Thursday, July 2, 2015

USIWAZE KUKOSA , WAZA KUPATA--AKILI INA NGUVU YA KUWEKA PICHA , KATIKA UHALISIA

AKILI  ina  nguvu  ya   kutengeneza  picha  ikawa  kweli. HUAMINI ? Ni  kwamba ,  PINDI  MAWAZO   YAKO  YANAPOKAZIA  KUPATA  KITU ,  NI  UHAKIKA  UTAKIPATA. Lakini ,  muhimu   ni   kuendelea  kukazia  mawzo  hayo ,  kwenye  kitu  hicho  bila   ya   kuhama  hama.

KUCHORA  PICHA   AKILINI , ni  njia   iliyofanyiwa  utafiti    na  imewaletea   watu   mafanikio.  KWA  NINI ?

    UNAPOWAZIA  KILA   SIKU   KUPATA   KITU  FULANI , BASI   NI  KAMA   SAWA    UMEJIPA   KAZI   YA   KUKIPATA.  Njia   za   kupata    kitu  hicho  lazima   zitaibuka.

     KWA   MFANO , umetunga   taswira     unamiliki    GARI  LA   KISASA aina   ya   RANGE  ROVER  VOGUE  na   uko   na  jamaa   na   ndugu    wanakupongeza ,  unadhani    utaishia  hapo ?   HAPANA !  Ni  hivi. Unaweza   kujikuta   ukilazimika   kuzungumza  na  watu   mbalimbali  ambao    unaona    kwamba   wanaweza    kukusaidia.  KWA   NINI ?  
      Kwa   sababu   kuna   nguvu   iko  ndani    ya   mwili   wako   ambayo   ilichora    picha   ya  GARI   LA  KISASA aina    ya    RANGE   ROVER  VOGUE nzuri   na   ndugu   wanakupongeza ,  na  sasa    inataka {kitu}  GARI  LA  KISASA  aina   ya   RANGE   ROVER   VOGUE   hiyo   itokee   kweli.
 
 
    KAMA  PIA , utatunga   taswira   kwamba    UNAMILIKI  PESA  NYINGI ,akili   itakuwa   na   FURAHA  na   AMANI. Ajabu   na   kweli !  Baadaye   unaweza    kumiliki   pesa   nyingi. Hii  ni   kwa   sababu ,  AKILI  INA   NGUVU   YA  KUTENGENEZA   PICHA   AMBAYO   BAADAYE  INAWEZA   KUWA    KWELI. Tunapotengeneza  picha  kuwa  tumepata  pesa , tunachochea  nguvu  ya   ajabu  kutoka   miilini  mwetu , ambayo  inataka  pesa  hizo   zitokee   kweli  katika   uhalisia. Huwezi  kupata  PESA  ilhali   mawazo  yako , yametawaliwa  na  kukosa   PESA.  Anza     kufanya   leo  ndugu     yangu , utaona    ajabu   kubwa !

WATANZANIA  WENGI  HAWAAMINI  KUHUSU  KUTUNGA   TASWIRA AU  PICHA ! KWANINI ?
Kuna  baadhi   ya  watanzania   ambao   huona   kuwa   kutunga  taswira  au  picha  hakuna  maana. Hawa   ni  kwa   sababu  hawafahamu  kuhusu   jambo  hili. 

JIFUNZE  SIRI  HII : WASANII  wengi ,  WAANDISHI  na  WANASAYANSI  wameweza  kufanya   maajabu  makubwa  kutokana  na   utungaji   wa   taswira au   picha.

MWANARIADHA  mmoja  wa  nchini  KENYA , alishinda  MAREKANI  medani  ya   dhahabu  katika  shindano  la  riadha  mwaka  1999.Alipohojiwa  kueleza     siri   ya   ushindi  wake , alisema :  

      "Muda  mchache  kabla   sijaingia   katika   uwanja  wa  mashindano ,  nilivuta   taswira   kwa   kuwaletea   washindani   wangu   akilini. Nilichora  picha  akilini   kuwa   tuko   uwanjani  tunakimbia   na   ninawapita    wote. "
 
 

Wanariadha   ambao  hufanya  zoezi  hili  la  kutunga    taswira   mara  nyingi  wamefanya   vizuri   na   kutunikiwa   zawadi.


KWANINI  WANAMICHEZO   WA  TANZANIA  HUFANYA  VIBAYA  KATIKA  MICHEZO ? Sababu  inayopelekea   watanzania   kushindwa  katika  michezo  mbalimbali   ni  kwamba  hawaamini   au  hawajui   jinsi   gani  suala  la  utungaji  taswira   au   picha kabla  ya  kuingia  uwanja  wa mashindano  linavyofanya   kazi na  kuleta   matokeo   mazuri ya   ushindi ! Wanamichezo   wengi  wa  tanzania  huwa  hawana   taswira   au  picha  ya  ushindi akilini  mwao. Wengi  huwa  wana  picha  au   taswira  ya  kushindwa , kukata   tamaa ,  hofu  hutawala  vichwani { fear  complex },huwaza  mambo   ya  starehe  zaidi ! matokeo  ni  kushindwa   vibaya !

USHAURI WANGU  KWA  WANAMICHEZO  WA  TANZANIA. Licha  ya  kukaa  kambini   kwa  muda  mrefu , kufanya   mazoezi  mengi , kupata  maelekezo  ya  kutosha  toka  kwa  waalimu   wa   michezo ,kupata   mahitaji  yote   yanayotakiwa  kambini , hiyo  haitoshi ! 

 KWANINI ? Kama  akili  imekata  tamaa, inawaza   kushindwa ,  inajenga  hofu  badala  ya  kujenga  hali   ya  kujiamini ,ushindi,  haina   taswira   au   picha   ya  ushindi   ni  kazi   bure . Maana  yake   ni  kwamba   Unashughulika   na   mwili  kuupatia   mahitaji   yake   lakini  unasahau   kushughulika  na  akili    yako, ambacho   ndicho  kitu   cha   muhimu  zaidi   ndugu  yangu    mpendwa.AKILI  INA   NGUVU    YA   KUTENGENEZA   PICHA   AMBAYO  UNAITENGENEZA  AKILINI  MWAKO   NA  BAADAYE   INAWEZA   KUWA   KWELI. Kuchora   picha   akilini , ni  njia   iliyofanyiwa  utafiti   na  imewaletea   watu   mbalimbali   mafanikio  makubwa. Kwa   mfano   Mwanasayansi  maarufu  ARCHIMEDES  alikuwa  akitumia       mbinu  ya  utungaji  taswira au  picha  katika tafiti  zake  na   kweli alifanikiwa  sana. 
Kama   unapenda  kuwa    mchezaji  fulani maarufu   ulimwenguni, kwa   mfano  pele  hebu   chukua  picha  yake   na  uiweke  ukutani  au   sehemu  ambayo  unadhani unaweza  kuiona  kila  siku. Na  tamka  maneno   ya  ushindi kila  siku,  waweza  kusema ,  "  Nataka  kuwa  bingwa  kaika  mchezo  wa  mpira  wa   miguu kama pele au  zaidi  ya  yeye ."  Utaniambia  ndugu  yangu   maneno  haya  hayapotei  bure  yana  athari  sana katika  akili  zetu"  ANZA  KUFANYA  LEO  , UTAONA  AJABU  KUBWA !

EWE   MWANAMICHEZO FANYA  HIVI :  Kabla  hujaingia  katika  uwanja  wa  mashindano , vuta   taswira  au  picha   kwa  kuwaleta   washindani   wako   akilini. Chora  picha  akilini  mwako   kuwa  mko   uwanjani  unawanyanyasa  washindani   wako   kwa  kuutawala  mpira.Ni   hivi , Njia    ya   ushindi  zitaibuka, kuna  nguvu   itataka  iwe  kweli, njia  zitajitokeza, utaamsha  nguvu  iliyolalal. FANYA  LEO UONE.

No comments:

Post a Comment