Kakaa/Dadaa....
Unajua shida kubwa inayowakumba wengi?
Wanaamka kila siku…
Wanakimbizana kama mchwa waliomwagiwa maji…
Lakini hawajui wanakimbilia wapi.
Kila siku ni kujituma…
Lakini mwisho wa mwezi, mfuko ni kama shimo la panya.
Kila mwaka unakatika…
Lakini hakuna mabadiliko ya maana.
Wengi wako kwenye 'autopilot' ya maisha.
Wanajisukuma tu.
Wakiamini ipo siku mambo yatajileta.
Mambo hayajileti. Wewe ndo lazima uyasogeze.
Hii Inatisha Kidogo…
Unaamka ukiwa na nguvu.
Unaota mafanikio.
Lakini kila jioni, unarudi na uchovu tu.
No progress.
No peace of mind.
Unasema utabadilika kesho.
Kesho ikifika, unafanya yaleyale.
Ni kama umefungwa pingu zisizoonekana.
Hii ni hatari sana.
Inaua ndoto zako taratibu bila kelele.
Alafu unakuja kushangaa:
“Mbona maisha yananizunguka?”
Ni kwa sababu hakuna mwongozo.
Kuna Uongo Mmoja Mkubwa…
Eti “kuwa na bidii, utafanikiwa.”
Wongo huo.
Watu wengi wana bidii kuliko hata gari la kubeba mawe.
Lakini wako pale pale.
Tatizo si bidii.
Tatizo ni kutokuwa na DIRA.
Hakuna ramani.
Hakuna mwongozo.
Na kama hujui unakokwenda…
Hutajua hata ukifika.
Sasa Sikiliza Vizuri…
Maisha yako yanahitaji mfumo.
Mfumo wa kuweka malengo.
Kujijua wewe ni nani.
Unataka nini.
Na kwa nini unakitaka.
Halafu?
Anza kupanga hatua ndogo ndogo.
Kila siku.
Kidogo kidogo hadi kikamilike.
Na muhimu zaidi, tafuta maarifa ya kweli.
Si porojo.
Maarifa ya watu waliopitia moto.
Walioungua.
Wakaamka.
Wakasimama tena.
Ngoja Nikupe Kisa Cha Huyu Bwana Mdogo Hapa…
Kuna Bwana Mdogo mmoja mtaani kwetu Anaitwa Baba T.
Miaka mitano iliyopita alikuwa anauza vocha na peremende stendi.
Maskini alikua anavaa viatu vilivyochanika…
Watu walimcheka.
Lakini kuna siku moja aliniambia:
“Bro, nimeshaamua. Sitaki kufa maskini. Nataka mafanikio ya ukweli.”
Akanunua daftari.
Akaandika malengo yake.
Akasoma vitabu.
Akatafuta mentor.
Akaanza kuandika kila kitu anachotumia.
Leo hii?
Ana duka lake la simu.
Anauza online.
Anatoa ushauri kwa vijana wengine.
Na bado ni yule yule – Baba T ila mwenye mwongozo mpya wa maisha.
Na Wewe Unaweza Kubadilika Leo…
Ukiamua, unaweza.
Ukiwa na mwongozo sahihi, maisha yanabadilika.
Unapunguza makosa.
Unafupisha safari ya mateso.
Unapanda ngazi haraka.
Chukua hatua.
Andika malengo yako.
Soma kila siku.
Tafuta watu wanaojua kuliko wewe.
Achana na kelele za mtaani.
Focus.
Maisha ni yako.
Na hakuna atakayeyaishi kwa niaba yako.
Unataka mafanikio ya kweli?
Tafuta mwongozo.
Fuata mfumo.
Jitahidi bila kusahau mwelekeo.
Maisha si bahati.
Ni maamuzi na maandalizi.
ENDELEA KUSOMA HAPA UTAPATA RAMANI YA MABADILIKO NA DIRA YA MAISHA YAKO.
No comments:
Post a Comment