Basi Sikiliza Hii Siri Ya Wale Wanaofanikiwa Na Kipato Kidogo!…
Mpendwa Rafiki,
Wengi wetu tunasoma, tunahangaika, tunachapa kazi usiku na mchana,
...lakini hela inavyopatikana si sawa na inavyopotea.
Kule shule waliwahi kukufundisha (compound interest), lakini hawakuwahi kukufundisha kutokutumia hela hovyo wiki ya mshahara.
Ujuzi wa fedha ni uwezo wa....
Kujua hela yako inaingia wapi na inatoka vipi,
Kujua muda gani ni wa matumizi na muda gani ni wa kuweka akiba,
Kuweza kupangilia matumizi kabla mshahara haujalala kwenye simu.
Na ukweli mchungu ni huu:
Si kiasi cha hela unachopata kinachokufanya uwe vizuri, ni vile unavyotumia hiyo hela.
Ebu Niambie, Wewe Uko Wapi?
Hebu kuwa mkweli...
Umewahi kupata mshahara, halafu wiki ya pili unakopa kwa mpesa?
Umewahi kuwa na hela nzuri mkononi, ukajisikia *bosi* – halafu baada ya wiki mbili ukawa broke kama mwanafunzi wa form one?
Umewahi kujiambia, *Mwezi huu nitapanga matumizi vizuri,* lakini siku ya tarehe 5 mshahara ushakwisha?
Kama jibu lako ni *ndiyo* hata mara moja,
... basi wewe si mgeni kwenye kasheshe hili la kukosa ujuzi wa fedha.
Waliokudanganya Kwamba…
Hela inaisha tu bro, hakuna jinsi ya kuizuia.
Maisha ni magumu kwa kila mtu, hakuna anayefanikiwa bila kuibia watu.
Weka hela benki? Hela ya matumizi si ya kuwekwa tu!
Hizi ni kauli tunazojidanganya nazo kila siku.
Lakini ukweli ni huu....
Hela yako haitoshi si kwa sababu hujui kupata, ni kwa sababu hujui kuitunza.
Na hakuna mtu atakayekuja kukuokoa hadi uanze kujifunza wewe mwenyewe.
Na Hii Ndio Njia....
Ujuzi wa fedha sio somo gumu kama hesabu za algebra.
Ni mambo madogo sana ambayo ukiyajua, unabadilika kama saa.
Zifuatazo Ni Njia Tatu (3) Rahisi Unazoweza Kuanza Kuzitumia.
1. Tenga asilimia 10 ya kipato chako mara tu inapopatikana.
Hata kama ni buku tano, anzia hapo.
2. Andika matumizi yako ya kila siku.
Ukishangaa unavyonunua vinywaji vya 3,000 kila jioni, utajua hela zako zinapotelea wapi.
3. Jifunze njia za kuongeza kipato bila kuongeza kazi.
Huu ndio wakati wa kujua kutumia maarifa yako, sio nguvu zako tu.
Chukua Hatua....
Bro, Dada, ukikaa unasema ‘nitabadilika tu muda ukifika’, muda wenyewe haufiki.
Muda upo, ila wewe ndo hujaamka.
Kumbuka;
Maisha yako ya kesho yanatengenezwa na maamuzi yako ya leo, si mshahara wako wa mwezi ujao.
No comments:
Post a Comment