Saturday, May 31, 2025

MAKALA : JE, WAJUA KUSUDI LAKO KUWAKO HAPA DUNIANI ?? NDANI YAKO KUNA MOTO WA NDOTO ZAKO UMEFICHWA------NA MWL JAPHET MASATU ------CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136

 Rafiki Yangu Mpendwa,

‎Watu wengi wanamka kila siku…

‎Wanaoga, wanavaa, wanatoka.

‎Lakini hawajui kwa nini wanaishi.

‎Wanapambana… lakini hawajui wanapambana kwa lipi.

‎Wanaume wanahangaika na mihangaiko,

‎Wanawake wanahangaika na wanaume.

‎Kila mtu anakimbia, lakini hakuna anayeuliza:

‎"Tunakoenda ni wapi?"

‎Ishu Hii Ndio Inasababisha Maisha Ya Watu Yatupwe Kama Karatasi Iliyotumika.

‎Unajikuta una miaka 30... lakini unahisi hujaanza kuishi.

‎Unajiona hufai.

‎Unachoka bila kazi.

‎Una usingizi wa saa 10 lakini bado umechoka.

‎Unapoteza nguvu kwenye mambo yasiyojenga.

‎Unapata hela unazimaliza bila hata kumbukumbu.

‎Unapenda unakataliwa.

‎Unajifunza lakini bado maisha yako yapo vile vile.

‎Unapambana, lakini unapambana gizani.

‎Umefungwa kwa minyororo usiyoiona…

‎Na minyororo hiyo inaitwa: "Kutokujua KUSUDI la maisha yako."

‎Kujua Kisudi Ni Siri Ya Waliotoka Chini Wakafika Juu.

‎Wewe si maskini umepoteza mwelekeo tu.

‎Wewe si mvivu hujagundua unachopaswa kufanya.

‎Wewe si mshindwa hujajua sababu ya wewe kuwa hai.

‎Watu wakishajua walichozaliwa kufanya,

‎wanabadilika kama mwewe aliyefunguliwa.

‎Wanapaa.

‎Wanang’ara.

‎Wanatesa!

‎Ukweli Ni Huu: Maisha Hayaanzi Kwa Kupata Pesa Yanaanza Kwa Kujielewa.

‎Na huwezi kujielewa bila MWONGOZO.

‎Huwezi kufika bila RAMANI.

‎Huwezi kushinda bila KUJUA UNAPIGANIA NINI.

‎Ukweli mwingine ni huu:

‎Watu wengi wameishia kuishi maisha ya kuigiza.

‎Maisha ya watu wengine.

‎Wanavaa kama wengine.

‎Wanakimbia mafanikio ya wengine.

‎Wanajilinganisha.

‎Wanashindana.

‎Lakini ndani yao kuna MOTO UMEFICHWA.

‎Moto wa ndoto zao.

‎Moto wa kusudi lao.

‎Moto wa ukubwa wao halisi.

‎SULUHISHO?

‎Chukua MWONGOZO huu: “MWONGOZO WA MAISHA YA MAFANIKIO.”

‎KWA   KUEDELEA    KUSOMA    VITABU  Ndani yake utajifunza:

✅ Jinsi ya kugundua kusudi lako.

‎Sheria 100 za maisha ya mafanikio.

✅ Jinsi ya kuamka kila asubuhi ukiwa na maana

✅ Jinsi ya kuishi maisha ya tofauti

✅ Jinsi ya kuacha kuigiza na kuanza kuishi maisha yako halisi

‎Bado namkumbuka Huyu Kijana.

‎Kuna kijana mmoja alinitafuta.

‎Alichoka kuishi maisha ya ‘kawaida.’

‎Alikuwa na degree.

‎Alikuwa na kazi.

‎Lakini kila kitu kilionekana kimekosa ladha.

‎Akaanza kunywa.

‎Akaanza kuchelewa kazini.

‎Akaanza kujichukia.

‎Siku moja akaniambia:

‎“Bro, naishi kama si mimi.”

‎Nikampa mwongozo huu.

‎Akarudi baada ya wiki tatu na macho yenye mwanga.

‎Sasa ameanzisha kitu chake.

‎Anaamka kabla ya saa kumi.

‎Anapata pesa.

‎Anapendwa.

‎Anajipenda.

‎Maana sasa anajua KUSUDI lake.

‎Uko Tayari Kuamka?

‎Ama utaendelea kuishi kama ndoto ya mtu mwingine?

👉 Usiishi kama kivuli jifunze kuangaza.

ENDELEA   KUSOMA   VITABU    KILA  SIKU  ILI  UENDELEE  KUANGAZA  NA    KUISHI  KUSUDI  LAKO

No comments:

Post a Comment