Mpendwa Rafiki,
Watu wengi wanaamini kuwa ili uanze kujenga utajiri, lazima uwe na hela nyingi ,milioni tano, kumi, au hata zaidi.
Wengine wanasema, *Mimi ni wa mshahara wa chini, siwezi kufika mbali.*
Lakini ukweli ni kwamba watu wengi hawajui kitu kimoja muhimu: nguvu ya *buku* moja tu.
Buku ambayo unaitumia bila mpango kila siku, inaweza kuwa tiketi yako ya kutoka kwenye umaskini hadi kwenye uhuru wa kifedha.
Ni mara ngapi umetumia buku kununua soda, chipsi, vocha, au kitu usichohitaji halafu ukaishia kusema, *Ah ni buku tu*?
Halafu mwisho wa mwezi unakuta umekopa, umeshindwa kuwekeza, hata akiba huna.
Inasikitisha, siyo? Sasa fikiria, kama kila siku unapoteza buku moja tu, ndani ya mwezi umepoteza buku 30.
Mwaka mzima? Hiyo ni buku 360,000!
Na kama ungezitumia kuanzisha biashara ndogo au kuwekeza, ungekuwa mbali.
Hiyo ndiyo nguvu tuliyo nayo lakini hatuitumii.
Wengi tulifundishwa kwamba hela nyingi ndiyo hujenga utajiri.
Tukaanza kusubiri *mshahara mkubwa,* *tenda kubwa za kibiashara," au *mjomba wa Dubai.*
Lakini hizo ni hadithi.
Angalia Uhalisia : Hela hujengeka kwa nidhamu na mpango, siyo kiasi.
Watu matajiri hawakuanza na mamilioni.
Walitumia kile kidogo walichokuwa nacho kwa akili.
Walitunza, wakawekeza, wakaendeleza.
Kwa hiyo, tukiachana na dhana ya *nitakapoanza kupata hela kubwa,* tunaweza kuanza safari ya utajiri hata leo,
Kwa ile buku tuliyonayo mfukoni.
Sasa hebu tuweke wazi, unataka kujenga utajiri kwa kutumia buku?
Hizi hapa ni hatua 3 rahisi lakini zenye nguvu:
a. Weka akiba ya buku 1 kila siku:
Tafuta kopo, lipachike mahali salama. Kila siku, kabla ya kutumia hela yoyote, tengeneza tabia ya kuweka buku moja pembeni.
b. Anza kuwekeza kidogo:
Baada ya mwezi mmoja, utakuwa na zaidi ya buku 30.
Tafuta biashara ndogo, lipia kozi fupi, au nunua bidhaa za kuuza mitandaoni.
c. Wekeza kwenye maarifa:
Buku moja inaweza kununua data. Tumia hiyo kusoma makala, kuangalia video za elimu ya fedha, au kusikiliza podcast. Maarifa ni mtaji.
Kuna jamaa yangu mmoja anaitwa Mussa,
Alikuwa na mshahara wa laki na 20 kwa mwezi.
Alikuwa na majukumu mengi lakini alianza kuweka buku moja kila siku.
Miezi sita baadaye, alikuwa na buku 180.
Akanunua kahawa na kuanza kuuza kikombe ofisini kwao, faida yake ilikuwa buku 2 kwa kila kikombe.
Siku moja akaniambia,
*Bro, ile tabia ya kuweka buku moja kwa siku ilinibadilishia maisha.
Sasa hivi nina biashara mbili na bado naendelea kuweka akiba!*
Ukweli ni huu:
Buku moja inaweza kuwa mtaji wa maisha yako mapya.
Usidharau kile kidogo, ndani yake kuna nguvu kubwa sana ya kifedha.
Anza leo, anza sasa.
Usisubiri mshahara mkubwa, anza na buku!
Kumbuka; Buku yako ya leo, ndiyo utajiri wako wa kesho.
No comments:
Post a Comment