Friday, May 16, 2025

MAKALA : SHERIA 100 ZA MAISHA NA MAFANIKIO -----NA MWL JAPHET MASATU ---- CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136

Kakaa/Dadaa Yangu...

‎Watu wengi wanakufa maskini si kwa sababu walizaliwa maskini…

‎Wanabaki maskini kwa sababu wanaishi bila sheria.

‎Wanapiga hatua moja mbele… halafu wanarudi tatu nyuma.

‎Siku zinaenda, miaka inasonga… maisha yanabaki pale pale.

‎Unaamka, unaenda kazini… lakini huna cha maana unaweka mezani.

‎Kila ukijaribu kusonga, kuna kitu kinakuvuta nyuma.

‎Unajua ni nini?

‎Huna ramani.

‎Huna sheria.

‎Huna mwelekeo.

‎Na Hapo Ndio Unatupwa Katika Kundi la “Wanaojitahidi Tu”

‎Unahangaika sana, lakini hakuna matokeo.

‎Unasoma vitabu, unaenda semina… lakini maisha yako hayabadiliki.

‎Una marafiki wanafanikiwa, lakini wewe bado unahaha.

‎Una ndoto, lakini hazina miguu.

‎Una malengo, lakini hayatimizwi.

‎Una nia nzuri, lakini hakuna mbinu.

‎Inachosha.

‎Inaumiza.

‎Inavunja moyo.

‎Unaweza ukajiona kama vile maisha yamekuchoka.

‎Kila kitu kinagoma.

‎Kila mtu anakupita.

‎Wewe unabaki unaangalia… ukiwa na maswali kuliko majibu.

‎Na Tatizo Halipo Kwenye Bahati… Lipo Kwenye Mfumo Wako

‎Wengi wanangoja bahati.

‎Wanasema: “Siku moja nitapanda juu.”

‎Hiyo siku haiji.

‎Kwa sababu hawafuati sheria.

‎Sheria za maisha.

‎Sheria za mafanikio.

‎Hakuna mafanikio bila sheria.

‎Kama vile gari halisafiri bila barabara.

‎Kama vile mti hauoti bila mizizi.

‎Maisha yanahitaji misingi.

‎Na misingi hiyo ni sheria.

‎Na sio sheria ngumu.

‎Ni zile rahisi.

‎Zenye mantiki.

‎Zenye mpangilio.

‎Lakini wengi hawajui.

‎Wengine wamewahi kusikia, lakini hawafuati.

‎Na ndio maana maisha yao ni kama gari lililoharibika breki, linaenda tu... bila mwelekeo.

‎Sasa Hii Ndio Dawa – Sheria 100 Za Maisha Ya Mafanikio

‎Nimekuandalia sheria hizi kwa jasho na damu.

‎Zimetoka kwa tajiri aliyewahi kulala kwenye dari la mabati.

‎Zimetoka kwa kijana aliyekua anauza vocha, leo ana kampuni.

‎Zimetoka kwa mwanamke aliyetelekezwa, leo ana biashara tano.

‎Sheria hizi ni silaha.

‎Zikupatie mwelekeo.

‎Zikupatie nguvu ya kupambana.

‎Zikusaidie kuachana na maisha ya mdundo mmoja.

‎Ukitaka kubadilisha maisha yako…

‎Ukitaka kuamka kutoka usingizini...

‎Sheria hizi ni Biblia / Juzuu yako mpya.

‎Sikiliza Story ya Kelvin Kijana Aliyeamua Kubadilika

‎Kelvin alikua anaishi Tandale, kwa mama wa kambo.

‎Alikua anafukuzwa shule kila siku —si kwa sababu ni mjinga, bali hakuwa na sare.

‎Alikua anaota kuwa mtu mkubwa, lakini mtaa ulimcheka.

‎Siku moja akapewa kitabu kidogo tu kilikua na "Sheria 100 Za Maisha Ya Mafanikio"

‎Akakisoma.

‎Akaanza kubadili tabia.

‎Akaanza kuamka mapema.

‎Akaanza kujifunza kila siku.

‎Akaacha kulalamika.

‎Leo Kelvin ni mkurugenzi wa kampuni inayouza bidhaa mitandaoni.

‎Analipa kodi.

‎Anasaidia mama yake.

‎Anafundisha vijana wenzie.

‎Na yeye anasema hivi:

‎"Maisha yanabadilika pale unapofuata sheria za maisha, si pale unapongoja msaada."

‎Sasa Ni Zamu Yako

‎Sheria 100 hizi si hadithi za kuburudisha.

‎Ni mashine ya kukutoa kwenye maisha ya hovyo hovyo.

‎Ni mwelekeo mpya wa mafanikio.

‎Ukiamua kuzifuata, hakuna kitakachokuzuia.

‎Ukiamua kuzipuuza, usilalamike maisha yanapokuchezea.

ENDELEA   KUPERUZI    NA   KUSOMA  BLOG  HII  "  MAISHA    NA   MAFANIKIO  (  AND  LIFE  )   BLOG " 

ILI  UJIFUNZE  SHERIA/  KANUNNI   ZA  KUFANIKIWA  KATIKA  MAISHA    YAKO.

No comments:

Post a Comment