake yote. Pia unaweza kumwona mtu ukafikiri hayupo vizuri kifedha kwa mwonekano
wake wa nje, kumbe anafanya uwekezaji ambao baadaye utamwezesha kufikia
uhuru wa kifedha.
Kwa kuwa ni vigumu kupima hatua ulizopiga kifedha kwa kuwatumia watu wengine, unahitaji kujitumia wewe mwenyewe.
Kiasi cha fedha unachotoa kwa wengine bila ya kutegemea kupata
chochote ni kiwango kingine muhimu sana cha kupima afya yako kifedha na
kujua hatua ulizopiga. Kwa kadiri unavyotoa zaidi ndivyo unavyoonesha
kwamba unaitumia fedha na siyo fedha inakutumia wewe.
Unahitaji kuwa na utaratibu wa kutoa fedha kuwasaidia wengine bila ya
kutegemea kulipwa fedha hizo. Kwa sababu tunatoshelezwa zaidi na utoaji
kuliko upokeaji.
Pia unapotoa fedha kwa wengine, unatengeneza pengo ambalo itabidi
lizibwe, hivyo unakuwa umejiweka kwenye nafasi ya kuongeza kipato chako
zaidi.
Hichi ni kiwango kinachoonesha maandalizi yako uliyonayo sasa kwa
upande wa fedha. Kadiri unavyokuwa na akiba kubwa kifedha, ndivyo
unavyoweza kujilinda na dharura mbalimbali zinazoweza kukutokea. Akiba
unayokuwa nayo ndiyo itakukinga usiingie kwenye madeni mabaya pale
unapokutana na changamoto ambazo hukuzitegemea.
Kiwango sahihi cha akiba unayopaswa kuwa nayo ni ile inayoweza
kutosheleza kuendesha maisha yako kwa miezi 6 mpaka mwaka mmoja hata
kama utakuwa huna kipato kabisa katika kipindi hicho.
Kuza kiwango chako cha akiba na hili litakupa pumziko na kukuondolea
wasiwasi kuhusu fedha kitu ambacho kitakuwezesha kufanya mambo yako kwa
utulivu na ufanisi mkubwa.
Kiasi cha fedha unachodaiwa na wengine kutokana na vitu ulivyonunua
bila ya kuwa na fedha ni kipimo cha maamuzi yako ya kifedha kwa siku za
nyuma. Kadiri madeni yako yanavyokuwa makubwa, ndivyo sehemu kubwa ya
kipato chako inavyoelekea kwenye kulipa madeni hayo na wewe kubaki na
kiasi kidogo ambacho hakiwezi kukutosheleza.
Unahitaji kutokuwa na deni binafsi kabisa, na madeni mazuri
unayopaswa kuwa nayo ni yale yanayojilipa yenyewe. Madeni yanayojilipa
yenyewe ni yale ambayo yanazalisha faida na faida hiyo unatumia kulipa
deni. Haya ni madeni ambayo hayakuumizi.
Lakini madeni ambayo unalipa kwa fedha zako unazopata kwenye shughuli
zako binafsi, ni utumwa ambao utakutesa kwa muda mrefu. Kama upo kwenye
madeni ya aina hii kazana kuondoka na usiingie tena ili kuepuka
kujiweka kwenye wakati mgumu kifedha.
Kiwango ambacho umekiwekeza kwenye maeneo ambayo yanazalisha riba au
faida ni kipimo muhimu kwa maandalizi yako ya kifedha ya baadaye. Kama
hapo ulipo hujafanya uwekezaji wote kwa ajili ya baadaye, kama hujawa na
maandalizi ya kukuwezesha kuingiza kipato bila ya wewe kufanya kazi
moja kwa moja, huna maandalizi ya kifedha ya baadaye, na haupo eneo zuri
kifedha.
Unahitaji kufanya uwekezaji kwa ajili ya baadaye, kwa sababu utakuja
wakati ambapo huna uwezo wa kufanya kazi kama unavyofanya sasa, lakini
una mahitaji muhimu kwa maisha yako. Unapokuwa umewekeza na uwekezaji
unazalisha, maisha yako yanakwenda vizuri.
Kiwango sahihi cha uwekezaji unachopaswa kuwa nacho ni kile ambacho
kinazalisha faida au riba ambayo inakuwezesha wewe kuendesha maisha yako
kwa kadiri ya mahitaji yako.
Watu wawili wanaweza kushindwa kwenye kitu kimoja, mmoja akachukulia
kushindwa huko kama kichocheo cha kufanya zaidi na akafanikiwa. Mwingine
anaweza kuchukulia kushindwa huko kama sababu ya kukata tamaa na
kushindwa kabisa.
Tukio ni moja, tafsiri tofauti na matokeo tofauti kabisa. Siyo kinachotokea, bali namna unavyotafsiri kinachotokea ndiyo inaleta madhara kwako. Kwenye Falsafa ya Ustoa pia kuna dhana inayoitwa upili wa udhibiti.
Dhana hii inaeleza kwamba vitu vyote vinavyotokea kwenye maisha yako,
vinagawanyika katika makundi mawili, kundi la kwanza ni vitu unavyoweza
kuviathiri, hivi vipo ndani ya uwezo wako. Kundi la pili ni vitu
usivyoweza kuviathiri, hivi vipo nje ya uwezo wako.
Hivyo unapokutana na chochote na ukajiambia ni kigumu au
kinakushinda, huna haja ya kusumbuka, badala yake jiulize je kipo ndani
ya uwezo wako au nje ya uwezo wako. Kama kipo ndani ya uwezo wako chukua
hatua sahihi, kama kipo nje ya uwezo wako kikubali kama kilivyo au
kipuuze. Hakuna namna bora ya kuendesha maisha yako kama hii, kwa sababu
hakuna chochote kitakachotokea, ambacho kitakuvuruga kabisa.
Ndugu yangu , nikukumbushe tena ya kwamba kama unataka kuitawala dunia,
kuna mtu mmoja unayepaswa kumtawala, na mtu huyo ni wewe mwenyewe.
Hutaweza kujitawala wewe mwenyewe kwa mabavu au nguvu, badala yake
utajitawala kwa kudhibiti mawazo yako na hisia zako.
Moja; penda kile unachofanya, usifanye kwa sababu ya fedha pekee,
fanya kwa sababu unapenda kufanya, fanya kwa sababu unajali, fanya kwa
sababu kuna mchango unaotoa kwa wengine.
Mbili; kuwa mtumiaji wa kwanza wa kile unachouza, hakikisha wewe
mwenyewe unaweza kutumia, au unaweza kumshauri mtu wako wa karibu
kabisa, unayempenda sana atumie. Kwa maneno mengine usiuze kitu ambacho
wewe mwenyewe huwezi kutumia au huwezi kumpa mtu wako wa karibu atumie.
Tatu; toa uhakika wa unachouza na mpe mteja nafasi ya kurudisha iwapo
alichonunua hakitamfaa au hakitafanya kazi kama alivyotegemea. Mfanye
mteja aone hana cha kupoteza anaponunua kwako. Nne; jua tatizo la mteja unalotatua na elezea kile unachouza kwa
namna kinavyotatua tatizo hilo. Usieleze sifa za kitu pekee, bali eleza
namna zinatatua tatizo la mteja wako.
Tano; usiwaseme vibaya washindani wako, usihangaike kuwashinda
wengine, kama unachouza ni kizuri kweli, huna haja ya kuhangaika na
wengine wanauza au kusema nini. Lakini kama huamini kwenye unachouza,
itabidi uanze kuwakosoa na kuwasema vibaya wengine, ili kumfanya mteja
wako aone wewe upo sahihi, lakini hata unapowasema vibaya wengine, mteja
anajua kuna shida kwenye biashara yako.
Kila mmoja anajitahidi kutafuta pesa popote anakojua. Habari njema ni kwamba kila anayetafuta pesa hii ya KULA anapata. Lakini..pamoja
na kuipata, wengi wamekuwa wakilalamika kuwa ni ndogo na kwamba
inatosha kula tu! Wengi wanatamani kupata pesa nyingi zaidi ya hiyo
wanayoipata kwasasa. Kwaujumla, wengi wanashangaa ni kwanini hawapati
pesa ya kutosha kuweza kufanya mambo makubwa zaidi ya KULA na kulipa ADA
za watoto.
Sababu mojawapo ya kushindwa kupata pesa ya kutosha ni malengo mahususi
tunayojiwekea kabla ya kutafuta pesa. Watu wengi wakiamka asubuhi,
malengo yao makubwa kabisa ni kutafuta pesa ya KULA, ADA na kujenga
NYUMBA ya makazi. Wengine akijikakamua kidogo analenga kununua GARI la
kutembelea. Malengo ya watu yanabainishwa kwenye maongezi yao ya
kawaida. Pindi ukiwasikiliza watu, utasikia wakiambizana kuwa “mimi natafuta pesa ya kula basi! Wengine utawasikia wakisema “natafuta pesa kwaajili ya watoto” wengine wamekwenda mbali na kusema kuwa wanatafuta pesa, “ili watoto wao angalau waweze kwenda choo”
Ni wazi kuwa maongezi ya namna hii, yanakupa jibu la moja kwa moja kuwa
watu wengi wana malengo ya kutafuta kiasi kinachotosha KULA, kulipa
KARO na kujenga NYUMBA ya makazi basi! kwamba zaidi ya hapo ni bahati
tu.
Wengi wa wale wanaolalamika kupata pesa kidogo ni wale walioweka malengo
ya kutafuta pesa ya KULA. Ukiweka malengo ya KULA, ujue malengo hayo ni
madogo sana na kwa vyovyote vile yatavutia pesa kidogo sana kwako. Mtu
yeyote mwenye malengo ya kupata pesa ya KULA, hawezi kuweka utajiri kama
kipaumbele chake. Na mwisho wake ujikuta hana ndoto yoyote ya
kutajirika maisha yake yote.
Ukweli ni kwamba, pesa ya KULA siku zote huwa ni ndogo japokuwa
inapatikana kila ikitafutwa. Pamoja na kupatikana kila siku, tatizo lake
ni moja; kwamba, ikishapatikana muhusika anakuwa tayari ana njaa na
hivyo kuitumia mara moja. Ikishaisha muhusika uenda kutafuta tena, na
huo ndio unakuwa mzunguko na mtindo mzima wa maisha ya kila siku.
Kujiwekea malengo ya kutafuta pesa ya KULA na ADA siyo jambo baya! Ubaya
unakuja pale utakapofanya suala la kutafuta pesa ya KULA kama lengo
lako kuu. Mara nyingi watu waliofanikiwa wanatushauri kuyaweka malengo
ya KULA na ADA ndani ya malengo makubwa zaidi (Utajiri). Tunahimizwa
kuachana na utamaduni wa kuweka KULA na ADA kama malengo makuu katika
maisha, kwasababu, kwa kufanya hivyo tutazidi kupoteza muda mwingi na
matokeo yake hututakaa tupate muda wa kufanya mambo makubwa.
Kwa mfano: “Ikiwa wewe unaishi DAR-ES-SALAAM na lengo lako kuu ni
kwenda KARAGWE, maana yake, inabidi ujipange kutafuta jinsi ya kupata
pesa itakayokuwezesha kufika KARAGWE. Pesa ya kufika KARAGWE
ikishapatikana, maana yake ni kwamba sehemu zote za njiani kabla ya
kufika mwisho wa safari yako kwa vyovyote vile, utafika sehemu zote za
njiani japo hilo halikuwa lengo lako kuu. Sehemu za njiani ambazo kwa
vyovyote vile lazima upite ni pamoja na Morogoro, Dodoma, singida,
Tabora, Kahama n.k. Sehemu zote hizi utaweza kufika kwa kutumia nauli
ile ile ya DAR-ES-SALAAM hadi KARAGWE”
Mfano huo hapo juu, unatufundisha kwamba tunahitaji kuweka juhudi na
maarifa yetu kwenye vitu vikubwa kama vile miradi ya maendeleo (majumba ya kupangisha, kilimo biashara, viwanda, biashara kubwa n.k).
Tukiwekeza akiri zetu kwenye mambo kama hayo ni wazi kwamba pesa ya
KULA na ADA za watoto zitapatikana humo humo ndani ya miradi hiyo. Kitu
cha msingi hapa ni kuhakikisha tunajizuia kufanya kazi ya kutafuta pesa
ya KULA na ADA kama malengo yetu makuu. Tusifanye KULA na ADA kuwa
mwisho wa safari yetu BALI suala la pesa ya kula na ADA liwe ni sehemu
za njiani kuelekea Kwenye ndoto kubwa (Utajiri).
Wito wangu kwako msomaji ni wewe kuiambia akili yako na nafsi yako
mwisho wa safari yako, yaani safari ya kuelekea kwenye maisha
unayotamani kuishi. Naamini ukiweza kuiambia ukweli akili na nafsi yako,
basi ujue hapo utakuwa umefikia hatua ya kutafuta pesa nyingi zaidi ya
hiyo ya KULA na kulipa ADA. Ili linawezekana, limewezekana kwangu,
limewezekana kwa wengine na hakuna sababu yoyote ya kutowezekana kwako.
Wapo watu wengi ambao wanakuwa na mipango
mizuri sana kabla hawajawa na fedha, wanajua kabisa wakipata fedha
watafanya nini na nini. Na tena watawashangaa sana wale wanaopata fedha
na kuzitumia vibaya. Lakini subiri watu hao hao wazipate fedha, mipango
yote inayeyuka, fedha zinatumika hovyo na mpaka zinapoisha ndiyo akili
zinawarudia.
Kitu kimoja ambacho nataka kushauri leo kwa wale wote wenye shida ya kukaa na fedha, ni hiki; ACHA KUWA KARANI WA FEDHA ZAKO. Watu wengi linapokuja swala la fedha, hawana tofauti na makarani,
ambao wanapokea fedha na kuzipelekeka zinapopaswa kwenda. Ukienda benki
kuweka fedha na ukamkabidhi karani wa benki fedha zako, utaona kama
anashika fedha nyingi, lakini mwisho wa siku fedha hizo habaki nazo
yeye, bali anakabidhi zinapohusika.
Sasa watu wengi wamekuwa wanayaishi maisha yao kama makarani wa fedha
zao. Kinachotokea ni hiki, mtu anafanya kazi au biashara na analipwa
mshahara au kupata faida kama kipato chake. Anachukua kipato hicho na
kwenda kulipia vitu na kununua vitu mbalimbali. Mwisho anabaki hana
fedha kabisa.
Alichokifanya mtu huyu ni kuchukua fedha kwenye kazi au biashara na
kwenda kuitoa kwa wale wanaomdai au wanaouza vitu mbalimbali. Mwisho wa
siku anabaki hana hata senti moja. Acha mara moja kuwa karani wa fedha zako, kwa kuzihamisha kutoka
unakozipata na kuzipeleka kwenye matumizi na wewe kubaki huna kitu. Na ipo njia moja rahisi kwako kuacha kuwa karani wa fedha zako, njia hiyo ni KUJILIPA WEWE MWENYEWE KWANZA.
Kwa kila kipato unachoingiza kwenye maisha yako, kabla hujapeleka
kwenye matumizi yoyote, toa sehemu ya kipato hicho na iweke pembeni.
Sehemu hiyo ya kipato uliyoitoa ndiyo malipo yako kwako na hupaswi
kuitumia kwa shughuli nyingine yoyote ya matumizi. Hichi ni kipato
ambacho utakiwekeza zaidi ili uweze kufanikiwa zaidi.
Sasa najua ni vigumu kukaa na fedha, kwa sababu kama wanavyosema
watu, fedha huwa hazikosi matumizi. Ukishakua na fedha, dunia
itahakikisha unazitumia kwa namna yoyote ile. Hivyo vitu vitaharibika,
watu wataumwa utashangaa unapokuwa na fedha ndiyo unapokea simu nyingi
zikitaka utoe msaada fulani.
Hivyo kuna njia nyingine bora kabisa ya kuhakikisha kile unachojilipa
hakipati matumizi na ukakipoteza. Njia hiyo ni KUJENGA GEREZA LA AKIBA
YAKO. Kile kiasi ambacho unajilipa wewe mwenyewe, kitengenezee gereza,
ambapo ukishaingiza, huwezi kutoa tena, hata itokee nini. Hata uwe na
dharura kiasi gani, gereza hilo halikuruhusu uondoe fedha ulizoweka.
Gereza la fedha zako ni mfumo wowote unaokuruhusu kuweka fedha lakini
kutoa inakuwa siyo rahisi. Na unaweza kufanya hivyo kwa kuwa na akaunti
maalumu ya benki ambayo inakuruhusu kuweka lakini siyo kutoa. Unaweza
pia kufanya uwekezaji wa moja kwa moja ambao utafanya kupata fedha yako
kuchukue muda. Lakini pia unaweza kuweka mpango na mtu au watu wengine,
na mkawa mnaweka fedha lakini hamtoi. Angalia njia inayokufaa wewe, ambapo ukiweka fedha, inakuwa vigumu
sana kwako kuitoa, na hilo litakusaidia kujiwekea fedha zako kulingana
na mipango uliyonayo.
Hivyo nimalize kwa kukumbusha mambo muhimu sana tuliyojadili hapa; ACHA KUWA KARANI WA FEDHA ZAKO. JILIPE WEWE MWENYEWE KWANZA. TENGENEZA GEREZA LA FEDHA ZAKO. Fanya hayo matatu na fedha yako itaweza kutulia, na utaweza kufanya
makubwa. Ukishaweza kuituliza fedha yako, utaweza kuiwekeza na kupitia
uwekezaji ndiyo utaweza kufikia utajiri na uhuru wa kifedha.
Moja ya changamoto kubwa zinazowapelekea wengi kushindwa kwenye
maisha ni kuendeshwa na hisia badala ya wao kuendesha hisia zao. Wote
tunajua kwamba pale tunaporuhusu hisia zitutawale, tunakuwa tumeondoa
kabisa uwezo wetu wa kufikiri. Kwa sababu hisia kali na fikra haviwezi
kukaa pamoja.
Kupitia falsafa ya ustoa, tunajifunza kwamba hisia ni kitu ambacho
tunakitengeneza sisi wenyewe na hakuna anayetupa, hivyo tunaweza
kuchagua kutoruhusu hisia zitawale maamuzi yetu. Epictetus ana maneno mazuri ya kutuambia kuhusu hisia; It isn’t the things themselves that disturb people, but the
judgements that they form about them. Death, for instance, is nothing
terrible, or else it would have seemed so to Socrates too; no, it is in
the judgement that death is terrible that the terror lies. Accordingly,
whenever we are impeded, disturbed or distressed, we should never blame
anyone else but only ourselves, that is, our judgements. It is an act of
a poorly educated person to blame others when things are going badly
for him; one who has taken the first step towards being properly
educated blames himself, while one who is fully educated blames neither
anyone else nor himself. – Epictetus, Handbook, 5 Kinachotusumbua siyo kile kinachotokea, bali tafsiri yetu kwa kile
kinachotokea. Kwa mfano kifo, siyo kitu cha kutisha, kama ingekuwa hivyo
wanafalsafa kama Socrates wangekiogopa. Ni tafsiri yetu kwamba kifo ni
kitu kibaya ndiyo inatusumbua. Hivyo hivyo, tunapokuwa tumekwazika,
tumesumbuka au kupata msongo, hatupaswi kumlaumu mtu yeyote bali sisi
wenyewe, kwa sababu hivyo vinatokana na tafsiri zetu wenyewe. Kwa
asiyekuwa na elimu, huwalaumu wengine pale mambo mabaya yanapomtokea,
anayeanza kujifunza hujilaumu mwenyewe wakati yule aliyeelimika hamlaumu
yeyote wala hajilaumu yeye mwenyewe.
Maisha siyo rahisi, hakuna chochote kwenye maisha yako kitaenda kama
ulivyopanga. Utakutana na magumu na changamoto ambazo zitakuangusha na
kujaribu kukukatisha tamaa. Ili uweze kufanikiwa, ili uweze kupata
chochote unachotaka, unapaswa kuwa mstahimilivu, unapaswa kuwa mgumu,
unapaswa kuwa kinga’ang’anizi na unapaswa kutokujua kabisa msamiati
unaoitwa kushindwa au kukata tamaa. Falsafa ya ustoa inatujenga tuwe wastahimilivu kwa kutuandaa kukutana na magumu na hata kuweza kuyavuka bila ya kukata tamaa.
Ili kuzuia mabaya yanayotokea yasituvuruge, tunapaswa kuwa na maandalizi ya mabaya na magumu yanayoweza kutokea.
Kama wastoa tunaweza kujiandaa na magumu kwa njia mbili. Njia ya
kwanza ni kuishi magumu yenyewe, kujiweka katika nyakati ngumu hata kama
hujafikia ugumu huo. Kufanya kama vile huna kitu fulani, hata kama
tayari unacho. Kwa njia hii, hutashtushwa pale kile ulichokuwa
unategemea kitakapokuwa hakipatikani. Njia ya pili ni kujijengea taswira ya magumu kabla hayajatokea.
Unapopanga chochote, usiangalie tu yale mazuri unayotegemea yatokee,
bali pia jenga taswira ya mabaya yanayoweza kutokea. Jiulize kipi kibaya
kabisa kinachoweza kutokea, kisha pata picha kwamba kitu hicho
kimetokea na ona utawezaje kukabiliana nacho. Zoezi hili la kujijengea
taswira ya mabaya linakufanya usipatwe na mshangao pale unapokutana na
magumu, kwa sababu ulishapata picha ya magumu hayo. Pia kwa sababu
hutapata magumu makubwa kabisa, utajiambia ulishaona magumu zaidi ya
uliyokutana nayo, hivyo hayakusumbui. Marcus anatuambia; Be like the headland, on which the waves break constantly, which
still stands firm, while the foaming waters are put to rest around it.
‘It is my bad luck that this has happened to me.’ On the contrary, say,
‘It is my good luck that, although this has happened to me, I can bear
it without getting upset, neither crushed by the present nor afraid of
the future.’ This kind of event could have happened to anyone, but not
everyone would have borne it without getting upset. – Marcus Aurelius, Meditations, 4.49 Kuwa kama ukingo wa mto au bahari ambao unapigwa na mawimbi ya maji
kila mara lakini unaendelea kusimama imara na kuyatuliza mawimbi ya
maji. Chochote kibaya kinapotokea, usijiambie nina bahati mbaya hiki
kimetokea kwangu, badala yake jiambie nina bahati nzuri hiki kimetokea
kwangu kwa sababu nitaweza kukikabili bila ya kukasirika au kuumizwa
nacho kwa sasa au wakati ujao. Kitu kama hicho kingeweza kutokea kwa
yeyote, lakini siyo kila mtu anaweza kukipokea kwa utulivu.
Pia Seneca anatukumbusha kuishi kila siku yetu kama ndiyo siku ya mwisho kwenye maisha yetu; Glad and cheerful, let us say, as we go to our rest: ‘I have finished
living; I have run the course that fortune set for me’. If God gives us
another day, let us receive it with joy. The happiest person, who owns
himself more fully, is the one who waits for the next day without
anxiety. Anyone who can say, ‘I have had my life’ rises with a bonus,
receiving one more day. – Seneca, Letters, 12.9.
Kila unapoimaliza siku yako jiambie kwa furaha na uchangamfu
nimemaliza kuishi, nimemaliza mwendo ambao asili imenitengenezea. Kama
Mungu atanipa tena siku nyingine, nitaipokea kwa furaha. mtu mwenye
furaha anajimiliki yeye kwa ujumla, anaisubiri siku nyingine bila ya
wasiwasi. Yeyote anayejiambia nimeyamaliza maisha yangu, anapata zawadi
ya siku nyingine tena ya kuishi.
Moja ya kisingizio cha watu wengi kwenye kushindwa kufanya yale
wanayotaka kufanya kimekua ni muda. Muda unaonekana kuwa mfupi sana na
mambo ya kufanya yakiwa mengi. Hivyo tumekuwa tunatamani kama masaa ya
siku yangeongezwa ili tuweze kufanya zaidi. Lakini ukweli ni kwamba, masaa ya siku hayataongezeka, ni yale yale
24. Na wale wanaofanikiwa sawa sawa na wanaoshindwa, wana masaa hayo
hayo kwa siku. Sasa kwa nini wachache wafanikiwe kwenye muda huo, wakati
wengi wanashindwa na kuona hawana muda? Seneca analo jibu zuri sana kwetu kuhusu muda; Life is long enough, and a sufficiently generous amount has been
given to us for the highest achievements if it were all well invested.
But when it is wasted in heedless luxury and spent on no good activity,
we are forced at last by death’s final constraint to realize that it has
passed away before we knew it was passing. So it is: we are not given a
short life but we make it short, and we are not ill-supplied but
wasteful of it. Just as when ample and princely wealth falls to a bad
owner it is squandered in a moment, but wealth however modest, if
entrusted to a good custodian, increases with use, so our lifetime
extends amply if you manage it properly. – Seneca, On The Shortness Of
Life. Maisha ni marefu vya kutosha na muda wa kutosha tumepewa kwa kufikia
yale makubwa kama tutauwekeza muda huo vizuri. Lakini tunapopoteza muda
huo kwa anasa zisizo na maana na kushindwa kufanya yale mazuri, tunakuja
kustuka tumepoteza muda na maisha yetu pale tunapofikia kifo. Hivyo
basi, siyo kwamba tuna maisha mafupi, bali tunayafanya kuwa mafupi, siyo
kwamba muda ni mdogo, bali tunao mwingi mpaka tunaupoteza. Kama ambavyo
utajiri ukiwa kwenye mikono ya mtu asiye makini unapotea na ukiwa
kwenye mikono ya mtu makini unakua, ndivyo maisha yetu yalivyo, yanakua
kama yataendeshwa vizuri.
”Do not go where the path may lead, go instead where there is no path and leave a trail.” – Ralph Waldo Emerson
Watu wengi wamekuwa wanashindwa kwenye maisha kwa sababu hawathubutu
kufanya vitu vipya, badala yake wanaangalia kile ambacho tayari
kimeshafanya na wao wanafanya. Hii ni kufuata njia, sasa unapochagua
kufuata njia fulani, jua utafika kule ambapo njia hiyo imeelekea. Kama
utafanya kile ambacho wengine wanafanya, utapata matokeo ambayo
wanayapata.
Njia pekee ya kufanikiwa zaidi, ni kufanya mambo mapya, kufanya yale
ambayo hakuna mwingine anayefanya, kutengeneza njia mpya, pale ambapo
hakuna njia. Hili linatisha, kwa sababu unakuwa huna uhakika, nafasi ya
kushindwa ni kubwa, lakini pia nafasi ya kufanikiwa ni kubwa zaidi. Kwenye chochote unachochagua kufanya, acha kuangalia wengine
wanafanya nini ili uige, badala yake angalia kipi muhimu kinachopaswa
kufanya kisha kifanye kwa njia ambayo ni sahihi kwako kufanya na kwa
wale unaowahudumia. Kwa namna hii utatengeneza njia mpya na wewe kama
kiongozi wa njia hiyo utanufaika zaidi. Rafiki, sindano za leo zimekuwa ndefu na kali, lakini kama
utazifanyia kazi, hutabaki hapo ulipo. Sina kingine cha kuongeza zaidi
ya kukukumbusha kanuni yetu muhimu ambayo ni MAARIFA SAHIHI + KUCHUKUA
HATUA KUBWA = MAFANIKIO MAKUBWA. Maarifa ni hayo, kazi kwako kuchukua
hatua ili ufanikiwe.
Sisi binadamu huwa tunasumbuka na mambo mengi sana, lakini tukianza
kuyaangalia mambo hayo, mengi tunajisumbua nayo bure, kwa sababu yapo
nje ya uwezo wetu, hakuna chochote tunachoweza kufanya tukayabadili au
kuyaathiri. Mambo yote yanayotokea kwenye maisha yetu tunaweza kuyagawa kwenye
makundi mawili, yaliyo ndani ya uwezo wetu, haya ni yale ambayo tunaweza
kuyaathiri, tunaweza kuyafanya kuwa bora zaidi. Na kuna yale ambayo
yapo nje ya uwezo wetu, ambapo hatuna cha kufanya.
Baadhi ya vitu vipo ndani ya uwezo wetu na vingine vipo nje ya uwezo
wetu. Vilivyo ndani ya uwezo wetu ni maoni yetu, fikra zetu, maamuzi
yetu na matendo yetu, kwa kifupi yale yote ambayo sisi tunayafanya. Vitu
vilivyo nje ya uwezo wetu ni miili yetu, mali zetu, sifa zetu na nafasi
nyingine tunazopewa, kwa kifupi chochote ambacho hatufanyi sisi moja
kwa moja, kipo nje ya uwezo wetu. Vitu vilivyo ndani ya uwezo wetu ni
bure, huru na visivyo na ukomo, vilivyo nje ya uwezo wetu ni dhaifu,
visivyo huru, vyenye ukomo na visivyo vyetu.
Kwa vyovyote vile, hupaswi kusumbuliwa na chochote, kwa sababu kama
kitu kipo ndani ya uwezo wako basi unahitaji kuchukua hatua, na kama
kipo ndani ya uwezo wako huna hatua ya kuchukua hivyo kubaliana nacho
kama kilivyo au kipuuze.
Huwa tunayaona maisha yetu ni magumu na tuna mengi ya kukabiliana
nayo, lakini hebu fikiria jinsi ulimwengu unavyojiendesha. Fikiria jinsi
ambavyo sayari yetu ya dunia inalizunguka jua mwaka mzima, na kutupatia
majira ya mwaka. Fikiria jinsi sayari hii inajizungusha kwenye mhimili
wake kila siku na kutupatia usiku na mchana. Asili imeyapangilia mambo
yake ambayo yanajiendesha vizuri.
Sisi pia tunapaswa kuishi kwa msingi wa asili, kujua kile ambacho
tunapaswa kufanya, kujipanga kukifanya na kukifanya kwa ubora na msimamo
kama ambavyo asili inafanya mambo yake. Kwa kuishi kulingana na asili,
hata matatizo yetu yanayotusumbua yanaonekana ni madogo sana
ukilinganisha na jinsi ulimwengu mzima unavyojiendesha.
Kazi za Mungu ndiyo zinatupa sisi riziki, na kazi za asili
hazitofautiani na asili yenyewe. Kila kitu kinatokana na asili. Kila
kitu ambacho ni muhimu na kinachohitajika na ulimwengu mzima kinatokana
na asili. Kila kinachotokana na asili na kila kinachoitunza asili ni
kizuri kwa kila sehemu ya asili. Mabadiliko ya kipengele chochote kwenye
asili, ndiyo yanaufanya ulimwengu kuwa kama ulivyo.
Sisi binadamu ni viumbe wa kijamii, hatuwezi kuishi kwa kujitegemea
wenyewe kwa kila kitu. Hivyo mahusiano yetu na wengine ni moja ya vitu
muhimu sana kwetu ili kuweza kuwa na maisha bora. Falsafa ya ustoa inatufundisha jinsi ya kutengeneza mahusiano bora na
wale wanaotuzunguka kwa kuimarisha mahusiano yetu na ushirikiano kwenye
mambo mbalimbali. Njia bora ya kuimarisha mahusiano na ushirikiano ni kuangalia tabia
nzuri zilizopo ndani ya wengine badala ya kuangalia mabaya pekee. Pia
kuangalia namna ya kushirikiana na siyo kupingana. Marcus ana maneno mazuri ya kutuambia kuhusu mahusiano; Say to yourself first thing in the morning: I shall meet with people
who are meddling, ungrateful, violent, treacherous, envious, and
unsociable. They are subject to these faults because of their ignorance
of what is good and bad. But I have recognised the nature of the good
and seen that it is the right, and the nature of the bad and seen that
it is the wrong, and the nature of the wrongdoer himself, and seen that
he is related to me, not because he has the same blood or seed, but
because he shares in the same mind and portion of divinity. So I cannot
be harmed by any of them, as no one will involve me in what is wrong.
Nor can I be angry with my relative or hate him. We were born for
cooperation, like feet, like hands, like eyelids, like the rows of upper
and lower teeth. So to work against each other is contrary to nature;
and resentment and rejection count as working against someone. – Marcus
Aurelius, Meditations, 2.1 Jiambie hili kitu cha kwanza asubuhi: Leo nakwenda kukutana na watu
ambao ni waovu, wasio na shukrani, wenye fujo, wasaliti, wenye wivu na
wasiojali. Watu hao wako hivyo kwa sababu hawajui kipi kizuri na kipi
kibaya. Lakini mimi natambua asili ya uzuri na nimeona kipi sahihi na
asili ya ubaya na kuona kipi kisicho sahihi na asili ya wanaofanya ubaya
na kuona wana uhusiano na mimi, kwa sababu wana damu sawa na yangu na
tunashirikiana mawazo yetu. Siwezi kuumizwa na yeyote kwa sababu hakuna
anayeweza kunihusisha kwenye ubaya wake. Pia siwezi kuwa na hasira au
kumchukia ndugu yangu. Sote tumezaliwa kwa ushirikiano, kama miguu,
mikono, kope za macho, meno ya juu na ya chini. Hivyo kufanya kazi kwa
kupingana ni kinyume na asili na chuki na kukataana ni kufanya kazi
kinyume na wengine.
Tabia njema ni moja ya misingi muhimu sana kwenye falsafa ya ustoa.
Kadiri unavyojijengea na kuishi kwa tabia njema, ndivyo
unavyojitengenezea maisha bora na yenye furaha wakati wote. Tabia njema
ndiyo zao la furaha. Kwenye ustoa, tabia njema ni pale unapoishi na
kusimamia yale yenye maana kwako na kwa wengine, na kuachana na yale
yasiyo na maana. Kwenye ustoa kuna tabia njema kuu nne; HEKIMA; Ubora katika kufikiri na kufanya maamuzi. UJASIRI; Uwezo wa kukabiliana na hatari kwa usahihi. HAKI; Ubora katika mahusiano yetu na wengine. KIASI; Uwezo wa kudhibiti hisia na tamaa. Marcus ana haya ya kutuambia kuhusu tabia njema;
If you can find anything in human life better than justice,
truthfulness, selfcontrol, courage […] turn to it with all your heart
and enjoy the supreme good that you have found […] but if you find all
other things to be trivial and valueless in comparison with virtue, give
no room to anything else, since, once you turn towards that and divert
from your proper path, you will no longer be able without inner conflict
to give the highest honour to what is properly good. It is not right to
set up as a rival to the rational and social good anything alien to its
nature, such as the praise of the many, or positions of power, wealth,
or enjoyment of pleasures. – Marcus Aurelius, Meditations, 3.6 Kama unaweza kupata kitu bora kwenye maisha ya mtu zaidi ya haki,
ukweli, kujidhibiti na ujasiri, kishikilie sana kitu hicho. Lakini kama
utakuta vitu vingine ni visivyo na maana ukilinganisha na tabia njema,
usitoe nafasi kwa kitu kingine bali tabia hizo njema. Kwa sababu
utakapoacha njia yako sahihi hutaweza tena kuzingatia yale ambayo ni
mazuri kwako. Siyo sahihi kuleta upinzani kati ya fikra sahihi na vitu
vya nje kama sifa kutoka kwa wengine, nafasi za madaraka, utajiri na
kufurahia raha.
Moja ya sababu zinazopelekea wengi kukosa furaha ni kufanya vitu
ambavyo wanajua siyo sahihi, lakini kwa sababu wengine wanafanya au
wanawategemea wafanye, basi wanafanya ili kuwaridhisha wengine. Hatari
nyingine kubwa ni watu kufanya kitu wakitegemea matokeo fulani yatokee.
Yaani unachukua hatua, ukitegemea matokeo fulani ili uwe na furaha. Hii
ni njia ya kujitengenezea kushindwa na kujinyima furaha. Cicero ana haya ya kutuambia kuhusu kufanya na kutegemea; The wise person does nothing that he could regret, nothing against
his will, but does everything honourably, consistently, seriously, and
rightly; he anticipates nothing as if it is bound to happen, but is
shocked by nothing when it does happen …. and refers everything to his
own judgement, and stands by his own decisions. I can conceive of
nothing which is happier that this. – Cicero, Tusculan Disputations 5.81 Mtu mwenye hekima hafanyi chochote atakachoweza kujutia, hafanyi
chochote kinyume na matakwa yake bali anafanya kila kitu kwa heshima,
msimamo, umakini na usahihi; hategemei chochote kitatokea kwa yeye
kufanya, lakini pia hashangazwi na chochote kinachotokea, na anarejea
kila kitu kwa maamuzi yake mwenyewe na kusimamia maamuzi hayo. Hakuna
kitu chenye furaha kama kuishi kwa namna hii. Kama ambavyo Cicero anatuambia, furaha siyo kitu unachokipata
kutokana na kupata vitu fulani au kuwa kwenye hali fulani kama wengi
wanavyofikiri. Bali furaha ni matokeo ya maisha unayoishi na namna unavyofanya mambo
yako. Kama unafanya kile kilicho sahihi mara zote, ukawa na msimamo na
kufanya kwa umakini na usahihi, utapata matokeo mazuri. Na kama hufanyi
ukitegemea matokeo mazuri, matokeo yoyote yatakayotokea hayatabadili
chochote kwenye furaha yako, kusudi lako wewe ni kufanya kwa usahihi na
siyo kulazimisha matokeo unayotaka wewe. Fanya maamuzi yako na yasimamie
kwenye maisha yako, hili litakupa furaha kuliko kuhangaika na kukosa
msimamo.
Kila siku tunayoishi ni nafasi nzuri kwetu kuwa bora zaidi, kwa
sababu kuna mengi tunakutana nayo ya kujifunza, kuna makosa
tunayoyafanya na yapo mazuri tunayafanya pia. Wengi wamekuwa wanakosa
nafasi ya kuzitumia siku zao kuwa bora zaidi kwa sababu hawapati muda wa
kutafakari kila siku yao. Kupitia Ustoa, tunashauriwa kuipima na kutafakari kila siku yetu
kabla ya kulala. Na hapa ndipo tunapata nafasi ya kujifunza na kujiandaa
kuwa bora zaidi kwenye siku inayofuata. Jioni unapoimaliza siku yako, usikimbilie tu kulala na kuona siku
imeisha, badala yake unahitaji kuwa na tahajudi ambayo utaipitia siku
yako yote. Kwenye tahajudi hii, pitia siku yako nzima, kwa kufikiria kila
ulichofanya kwenye siku yako, kila uliyekutana naye na mawazo na hisia
ulizokuwa nazo siku nzima. Kisha jiulize na kujijibu maswali haya matatu; Moja; vitu gani umefanya vibaya? Katika yale uliyofanya kwa siku
nzima, je vitu gani umefanya kwa ubaya au kwa njia ambazo siyo sahihi? Mbili; vitu gani umefanya vizuri? Katika vitu vyote ulivyofanya kwa
siku nzima, vipi ambavyo umevifanya kwa uzuri, ni kwa namna gani umeishi
misingi na tabia za ustoa? Tatu; Vitu gani utakwenda kufanya tofauti? Ni vitu gani unahitaji
kuvifanya kwa utofauti ili kuweza kuishi kulingana na msingi na tabia za
ustoa? Kwa kujiuliza na kujipa majibu ya maswali hayo matatu, utaweza
kujipima kwa kila siku yako, na pia kujiandaa vyema kwa siku inayofuata.
Pia utaepuka kurudia makosa uliyofanya kwa siku husika. Kauli ya Epictetus kwenye tahajudi ya jioni; “Allow not sleep to close your wearied eyes, Until you have reckoned
up each daytime deed: “Where did I go wrong? What did I do? And what
duty’s left undone?” From first to last review your acts and then
Reprove yourself for wretched [or cowardly] acts, but rejoice in those
done well.” (Discourses, 3.10.2–3) Anasema usikubali usingizi ufumbe macho yako kabla hujahesabu kila
tendo ulilofanya kwenye siku yako. kipi umekosea, kipi umefanya vizuri
na kipi ambacho hujakamilisha. Kuanzia tendo la kwanza mpaka la mwisho,
jikaripie kwa yale uliyofanya vibaya na jisifie kwa yale uliyofanya
vizuri.
Huwa tunazianza siku zetu tukitegemea kutekeleza yale tuliyopanga na
kufanya mambo makubwa sana. Lakini siku zetu zimekuwa haziendi kama
ambayo tumepanga, yamekuwa yanatokea mambo ambayo hatukutegemea yatokee,
hasa kwa wale ambao tulitegemea wafanye vitu fulani na wasifanye.
Hili limekuwa linawanyima wengi furaha, lakini kwa falsafa ya ustoa,
hupaswi kukosa furaha kwa mambo kama hayo, kwa sababu unapaswa
kuyategemea yakitokea kabla hata hayajatokea. Mstoa Marcus Aurelius ana hili la kutuambia pale tunapoianza siku yetu; “Say to yourself first thing in the morning: I shall meet with people
who are meddling, ungrateful, violent, treacherous, envious, and
unsociable. They are subject to these faults because of their ignorance
of what is good and bad.” (Meditations, 2.1) Jiambie unakwenda kuianza siku ambayo utakutana na watu wachafu,
wasio na shukrani, wenye fujo, wasaliti, wenye wivu na wasiojali mambo
ya wengine. Na wanafanya mambo hayo kwa sababu hawajui mazuri na mabaya. Kwa kuianza asubuhi yako kwa tafakari yenye nguvu namna hii, hakuna
chochote kitakachokutokea ambacho kitakushangaza, maana ulishakitegemea.
“What is a happy life? It is peacefulness and lasting tranquillity,
the sources of which are a great spirit and a steady determination to
hold fast to good decisions. How does one arrive at these things? By
recognizing the truth in all its completeness, by maintaining order,
moderation and appropriateness in one’s actions, by having a will which
is always well-intentioned and generous, focused on reason and never
deviating from it, as lovable as it is admirable.” – Seneca, Letters, 92.3
Seneca anauliza maisha ya furaha maana yake nini? Ni maisha ambayo
yana amani na utulivu, ambayo chanzo chake ni imani kuu na maamuzi ya
kushikilia maamuzi sahihi. Na je mtu anawezaje kufikia hili? Ni kwa
kugundua ukweli kamili, kwa kuenda kulingana na mipango, kuwa na kiasi
katika matendo na kuwa na nia njema na ukarimu, kuongozwa na fikra
sahihi na kutokupotoka.
USTOA ni falsafa ya matendo, ni falsafa ambayo imelenga kumwezesha
mtu kuwa na maisha bora, kwa kufikiri sahihi na kuchukua hatua sahihi
kwenye maisha yake. Falsafa ya ustoa siyo kama falsafa nyingine za
kubishana na kutaka kuonekana unajua zaidi, badala yake ni falsafa ya
kufikiri sahihi na kuchukua hatua sahihi. Falsafa ya ustoa inalenga
kudhibiti hisia zetu na kuishi kulingana na asili. Kwa njia hiyo,
tunakuwa na maisha bora wakati wote.
Falsafa ya ustoa ilianzishwa na Zeno wa Citium miaka ya 301 K.K na
baadaye kupokelewa na kukuzwa na wanafalsafa Cato, Seneca, Epictetus na
Marcus Aurelius. Hawa wote ni wanafalsafa walioishi zaidi ya miaka 2000
iliyopita, wakati wa utawala wa Roma.