Wednesday, January 7, 2015

MMILIKI WA BENDI ANAVYOWEZA KUFAIDIKA NA BIASHARA YA MUZIKI.

Mmiliki  wa  Bendi Na  Biashara  Ya   Muziki
 

  Asha  Baraka  mmiliki  wa  bendi  ya  Twanga pepeta ,Tanzania amepata mafanikio  makubwa   katika  sanaa  ya  Muziki !!
Ili  kuwa  mmiliki  wa   bendi  unapaswa   uwe   na   mapenzi  na  Muziki.  Wakati   mwingine  wamiliki   wa  bendi  za  muziki  wanakuwa  ni  wanamuziki. Biashara  hii  inahitaji  mtaji  mkubwa  kununulia  vyombo   vya  muziki  ambavyo  ni  aghali  sana  na  pia  kuwalipa  mshahara   wanamuziki.Biashara  hii  inahitaji  ubunifu  ili  uweze   kupata   fedha.Biashara   hii  inaweza  kuingiza  mapato  kwa   njia  mbalimbali   pamoja  na   viingilio  kwenye  kumbi  za   starehe, mialiko  ya   kutumbuiza   katika  sherehe , mikataba  ya  kupiga  muziki    katika   kumbi  au  mahoteli   kwa   malipo  maalumu  pamoja na   mauzo  ya   kanda  za   muziki.
  
Matatizo  ya  biashara  hii  ni : kukosekana  kwa   ubunifu  kwa  mmiliki  wa  bendi  au   wanamuziki, hivyo  kuwa  kuwa  gharama  kubwa  za  uendeshaji, uchakavu  wa  vyombo , maendeleo  ya  teknolojia ambapo   mwanamuziki  anaweza  kwenda  studio  na   kurekodi  nyimbo  zake  hivyo  kuondokana  na  umuhimu  wa  kujiunga  na  bendi. Ili  kukabiliana  na  matatizo  haya   unatakiwa  uwe   mbunifu  na  kundi  dogo  la  wanamuziki  wabunifu ,  wanaojua  kuimba  na  kupiga  chombo  zaidi ya  kimoja.Waanzishe  mitindo  inayovutia  wateja. Wajiepushe  kuiga   muziki  wa  watu  wengine.Bendi  itangazwe , iwe   na  malengo  ya   kuwa  bendi   ya   Kimataifa.Ifanye  ziara  nje  ya  nchi  kwani  huko  nako  wangependa  kupata  vionjo  vya    muziki  tofauti  tofauti   na  wa   kwao.   Bendi  irekodi  nyimbo  nzuri   na   kuuza  kanda  za  kaseti ,  video , CD na  DVD. Bendi  iendeshe  matamasha, Pia   mmiliki  wa  Bendi  anatakiwa  kuwa   na   Ukumbi  wake   ambapo  ni   makao   makuu  ya   bendi     na    washabiki   wajue   hivyo.

No comments:

Post a Comment