Thursday, May 22, 2025

MAKALA : MAISHA SI BAHATI NASIBU AU KUBET . NI RAMANNI YA MABADILIKO NA DIRA . NI MAAMUZI NA MAANDALIZI------NA MWL. JAPHET MASATU------TANZANIA -------FRIKA YA MASHARIKI--------CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136

 Kakaa/Dadaa....

‎Unajua shida kubwa inayowakumba wengi?

Wanaamka kila siku…

‎Wanakimbizana kama mchwa waliomwagiwa maji…

‎Lakini hawajui wanakimbilia wapi.

‎Kila siku ni kujituma…

‎Lakini mwisho wa mwezi, mfuko ni kama shimo la panya.

‎Kila mwaka unakatika…

‎Lakini hakuna mabadiliko ya maana.

‎Wengi wako kwenye 'autopilot' ya maisha.

‎Wanajisukuma tu.

‎Wakiamini ipo siku mambo yatajileta.

‎Mambo hayajileti. Wewe ndo lazima uyasogeze.

‎Hii Inatisha Kidogo…

‎Unaamka ukiwa na nguvu.

‎Unaota mafanikio.

‎Lakini kila jioni, unarudi na uchovu tu.

‎No progress.

‎No peace of mind.

‎Unasema utabadilika kesho.

‎Kesho ikifika, unafanya yaleyale.

‎Ni kama umefungwa pingu zisizoonekana.

‎Hii ni hatari sana.

‎Inaua ndoto zako taratibu bila kelele.

‎Alafu unakuja kushangaa:

‎“Mbona maisha yananizunguka?”

‎Ni kwa sababu hakuna mwongozo.

‎Kuna Uongo Mmoja Mkubwa…

‎Eti “kuwa na bidii, utafanikiwa.”

‎Wongo huo.

‎Watu wengi wana bidii kuliko hata gari la kubeba mawe.

‎Lakini wako pale pale.

‎Tatizo si bidii.

‎Tatizo ni kutokuwa na DIRA.

‎Hakuna ramani.

‎Hakuna mwongozo.

‎Na kama hujui unakokwenda…

‎Hutajua hata ukifika.

Sasa Sikiliza Vizuri…

‎Maisha yako yanahitaji mfumo.

‎Mfumo wa kuweka malengo.

‎Kujijua wewe ni nani.

‎Unataka nini.

‎Na kwa nini unakitaka.

‎Halafu?

‎Anza kupanga hatua ndogo ndogo.

‎Kila siku.

‎Kidogo kidogo hadi kikamilike.

‎Na muhimu zaidi, tafuta maarifa ya kweli.

‎Si porojo.

‎Maarifa ya watu waliopitia moto.

‎Walioungua.

‎Wakaamka.

‎Wakasimama tena.

‎Ngoja Nikupe Kisa Cha Huyu Bwana Mdogo Hapa…

‎Kuna Bwana Mdogo mmoja mtaani kwetu Anaitwa Baba T.

‎‎Miaka mitano iliyopita alikuwa anauza vocha na peremende stendi.

‎Maskini alikua anavaa viatu vilivyochanika…

‎Watu walimcheka.

‎Lakini kuna siku moja aliniambia:

‎“Bro, nimeshaamua. Sitaki kufa maskini. Nataka mafanikio ya ukweli.”

‎Akanunua daftari.

‎Akaandika malengo yake.

‎Akasoma vitabu.

‎Akatafuta mentor.

‎Akaanza kuandika kila kitu anachotumia.

‎Leo hii?

‎Ana duka lake la simu.

‎Anauza online.

‎Anatoa ushauri kwa vijana wengine.

‎Na bado ni yule yule – Baba T ila mwenye mwongozo mpya wa maisha.

‎Na Wewe Unaweza Kubadilika Leo…

‎Ukiamua, unaweza.

‎Ukiwa na mwongozo sahihi, maisha yanabadilika.

‎Unapunguza makosa.

‎Unafupisha safari ya mateso.

‎Unapanda ngazi haraka.

‎Chukua hatua.

‎Andika malengo yako.

‎Soma kila siku.

‎Tafuta watu wanaojua kuliko wewe.

‎Achana na kelele za mtaani.

‎Focus.

‎Maisha ni yako.

‎Na hakuna atakayeyaishi kwa niaba yako.

‎Unataka mafanikio ya kweli?

‎Tafuta mwongozo.

‎Fuata mfumo.

‎Jitahidi bila kusahau mwelekeo.

‎Maisha si bahati.

‎Ni maamuzi na maandalizi.

ENDELEA   KUSOMA  HAPA   UTAPATA    RAMANI  YA  MABADILIKO   NA  DIRA    YA  MAISHA  YAKO. 

No comments:

Post a Comment