Kakaa/Dadaa Yangu...
Umesahau wewe ni nani.
Umesahau kuwa ndani yako kuna nguvu ya kutikisa dunia.
Umejikatia tamaa kimya kimya.
Kila siku unasema *labda mimi sina bahati.*
Umeanza kuamini maisha ni magumu na huwezi kubadilisha chochote.
Lakini ukweli ni huu: UNA NGUVU YA MIUJIZA NDANI YAKO ,
Unaitumia vibaya.
Au hujui hata ipo.
Ulishawahi kumuona mtu aliyeanzisha biashara kwa buku 5 akafika juu?
Ulishawahi kumuona mtu aliyefeli shule lakini leo anaajiri waliopata division one?
Ulishawahi kumuona mtu aliyetelekezwa, akasota, lakini leo anajenga nyumba yake?
Wote hawa hawakuwa na miujiza ya mbinguni.
Walitumia nguvu ya ndani waliyoamka nayo kila siku.
Na hiyo nguvu wewe pia unayo.
Lakini... unaitumia kuskroll TikTok.
Unaitumia kulalamika.
Unaitumia kutafuta huruma badala ya suluhisho.
Una nguvu lakini hauna mwelekeo.
Miujiza sio kupasuliwa mbingu.
Sio malaika kushuka.
Miujiza ni pale mtu wa kawaida anapoamua kuamka na kuchukua hatua isiyo ya kawaida.
Ni pale mtu anapoamua kuamka kabla ya wengine.
Kuanza kuandika ndoto zake.
Kuanza kusoma vitabu badala ya magazeti ya udaku.
Kuanza kuomba kazi kwa bidii badala ya kuomba msaada.
Miujiza ni matokeo ya msimamo.
Suluhisho Lipo. Na Lipo Ndani Yako.
Badilisha namna unavyofikiri.
Acha kusema “sina mtaji” sema “naanza na hiki kidogo.”
Acha kusema “nimechelewa” sema “leo ndiyo siku yangu ya kwanza.”
Acha kujificha nyuma ya visingizio.
Toka uvunguni.
Toka kwenye comfort zone ya umaskini wa mawazo.
Chukua hatua.
Anza leo.
Fanya kitu.
Kwa sababu NGUVU YA MIUJIZA UMEIBEBEA WEWE MWENYEWE.
Bado namkumbuka....
Kuna bro mmoja alichoka na maisha.
Alikuwa hana kazi. Hana mtaji. Hana cheti.
Alikaa chini akaandika: “Mwaka huu lazima niwe mtu mwingine.”
Akaanza kuuza karanga mtaani.
Akaweka akiba ya mia mia.
Alikuwa anasoma vitabu alivyokopeshwa.
Alifungua YouTube kujifunza marketing.
Miaka mitatu baadaye...
Ana biashara ya kuuza nafaka.
Ana familia.
Ana ndoto mpya kila mwaka.
Aliniambia hivi:
“Miujiza haikunitokea, niliitengeneza mwenyewe.”
Sasa Wewe Una Sababu Gani Ya Kukata Tamaa?
Huna sababu.
Una kila sababu ya kusimama.
Chukua kalamu na kuandika ndoto zako.
Zima data saa tatu usiku na kupanga kesho yako.
Na anza kutenda miujiza ya kweli kupitia nguvu yako ya ndani.
Kumbuka: Miujiza Haiporomoki.
Miujiza hutengenezwa.
Na hutengenezwa na watu kama wewe.
Watu wa kawaida lakini walioamua kuishi maisha ya ajabu.
ENDELEA KUTEMBELEA BLOG HII UTAJIFUNZA MENGI " MAISHA NA MAFANIKIO ( LIFE & YOU ) BLOG " PENDA KUNUNUA VITABU NA KUVISOMA UTAGUNDUA SIRI NYINGI ZA DUNIA HII.
No comments:
Post a Comment