Tuesday, January 6, 2015

MWANAMUZIKI ANAVYOWEZA KUFAIDIKA NA BIASHARA YA MUZIKI.

Mwanamuziki   Na   Biashara  Ya  Muziki
 
 Marehemu  Dr.  Remmy  Ongala wa  Tanzania  alipata  Mafanikio  makubwa   katika  sanaa  ya  Muziki. Nyimbo  zake   zinakumbukwa  mpaka  leo  kwa   ujumbe  wenye   mafundisho. 
Biashara  ya muziki  ni  nzuri  kwa  mwanamuziki  akiwa  na  kipaji  na  akijua  namna  ya  kukiendeleza  kipaji  chake.Anaweza   kuwa   mwimbaji, Mpigaji  wa  chombo  Fulani  cha  muziki  kama  vile  gitaa , filimbi , tarumbeta, zumari , kinanda  au  ngoma. Baada  ya kujua kipaji chako  unapaswa  kukiendeleza  kipaji  hicho  kwa  kusomea  muziki  au  kujifunza  kutoka  kwa  wanamuziki  mahiri   na  ukishaujua  muziki unaweza  kuanzisha  bendi  au  kutafuta   studio  ya  kurekodi  muziki  wako  na   kuuza  kanda  zako. Katika  kurekodi  unapaswa  kuwa  na  fedha  za  kulipa  gharama  za  kurekodi. Kama  huna  fedha  unaweza  kutafuta   mfadhili  na  ukaingia  naye  mkataba  wa  kugawana  mapato  ya   muziki  ambapo  itabidi  litafutwe   soko   na  kutangazwa.Mbinu  inayotumika  kutangazwa  ni  kupeleka  kanda  hiyo   katika  studio  za  redio, ikapigwa  sana  na  kusifiwa.  Baada  ya  hapo  mwanamuziki  huandaa  uzinduzi  wa  kanda   yake.  Ili  kuvuta  wateja unaweza, kufanya   hivi : Unaweza  kufanya  ziara   ya   mikoani   kutangaza  muziki  wako  na  kuuza  kanda     zako.

Matatizo  ya   biashara  ya  muziki   kwa  wanamuziki  ni :  kazi   zao   kudhulumiwa  na   wafadhili /  wakala , kukosekana  kwa  makali  katika  utekelezaji  wa  sheria  ya    haki  miliki  katika   kutoa  adhabu  kwa   wanaoiba  au   kurudufu  kanda ,  wanamuziki  kulewa   sifa  na   kujisahau  hivyo   kuporomoka  kimuziki ,  ulevi  wa  pombe   na   madawa   ya  kulevya  hivyo   kuharibu   maendeleo   ya  muziki ,  kuwa  na  wapenzi  wengi  kutokana   na  umaarufu  baada  ya  kupapatikiwa  na  washabiki , kuwa   na   matumizi  makubwa   na  kushindwa  kuweka  AKIBA  na   kadhalika.  Ili  kukabiliana  na   matatizo  haya    mwanamuziki  anapaswa  kuwa   MBUNIFU ,  afanyaye   kazi  yake  kwa   bidii ,  awe  na  malengo  makubwa  ya  kuwa   mwanamuziki  wa  kimataifa.Pia  ajiepushe  na  tabia  mbaya   kama  vile  ulevi  wa  pombe  na  utumiaji  wa   madawa  ya  kulevya. AWEKE  fedha  zake   AKIBA  angalau  asilimia  10%  kwa   ajili  ya   kuwekeza     na   matumizi  ya  baadaye !!!
 

No comments:

Post a Comment