Thursday, May 13, 2021

ELIMU YA MSINGI YA BIASHARA ITAKAYOKUPA MAFANIKIO MAKUBWA NDANI YA MWAKA MMOJA KULIKO WASHINDANI WAKO.

Nenda shule, soma kwa bidii na ufaulu vizuri.

Utapata kazi inayokulipa vizuri na utakuwa na maisha mazuri.

Huu ulikuwa ushauri maarufu na uliofanya kazi kwenye karne ya 20 na muongo wa kwanza wa karne ya 21.

Lakini sasa mambo yamebadilika kabisa,

Waliofuata ushauri huo ni wengi, wameenda shule, wamesoma kwa bidii,

Wakahitimu na ufaulu mkubwa, lakini kazi hakuna.

Karne ya 21 imekuwa na mapinduzi makubwa ya kiteknolojia kiasi kwamba nafasi za kazi ni chache kuliko wahitaji wanaozitaka nafasi hizo.

Hivyo licha ya juhudi mbalimbali zinazofanyika na serikali mbalimbali duniani,

Bado tatizo la kukosekana kwa ajira linaendelea kukua kila siku.

Pamoja na tatizo la kukosekana kwa ajira kuwepo,

Bado ushauri unaendelea na vyuo vinaendelea kuzalisha wahitimu anaotegemea kupata ajira.

Wanafunzi wanapohitimu na kukaa mtaani kutafuta kazi bila mafanikio,

Wanapewa ushauri mwingine ambao unawachanganya zaidi.

Wanaambiwa usisubiri tu kuajiriwa,

Jiajiri mwenyewe, anzisha biashara.

Hapo ndipo wanachanganyikiwa zaidi,

Mtu amekaa darasani kwa zaidi ya miaka 15 na miaka yote hiyo alikuwa anafundishwa kuja kuwa mwajiriwa.

Halafu amehitimu anaambiwa ajiajiri?

Mtu hana maandalizi yoyote katika kujiajiri au kuanzisha biashara,

Hivyo hata pale wanaposaidiwa mtaji wa kuanza biashara,

 zinaishia kufa.

Ukweli ni kwamba, ushauri wa karne ya 20 haufanyi tena kazi kwenye karne ya 21 na watu hawajaandaliwa kukabiliana na mabadiliko haya.

Njia ya uhakika kabisa ya kuingiza kipato kwenye karne hii ya 21 ni kufanya biashara.

Njia hii haina ukomo kwenye ukuaji au kipato,

Lakini siyo njia rahisi ambayo mtu atafanikiwa kwa kuambiwa tu mara moja.

Unahitaji kupata mafunzo sahihi ndiyo uweze kufanikiwa kwenye kuanzisha na kukuza biashara inayokupa kipato kisicho na ukomo na pia kukupa uhuru wako.

Miaka 15 uliyokaa darasani, haikukufundisha hilo.

Lakini una bahati, kuna njia ya kujifunza yale ya msingi kabisa kuhusu biashara kwa njia rahisi,

Huku ukielewa na kuwa na hatua za kuchukua.

 

JIUNGE     NA   " DARASA   ONLINE " SASA  HUJACHELEWA.

 

Wasiliana  na  KOCHA  MWL.  JAPHET  MASATU

WhatsApp + 255 716  924 136 /  + 255 755 400 128 /  + 255 688 361 539  /  + 255 629748  937

EMAIL :  japhetmasatu@gmail.com

 

No comments:

Post a Comment