Sunday, October 4, 2020

UTABIRI UTAKAOKUSAIDIA KWENYE MAISHA YAKO ?

Utabiri wa wataalamu ni wa uongo na umekuwa na upotoshaji mkubwa, je unawezaje kupanga mambo yako na kuchukua hatua zitakazokuwezesha kufanikiwa zaidi?

Kuna aina moja tu ya utabiri unaopaswa kuufanya mwenyewe na kuuishi kila siku. Utabiri huo ni huu kwamba kuna mabadiliko yanakuja, kwamba kila unachofanya sasa, kitaondoka na kupotea kabisa, hivyo kila mara uwe na maandalizi sahihi ya kuweza kukabiliana na mabadiliko hayo.

Kama umeajiriwa, kila siku ishi kwa kufikiri kesho unaweza kuamka na ajira yako isiwepo, kisha jiulize maisha yako yataendaje?

Kama unafanya biashara, kila siku ishi na utabiri kwamba kesho biashara hiyo haitakuwepo kabisa, halafu ona maisha yako yataendaje katika hali hiyo.

Utabiri huu unakufanya uwe na njia mbadala za kukabiliana na maisha yako ili chochote kinachotokea, isiwe mshangao kwako, badala yake iwe ni kitu ulichotegemea na kinachofuata ni kuchukua hatua ulizokuwa umepanga.

Kwa kuishi kwa namna hii, hutatikiswa na chochote, hutababaishwa na utabiri wa wengine na maisha yako yataendelea kwenda vizuri bila ya kutegemea nini kinaendelea.

No comments:

Post a Comment