Rafiki Yangu Mpendwa,
Watu wengi wanamka kila siku…
Wanaoga, wanavaa, wanatoka.
Lakini hawajui kwa nini wanaishi.
Wanapambana… lakini hawajui wanapambana kwa lipi.
Wanaume wanahangaika na mihangaiko,
Wanawake wanahangaika na wanaume.
Kila mtu anakimbia, lakini hakuna anayeuliza:
"Tunakoenda ni wapi?"
Ishu Hii Ndio Inasababisha Maisha Ya Watu Yatupwe Kama Karatasi Iliyotumika.
Unajikuta una miaka 30... lakini unahisi hujaanza kuishi.
Unajiona hufai.
Unachoka bila kazi.
Una usingizi wa saa 10 lakini bado umechoka.
Unapoteza nguvu kwenye mambo yasiyojenga.
Unapata hela unazimaliza bila hata kumbukumbu.
Unapenda unakataliwa.
Unajifunza lakini bado maisha yako yapo vile vile.
Unapambana, lakini unapambana gizani.
Umefungwa kwa minyororo usiyoiona…
Na minyororo hiyo inaitwa: "Kutokujua KUSUDI la maisha yako."
Kujua Kisudi Ni Siri Ya Waliotoka Chini Wakafika Juu.
Wewe si maskini umepoteza mwelekeo tu.
Wewe si mvivu hujagundua unachopaswa kufanya.
Wewe si mshindwa hujajua sababu ya wewe kuwa hai.
Watu wakishajua walichozaliwa kufanya,
wanabadilika kama mwewe aliyefunguliwa.
Wanapaa.
Wanang’ara.
Wanatesa!
Ukweli Ni Huu: Maisha Hayaanzi Kwa Kupata Pesa Yanaanza Kwa Kujielewa.
Na huwezi kujielewa bila MWONGOZO.
Huwezi kufika bila RAMANI.
Huwezi kushinda bila KUJUA UNAPIGANIA NINI.
Ukweli mwingine ni huu:
Watu wengi wameishia kuishi maisha ya kuigiza.
Maisha ya watu wengine.
Wanavaa kama wengine.
Wanakimbia mafanikio ya wengine.
Wanajilinganisha.
Wanashindana.
Lakini ndani yao kuna MOTO UMEFICHWA.
Moto wa ndoto zao.
Moto wa kusudi lao.
Moto wa ukubwa wao halisi.
SULUHISHO?
Chukua MWONGOZO huu: “MWONGOZO WA MAISHA YA MAFANIKIO.”
KWA KUEDELEA KUSOMA VITABU Ndani yake utajifunza:
Jinsi ya kugundua kusudi lako.
Sheria 100 za maisha ya mafanikio.
Jinsi ya kuamka kila asubuhi ukiwa na maana
Jinsi ya kuishi maisha ya tofauti
Jinsi ya kuacha kuigiza na kuanza kuishi maisha yako halisi
Bado namkumbuka Huyu Kijana.
Kuna kijana mmoja alinitafuta.
Alichoka kuishi maisha ya ‘kawaida.’
Alikuwa na degree.
Alikuwa na kazi.
Lakini kila kitu kilionekana kimekosa ladha.
Akaanza kunywa.
Akaanza kuchelewa kazini.
Akaanza kujichukia.
Siku moja akaniambia:
“Bro, naishi kama si mimi.”
Nikampa mwongozo huu.
Akarudi baada ya wiki tatu na macho yenye mwanga.
Sasa ameanzisha kitu chake.
Anaamka kabla ya saa kumi.
Anapata pesa.
Anapendwa.
Anajipenda.
Maana sasa anajua KUSUDI lake.
Uko Tayari Kuamka?
Ama utaendelea kuishi kama ndoto ya mtu mwingine?
Usiishi kama kivuli jifunze kuangaza.
ENDELEA KUSOMA VITABU KILA SIKU ILI UENDELEE KUANGAZA NA KUISHI KUSUDI LAKO