Saturday, May 8, 2021

KWA NINI WENZAKO WANAFANIKIWA NA WEWE UNABAKI ULIPO ??

Rafiki yangu mpendwa,

Huenda hili ni swali umekuwa unajiuliza kwa muda mrefu.

Unapoona wenzako ambao mmeanza kazi pamoja, kazi ambayo ni sawa na malipo yanalingana, ila wao wanapiga hatua huku wewe unabaki nyuma.

Au ni kwenye biashara ambapo unaona wengine wanaofanya biashara ya aina hiyo na mlioanzia kwa kiwango sawa wanapiga hatua wewe unabaki ulipo.

Watu wa kawaida, ambao hawawezi kufanikiwa huwa wanatafuta sababu za kuhalalisha hali zao.

Wanajiambia wale waliopiga hatua wamependelewa au wamepata bahati au kuna njia zisizo sahihi wanazotumia.

Ni kweli hivyo vinaweza kuchangia kwa namna fulani, lakini siyo sababu hasa.

Wale waliopiga hatua kuliko wewe kuna mambo mawili yanayowatofautisha na wewe ambayo kama hutayajua na kuyafanyia kazi, utaendelea kubaki hapo ulipo.

Jambo la kwanza ni namna wanavyofikiri.

Kuna watu wanapewa urithi na wanaweza kuuendeleza na kufanikiwa. Wakati kuna wengine wanapewa urithi na kuupoteza wote.




Kinachowatofautisha watu hau siyo wanachopewa, bali namna wanavyokichukulia.

Namna mtu anavyofikiri inaathiri sana yale anayofanya kwenye maisha yake. Wanaopiga hatua wanafikiri kwa uchanya, uwezekano na ukuaji.

Kwenye fikra zao wanaona picha kubwa ambayo wanapambana kuifikia. Wanaamini bila ya shaka yoyote kwamba watafikia picha hiyo.

Na pale wanapokutana na vikwazo mbalimbali, wanajua siyo mwishi wa safari, bali wanaimarishwa ili waweze kupokea makubwa.

Wasiofajikiwa wao hufikiri kwa udogo, uhasi na kutokuwezekana. Hawana picha kubwa, wanaona mengi ni mabaya na wanapokutana na changamoto wanaona ni mwisho.

Kama hutabadili namna unavyofikiri hutaweza kupiga hatua kubwa kwenye maisha yako.

Jambo la pili ni namna watu wanavyofanya.

Kama watu wawili wanafanya kazi au biashara ya aina moja na mmoja akapiga hatua kuliko mwingine, ukimuangalia utaona wazi kuna vitu anafanya tofauti.




Wanaofanikiwa na kupiga hatua wanafanya mambo yao kwa namba ya tofauti kabisa.

Wana viwango walivyojiwekea katika kufanya, viwango ambavyo ni vya tofauti kabisa na wengine.

Wanakwenda hatua ya ziada na kutoa thamani kubwa tofauti na wanavyotegemewa kufanya.

Wanajua mafanikio ni mbio za muda mrefu na hivyo hujipanga vizuri kwenye ufanyaji wao.

Kamwe hawaahirishi yale waliyopanga kufanya, wana nidhamu kubwa ya kutekeleza kama walivyopanga.

Wale wasiofanikiwa huwa wanafanya mambo yao kwa mazoea, hawawezi kujituma wenyewe mpaka wasukumwe na ni wazuri sana kwenye kuahirisha yale waliyopanga kufanya.

Kama hutajifunza namna waliofanikiwa wanavyofanya na wewe kufanya kwa namna hiyo, utaendelea kubaki pale ulipo.

Habari njema kwako rafiki yangu ni una nafasi nzuri ya kujifunza kwa kina namna ya kufikiri na kutenda ili uweze kufanikiwa sana.

JIUNGE   NA  DARASA  ONLINE  --UJIFUNZE    KWA   KINA    NA  VITENDO

JIFUNZE  ,ELIMIKA   NA   CHUKUA  HATUA.

TUWASILIANE  SASA    KWA  MAELEKEZO  ZAIDI

NA  KOCHA  MWL.  JAPHET   MASATU

WhatsApp  + 255 716  924 136  /   +  255  755 400 128  /  + 255 688 361  539

EMAIL : japhetmasatuy@gmail.com




No comments:

Post a Comment