Kakaa/Dadaa Yangu...
Watu wengi wanakufa maskini si kwa sababu walizaliwa maskini…
Wanabaki maskini kwa sababu wanaishi bila sheria.
Wanapiga hatua moja mbele… halafu wanarudi tatu nyuma.
Siku zinaenda, miaka inasonga… maisha yanabaki pale pale.
Unaamka, unaenda kazini… lakini huna cha maana unaweka mezani.
Kila ukijaribu kusonga, kuna kitu kinakuvuta nyuma.
Unajua ni nini?
Huna ramani.
Huna sheria.
Huna mwelekeo.
Na Hapo Ndio Unatupwa Katika Kundi la “Wanaojitahidi Tu”
Unahangaika sana, lakini hakuna matokeo.
Unasoma vitabu, unaenda semina… lakini maisha yako hayabadiliki.
Una marafiki wanafanikiwa, lakini wewe bado unahaha.
Una ndoto, lakini hazina miguu.
Una malengo, lakini hayatimizwi.
Una nia nzuri, lakini hakuna mbinu.
Inachosha.
Inaumiza.
Inavunja moyo.
Unaweza ukajiona kama vile maisha yamekuchoka.
Kila kitu kinagoma.
Kila mtu anakupita.
Wewe unabaki unaangalia… ukiwa na maswali kuliko majibu.
Na Tatizo Halipo Kwenye Bahati… Lipo Kwenye Mfumo Wako
Wengi wanangoja bahati.
Wanasema: “Siku moja nitapanda juu.”
Hiyo siku haiji.
Kwa sababu hawafuati sheria.
Sheria za maisha.
Sheria za mafanikio.
Hakuna mafanikio bila sheria.
Kama vile gari halisafiri bila barabara.
Kama vile mti hauoti bila mizizi.
Maisha yanahitaji misingi.
Na misingi hiyo ni sheria.
Na sio sheria ngumu.
Ni zile rahisi.
Zenye mantiki.
Zenye mpangilio.
Lakini wengi hawajui.
Wengine wamewahi kusikia, lakini hawafuati.
Na ndio maana maisha yao ni kama gari lililoharibika breki, linaenda tu... bila mwelekeo.
Sasa Hii Ndio Dawa – Sheria 100 Za Maisha Ya Mafanikio
Nimekuandalia sheria hizi kwa jasho na damu.
Zimetoka kwa tajiri aliyewahi kulala kwenye dari la mabati.
Zimetoka kwa kijana aliyekua anauza vocha, leo ana kampuni.
Zimetoka kwa mwanamke aliyetelekezwa, leo ana biashara tano.
Sheria hizi ni silaha.
Zikupatie mwelekeo.
Zikupatie nguvu ya kupambana.
Zikusaidie kuachana na maisha ya mdundo mmoja.
Ukitaka kubadilisha maisha yako…
Ukitaka kuamka kutoka usingizini...
Sheria hizi ni Biblia / Juzuu yako mpya.
Sikiliza Story ya Kelvin Kijana Aliyeamua Kubadilika
Kelvin alikua anaishi Tandale, kwa mama wa kambo.
Alikua anafukuzwa shule kila siku —si kwa sababu ni mjinga, bali hakuwa na sare.
Alikua anaota kuwa mtu mkubwa, lakini mtaa ulimcheka.
Siku moja akapewa kitabu kidogo tu kilikua na "Sheria 100 Za Maisha Ya Mafanikio"
Akakisoma.
Akaanza kubadili tabia.
Akaanza kuamka mapema.
Akaanza kujifunza kila siku.
Akaacha kulalamika.
Leo Kelvin ni mkurugenzi wa kampuni inayouza bidhaa mitandaoni.
Analipa kodi.
Anasaidia mama yake.
Anafundisha vijana wenzie.
Na yeye anasema hivi:
"Maisha yanabadilika pale unapofuata sheria za maisha, si pale unapongoja msaada."
Sasa Ni Zamu Yako
Sheria 100 hizi si hadithi za kuburudisha.
Ni mashine ya kukutoa kwenye maisha ya hovyo hovyo.
Ni mwelekeo mpya wa mafanikio.
Ukiamua kuzifuata, hakuna kitakachokuzuia.
Ukiamua kuzipuuza, usilalamike maisha yanapokuchezea.
ENDELEA KUPERUZI NA KUSOMA BLOG HII " MAISHA NA MAFANIKIO ( AND LIFE ) BLOG "
ILI UJIFUNZE SHERIA/ KANUNNI ZA KUFANIKIWA KATIKA MAISHA YAKO.
No comments:
Post a Comment