BADILI FIKRA.FIKIRI TOFAUTI .BADILI MAISHA.JITAMBUE .JIFUNZE ELIMU YA SAIKOLOJIA,TEOLOJIA , FEDHA ,UTAMBUZI(SELF HELP EDUCATION),FALSAFA YA MAISHA,MAISHA NA MAFANIKIO,BIASHARA / UJASIRIAMALI.FURAHIA WASAA WAKO NA MAISHA NA MAFANIKIO BLOGU.THIS IS THE COMMUNITY CAPACITY BUILDING BLOG.ENJOY THE BLOG.STRETCH YOUR MIND. YOU CAN CHANGE YOUR LIFE FOR EVER. YOU CAN ACHIEVE EXCELLENCE.YOU CAN MAKE A DIFFERENCE.
Saturday, May 31, 2025
MAKALA : JE, WAJUA KUSUDI LAKO KUWAKO HAPA DUNIANI ?? NDANI YAKO KUNA MOTO WA NDOTO ZAKO UMEFICHWA------NA MWL JAPHET MASATU ------CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136
Rafiki Yangu Mpendwa,
Watu wengi wanamka kila siku…
Wanaoga, wanavaa, wanatoka.
Lakini hawajui kwa nini wanaishi.
Wanapambana… lakini hawajui wanapambana kwa lipi.
Wanaume wanahangaika na mihangaiko,
Wanawake wanahangaika na wanaume.
Kila mtu anakimbia, lakini hakuna anayeuliza:
"Tunakoenda ni wapi?"
Ishu Hii Ndio Inasababisha Maisha Ya Watu Yatupwe Kama Karatasi Iliyotumika.
Unajikuta una miaka 30... lakini unahisi hujaanza kuishi.
Unajiona hufai.
Unachoka bila kazi.
Una usingizi wa saa 10 lakini bado umechoka.
Unapoteza nguvu kwenye mambo yasiyojenga.
Unapata hela unazimaliza bila hata kumbukumbu.
Unapenda unakataliwa.
Unajifunza lakini bado maisha yako yapo vile vile.
Unapambana, lakini unapambana gizani.
Umefungwa kwa minyororo usiyoiona…
Na minyororo hiyo inaitwa: "Kutokujua KUSUDI la maisha yako."
Kujua Kisudi Ni Siri Ya Waliotoka Chini Wakafika Juu.
Wewe si maskini umepoteza mwelekeo tu.
Wewe si mvivu hujagundua unachopaswa kufanya.
Wewe si mshindwa hujajua sababu ya wewe kuwa hai.
Watu wakishajua walichozaliwa kufanya,
wanabadilika kama mwewe aliyefunguliwa.
Wanapaa.
Wanang’ara.
Wanatesa!
Ukweli Ni Huu: Maisha Hayaanzi Kwa Kupata Pesa Yanaanza Kwa Kujielewa.
Na huwezi kujielewa bila MWONGOZO.
Huwezi kufika bila RAMANI.
Huwezi kushinda bila KUJUA UNAPIGANIA NINI.
Ukweli mwingine ni huu:
Watu wengi wameishia kuishi maisha ya kuigiza.
Maisha ya watu wengine.
Wanavaa kama wengine.
Wanakimbia mafanikio ya wengine.
Wanajilinganisha.
Wanashindana.
Lakini ndani yao kuna MOTO UMEFICHWA.
Moto wa ndoto zao.
Moto wa kusudi lao.
Moto wa ukubwa wao halisi.
SULUHISHO?
Chukua MWONGOZO huu: “MWONGOZO WA MAISHA YA MAFANIKIO.”
KWA KUEDELEA KUSOMA VITABU Ndani yake utajifunza:
Jinsi ya kugundua kusudi lako.
Sheria 100 za maisha ya mafanikio.
Jinsi ya kuamka kila asubuhi ukiwa na maana
Jinsi ya kuishi maisha ya tofauti
Jinsi ya kuacha kuigiza na kuanza kuishi maisha yako halisi
Bado namkumbuka Huyu Kijana.
Kuna kijana mmoja alinitafuta.
Alichoka kuishi maisha ya ‘kawaida.’
Alikuwa na degree.
Alikuwa na kazi.
Lakini kila kitu kilionekana kimekosa ladha.
Akaanza kunywa.
Akaanza kuchelewa kazini.
Akaanza kujichukia.
Siku moja akaniambia:
“Bro, naishi kama si mimi.”
Nikampa mwongozo huu.
Akarudi baada ya wiki tatu na macho yenye mwanga.
Sasa ameanzisha kitu chake.
Anaamka kabla ya saa kumi.
Anapata pesa.
Anapendwa.
Anajipenda.
Maana sasa anajua KUSUDI lake.
Uko Tayari Kuamka?
Ama utaendelea kuishi kama ndoto ya mtu mwingine?
Usiishi kama kivuli jifunze kuangaza.
ENDELEA KUSOMA VITABU KILA SIKU ILI UENDELEE KUANGAZA NA KUISHI KUSUDI LAKO
Friday, May 30, 2025
MAKALA : MJASIRIAMARI MJANJA ANA TABIA GANI ???
Kakaa/Dadaa Yangu,
Unajua shida ya wengi?
Wengi wanaanza biashara kwa kishindo...
Lakini baada ya miezi mitatu,
BAM! Kimya kama kaburi la usiku.
Wanaanza kuuza nguo,
Wanaingiza mzigo wa milioni mbili,
Lakini hakuna anayenunua.
Wanashindwa kuelewa nini kinakwenda kombo.
Wanakata tamaa fasta.
Wanarejea kutegemea mshahara.
Wengine wanakata tamaa kabisa—wanakufa na ndoto zao.
Na hapa ndipo kuna maumivu makali.
Biashara si kupost tu bidhaa kwenye status.
Si kutegemea rafiki zako watanunua.
Wala si kushusha bei kila siku eti "promo."
Ukiwa huna akili ya mjasiriamali mjanja
utachezewa kama karata mitaani.
Ngoja nikufunze kitu.
Mjasiriamali mjanja ana akili ya pesa.
Anajua kutafuta wateja wake popote.
Anajua jinsi ya kuwashawishi bila kusumbua.
Anajua kutoa ofa ambayo haiwezi kukataliwa.
Anaelewa psychology ya mteja.
Na zaidi ya yote, anajua kuji-brand.
Na kama hujui hayo yote,
Usijidanganye eti “ni mapenzi ya Mungu.”
Ni mapenzi ya kukosa maarifa.
Sasa suluhisho liko hivi:
Ukiamua kuwa mjanja kwenye biashara
Lazima ujue kuuza hadithi.
Ndiyo, HADITHI!
Watu wananunua stori kabla ya bidhaa.
Wakiigusa hadithi yako,
Wanafika mwisho wa status tayari wamejishawishi.
Ukiuza sabuni,
Usiuze sabuni uza usafi wa mtoto wako.
Ukiuza viatu,
Usiuze kiatu uza heshima ya mguu wake kazini.
Mjasiriamali mjanja anauza HISIA si bidhaa tu.
Nikupe hadithi moja ya kweli.
Mrembo mmoja anaitwa Amina.
Alikuwa anauza mikoba Kariakoo.
Alihangaika sana, kila siku status 50, likes 2, wateja 0.
Alipojifunza kuuza kwa stori, mambo yalianza kubadilika.
Siku moja aliandika:
“Mwanamke mmoja alikuja dukani kwangu, akiwa amechoka, alinyamaza muda mrefu...
Aliponunua hii handbag,
Alisema, ‘Kwa mara ya kwanza najihisi mwanamke kamili.’
Niliogopa kusema chochote,
Ila moyo wangu ulichanua.
Na hapo ndipo nilijua,
Siuzi mikoba, nauza imani kwa mwanamke.”
Dakika 20 baadaye mikoba 7 iliuzwa.
MAKALA : MJASIRIAMALI MJANJA NA MBUNIFU NI NANI ??
Ni yule anayejifunza kila siku.
Anayefikiria tofauti.
Anayejua kutumia lugha ya wateja.
Anayeuza kwa hisia, si bei.
Wewe je?
Upo kwenye biashara kwa bahati,
Au umeamua kuwa MJASIRIAMALI MJANJA?
Kumbuka hii ya mwisho:
Wakati wengine wanauza bidhaa,
MJANJA ANAUZA STORI INAYOCHOMA MOYO.
MUHIMU; Kama bado hujasoma kitabu cha MJASIRIAMALI MJANJA,
Ukweli ni kwamba unajipunja,
Thursday, May 29, 2025
Tuesday, May 27, 2025
Thursday, May 22, 2025
MAKALA : MAISHA SI BAHATI NASIBU AU KUBET . NI RAMANNI YA MABADILIKO NA DIRA . NI MAAMUZI NA MAANDALIZI------NA MWL. JAPHET MASATU------TANZANIA -------FRIKA YA MASHARIKI--------CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136
Kakaa/Dadaa....
Unajua shida kubwa inayowakumba wengi?
Wanaamka kila siku…
Wanakimbizana kama mchwa waliomwagiwa maji…
Lakini hawajui wanakimbilia wapi.
Kila siku ni kujituma…
Lakini mwisho wa mwezi, mfuko ni kama shimo la panya.
Kila mwaka unakatika…
Lakini hakuna mabadiliko ya maana.
Wengi wako kwenye 'autopilot' ya maisha.
Wanajisukuma tu.
Wakiamini ipo siku mambo yatajileta.
Mambo hayajileti. Wewe ndo lazima uyasogeze.
Hii Inatisha Kidogo…
Unaamka ukiwa na nguvu.
Unaota mafanikio.
Lakini kila jioni, unarudi na uchovu tu.
No progress.
No peace of mind.
Unasema utabadilika kesho.
Kesho ikifika, unafanya yaleyale.
Ni kama umefungwa pingu zisizoonekana.
Hii ni hatari sana.
Inaua ndoto zako taratibu bila kelele.
Alafu unakuja kushangaa:
“Mbona maisha yananizunguka?”
Ni kwa sababu hakuna mwongozo.
Kuna Uongo Mmoja Mkubwa…
Eti “kuwa na bidii, utafanikiwa.”
Wongo huo.
Watu wengi wana bidii kuliko hata gari la kubeba mawe.
Lakini wako pale pale.
Tatizo si bidii.
Tatizo ni kutokuwa na DIRA.
Hakuna ramani.
Hakuna mwongozo.
Na kama hujui unakokwenda…
Hutajua hata ukifika.
Sasa Sikiliza Vizuri…
Maisha yako yanahitaji mfumo.
Mfumo wa kuweka malengo.
Kujijua wewe ni nani.
Unataka nini.
Na kwa nini unakitaka.
Halafu?
Anza kupanga hatua ndogo ndogo.
Kila siku.
Kidogo kidogo hadi kikamilike.
Na muhimu zaidi, tafuta maarifa ya kweli.
Si porojo.
Maarifa ya watu waliopitia moto.
Walioungua.
Wakaamka.
Wakasimama tena.
Ngoja Nikupe Kisa Cha Huyu Bwana Mdogo Hapa…
Kuna Bwana Mdogo mmoja mtaani kwetu Anaitwa Baba T.
Miaka mitano iliyopita alikuwa anauza vocha na peremende stendi.
Maskini alikua anavaa viatu vilivyochanika…
Watu walimcheka.
Lakini kuna siku moja aliniambia:
“Bro, nimeshaamua. Sitaki kufa maskini. Nataka mafanikio ya ukweli.”
Akanunua daftari.
Akaandika malengo yake.
Akasoma vitabu.
Akatafuta mentor.
Akaanza kuandika kila kitu anachotumia.
Leo hii?
Ana duka lake la simu.
Anauza online.
Anatoa ushauri kwa vijana wengine.
Na bado ni yule yule – Baba T ila mwenye mwongozo mpya wa maisha.
Na Wewe Unaweza Kubadilika Leo…
Ukiamua, unaweza.
Ukiwa na mwongozo sahihi, maisha yanabadilika.
Unapunguza makosa.
Unafupisha safari ya mateso.
Unapanda ngazi haraka.
Chukua hatua.
Andika malengo yako.
Soma kila siku.
Tafuta watu wanaojua kuliko wewe.
Achana na kelele za mtaani.
Focus.
Maisha ni yako.
Na hakuna atakayeyaishi kwa niaba yako.
Unataka mafanikio ya kweli?
Tafuta mwongozo.
Fuata mfumo.
Jitahidi bila kusahau mwelekeo.
Maisha si bahati.
Ni maamuzi na maandalizi.
ENDELEA KUSOMA HAPA UTAPATA RAMANI YA MABADILIKO NA DIRA YA MAISHA YAKO.
Sunday, May 18, 2025
MAKALA : NGUVU YA KUTENDA MIUJIZA NA NDOTO ZAKO UMEIBEBA WEWE MWENYEWE NA SI MTU MWINGINE--------NA MWL. JAPHET MASATU -------CALL / SMS / WHATSAPP + 266 716 924 136
Kakaa/Dadaa Yangu...
Umesahau wewe ni nani.
Umesahau kuwa ndani yako kuna nguvu ya kutikisa dunia.
Umejikatia tamaa kimya kimya.
Kila siku unasema *labda mimi sina bahati.*
Umeanza kuamini maisha ni magumu na huwezi kubadilisha chochote.
Lakini ukweli ni huu: UNA NGUVU YA MIUJIZA NDANI YAKO ,
Unaitumia vibaya.
Au hujui hata ipo.
Ulishawahi kumuona mtu aliyeanzisha biashara kwa buku 5 akafika juu?
Ulishawahi kumuona mtu aliyefeli shule lakini leo anaajiri waliopata division one?
Ulishawahi kumuona mtu aliyetelekezwa, akasota, lakini leo anajenga nyumba yake?
Wote hawa hawakuwa na miujiza ya mbinguni.
Walitumia nguvu ya ndani waliyoamka nayo kila siku.
Na hiyo nguvu wewe pia unayo.
Lakini... unaitumia kuskroll TikTok.
Unaitumia kulalamika.
Unaitumia kutafuta huruma badala ya suluhisho.
Una nguvu lakini hauna mwelekeo.
Miujiza sio kupasuliwa mbingu.
Sio malaika kushuka.
Miujiza ni pale mtu wa kawaida anapoamua kuamka na kuchukua hatua isiyo ya kawaida.
Ni pale mtu anapoamua kuamka kabla ya wengine.
Kuanza kuandika ndoto zake.
Kuanza kusoma vitabu badala ya magazeti ya udaku.
Kuanza kuomba kazi kwa bidii badala ya kuomba msaada.
Miujiza ni matokeo ya msimamo.
Suluhisho Lipo. Na Lipo Ndani Yako.
Badilisha namna unavyofikiri.
Acha kusema “sina mtaji” sema “naanza na hiki kidogo.”
Acha kusema “nimechelewa” sema “leo ndiyo siku yangu ya kwanza.”
Acha kujificha nyuma ya visingizio.
Toka uvunguni.
Toka kwenye comfort zone ya umaskini wa mawazo.
Chukua hatua.
Anza leo.
Fanya kitu.
Kwa sababu NGUVU YA MIUJIZA UMEIBEBEA WEWE MWENYEWE.
Bado namkumbuka....
Kuna bro mmoja alichoka na maisha.
Alikuwa hana kazi. Hana mtaji. Hana cheti.
Alikaa chini akaandika: “Mwaka huu lazima niwe mtu mwingine.”
Akaanza kuuza karanga mtaani.
Akaweka akiba ya mia mia.
Alikuwa anasoma vitabu alivyokopeshwa.
Alifungua YouTube kujifunza marketing.
Miaka mitatu baadaye...
Ana biashara ya kuuza nafaka.
Ana familia.
Ana ndoto mpya kila mwaka.
Aliniambia hivi:
“Miujiza haikunitokea, niliitengeneza mwenyewe.”
Sasa Wewe Una Sababu Gani Ya Kukata Tamaa?
Huna sababu.
Una kila sababu ya kusimama.
Chukua kalamu na kuandika ndoto zako.
Zima data saa tatu usiku na kupanga kesho yako.
Na anza kutenda miujiza ya kweli kupitia nguvu yako ya ndani.
Kumbuka: Miujiza Haiporomoki.
Miujiza hutengenezwa.
Na hutengenezwa na watu kama wewe.
Watu wa kawaida lakini walioamua kuishi maisha ya ajabu.
ENDELEA KUTEMBELEA BLOG HII UTAJIFUNZA MENGI " MAISHA NA MAFANIKIO ( LIFE & YOU ) BLOG " PENDA KUNUNUA VITABU NA KUVISOMA UTAGUNDUA SIRI NYINGI ZA DUNIA HII.
Friday, May 16, 2025
MAKALA : SHERIA 100 ZA MAISHA NA MAFANIKIO -----NA MWL JAPHET MASATU ---- CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136
Kakaa/Dadaa Yangu...
Watu wengi wanakufa maskini si kwa sababu walizaliwa maskini…
Wanabaki maskini kwa sababu wanaishi bila sheria.
Wanapiga hatua moja mbele… halafu wanarudi tatu nyuma.
Siku zinaenda, miaka inasonga… maisha yanabaki pale pale.
Unaamka, unaenda kazini… lakini huna cha maana unaweka mezani.
Kila ukijaribu kusonga, kuna kitu kinakuvuta nyuma.
Unajua ni nini?
Huna ramani.
Huna sheria.
Huna mwelekeo.
Na Hapo Ndio Unatupwa Katika Kundi la “Wanaojitahidi Tu”
Unahangaika sana, lakini hakuna matokeo.
Unasoma vitabu, unaenda semina… lakini maisha yako hayabadiliki.
Una marafiki wanafanikiwa, lakini wewe bado unahaha.
Una ndoto, lakini hazina miguu.
Una malengo, lakini hayatimizwi.
Una nia nzuri, lakini hakuna mbinu.
Inachosha.
Inaumiza.
Inavunja moyo.
Unaweza ukajiona kama vile maisha yamekuchoka.
Kila kitu kinagoma.
Kila mtu anakupita.
Wewe unabaki unaangalia… ukiwa na maswali kuliko majibu.
Na Tatizo Halipo Kwenye Bahati… Lipo Kwenye Mfumo Wako
Wengi wanangoja bahati.
Wanasema: “Siku moja nitapanda juu.”
Hiyo siku haiji.
Kwa sababu hawafuati sheria.
Sheria za maisha.
Sheria za mafanikio.
Hakuna mafanikio bila sheria.
Kama vile gari halisafiri bila barabara.
Kama vile mti hauoti bila mizizi.
Maisha yanahitaji misingi.
Na misingi hiyo ni sheria.
Na sio sheria ngumu.
Ni zile rahisi.
Zenye mantiki.
Zenye mpangilio.
Lakini wengi hawajui.
Wengine wamewahi kusikia, lakini hawafuati.
Na ndio maana maisha yao ni kama gari lililoharibika breki, linaenda tu... bila mwelekeo.
Sasa Hii Ndio Dawa – Sheria 100 Za Maisha Ya Mafanikio
Nimekuandalia sheria hizi kwa jasho na damu.
Zimetoka kwa tajiri aliyewahi kulala kwenye dari la mabati.
Zimetoka kwa kijana aliyekua anauza vocha, leo ana kampuni.
Zimetoka kwa mwanamke aliyetelekezwa, leo ana biashara tano.
Sheria hizi ni silaha.
Zikupatie mwelekeo.
Zikupatie nguvu ya kupambana.
Zikusaidie kuachana na maisha ya mdundo mmoja.
Ukitaka kubadilisha maisha yako…
Ukitaka kuamka kutoka usingizini...
Sheria hizi ni Biblia / Juzuu yako mpya.
Sikiliza Story ya Kelvin Kijana Aliyeamua Kubadilika
Kelvin alikua anaishi Tandale, kwa mama wa kambo.
Alikua anafukuzwa shule kila siku —si kwa sababu ni mjinga, bali hakuwa na sare.
Alikua anaota kuwa mtu mkubwa, lakini mtaa ulimcheka.
Siku moja akapewa kitabu kidogo tu kilikua na "Sheria 100 Za Maisha Ya Mafanikio"
Akakisoma.
Akaanza kubadili tabia.
Akaanza kuamka mapema.
Akaanza kujifunza kila siku.
Akaacha kulalamika.
Leo Kelvin ni mkurugenzi wa kampuni inayouza bidhaa mitandaoni.
Analipa kodi.
Anasaidia mama yake.
Anafundisha vijana wenzie.
Na yeye anasema hivi:
"Maisha yanabadilika pale unapofuata sheria za maisha, si pale unapongoja msaada."
Sasa Ni Zamu Yako
Sheria 100 hizi si hadithi za kuburudisha.
Ni mashine ya kukutoa kwenye maisha ya hovyo hovyo.
Ni mwelekeo mpya wa mafanikio.
Ukiamua kuzifuata, hakuna kitakachokuzuia.
Ukiamua kuzipuuza, usilalamike maisha yanapokuchezea.
ENDELEA KUPERUZI NA KUSOMA BLOG HII " MAISHA NA MAFANIKIO ( AND LIFE ) BLOG "
ILI UJIFUNZE SHERIA/ KANUNNI ZA KUFANIKIWA KATIKA MAISHA YAKO.
Thursday, May 15, 2025
MAKALA : USILAUMU WAZAZI , SI KOSA LAKO HATUKUFUNDISHWA KUHUSU ELIMU YA MSINGI YA BIASHARA NA MAUZO---JIFUNZE UINUKE---BIASHARA NI AKILI NA MAARIFA------------CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136
*Siyo Kosa Lako, Hujafundishwa TU!*
Kakaa/Dadaa..
Unajua kuna watu wanawacheka wajasiriamali wadogo?
Huku wakiwasema vibaya:...
*Mbona kila biashara unayoanzisha haifiki miezi mitatu?*
*Unapenda kulalamika sana!”
*Wewe huwezi fanikiwa kamwe!*
Na huwa naumia nikisikia haya maneno.
Kwa sababu…
Watu hawajui mateso yanayomfanya mtu aamue kuuza maandazi saa 12 asubuhi bila hata chai.
Hawajui…
Maumivu ya kutafuta mtaji wa elfu 20 kwa kuazima mia mia.
Kunyanyaswa na maneno ya jamaa zako:
“Kama ni biashara ya maandazi si kila mtu anafanya?”
Kukesha ukitengeneza sabuni halafu asubuhi mvua inanyesha, hakuna mtu hata mmoja kununua.
Sasa leo nakuambia ukweli:
Siyo Kosa LAKO.
Haujafundishwa TU!..
Tatizo Si Wewe, Ni Mfumo Wetu.
Shule zetu hazikufundisha namna ya kuuza.
Hazikufundisha namna ya kujua faida.
Hazikufundisha namna ya kumshawishi mteja.
Tulifundishwa 1+1=2.
Lakini hatukufundishwa jinsi ya kutengeneza buku kwa kuuza karanga.
Ukatoka shule ukiwa na degree.
Au ukiwa form four.
Au hata bila cheti.
Lakini wote mko sokoni mnaanza biashara kama vipofu wanaovuka barabara.
Na Ndio Maana…
Unajikuta unafungua duka la vocha,
Unaanza kuuza na sabuni tano, pipi za mchina, na airtime ya mia.
Mwishoni mwa mwezi…
Umeuza elfu 50.
Umebakiwa na 10.
Na hata hujui imepotelea wapi.
Wewe si mzembe.
Wewe si mjinga.
Wewe ni mtu jasiri lakini hujapewa silaha.
Sasa Sikiliza Hii:
Kabla hujaanza biashara yoyote…
Unahitaji kujua vitu vitano tu vya msingi:
1. Shida ya watu ni ipi?
Watu hawataki bidhaa, wanataka suluhisho.
2. Unawauzia kina nani?
Hakuna biashara ya “kila mtu”
3. Unawafikiaje?
Kama hawaitwi hawaji. Kama hawajui hawanunui.
4. Bei yako inasemaje?
Bei nzuri haimaanishi rahisi inamaanisha INAOANA na thamani.
5. Faida yako iko wapi?
Si pesa inayoingia, ni pesa inayobaki baada ya gharama.
Stori Ya Kweli Ya Dada Zawadi Wa Gongo La Mboto....
Zawadi alikuwa anafua nguo kwa watu.
Kila siku jua likitoka, anajitwika ndoo, anazunguka mtaani akitafuta wateja wa kuwafulia hadi jioni.
Analipwa elfu mbili elfu tatu.
Anaondoka na macho mekundu, mikono iliyochubuka,
Lakini hana hela hata ya sabuni.
Siku moja alihudhuria semina ya biashara.
Akaambiwa kitu kimoja tu:
*Fungua huduma yako. Uisajili. Toa package. Weka namba zako mitandaoni.*
Leo Zawadi haendi nyumba hadi nyumba.
Anapokea simu.
Wateja wanamfuata.
Anatoza elfu kumi hadi elfu ishirini kwa huduma ya kitaalamu.
Na bado anafua nguo.
Lakini kwa akili.
Tunaambiwa tukomae. Lakini hatuambiwi namna.
Tunaambiwa tufanye kazi kwa bidii. Lakini bidii bila maarifa ni kama kukata mti kwa kijiko.
SULUHISHO?
Sihitaji nikuambie uache biashara.
La hasha.
Nakuheshimu.
Ninachokuambia ni hivii…:
Chukua hatua ya kutafuta elimu ya msingi ya biashara.
Elimu inayoeleweka.
Elimu ya mtaani.
Elimu ya kweli.
Kabla hujapoteza muda tena,
Kabla hujakataliwa tena,
Kabla hujachoka kujaribu jifunze.
Kwa Nini?
Kwa sababu:
Huwezi kufanikiwa kwa kukurupuka.
Na
Siyo kosa lako kuwa hujui.
Lakini litakuwa kosa lako ukikataa kujua.
Kama makala hii imekuongelea wewe, huna haja ya kujionea aibu.
Kila shujaa alianza akiwa hajui.
Lakini waliamua KUJIFUNZA.
Nataka nikupe silaha mbili za siri.
Ni silaha za kumtokomeza ujinga,
Silaha hizo ni Elimu Ya Msingi Ya Biashara na CHUO CHA MAUZO, Kwa Mtu Wa Mtaa.
#SioKosaLako
#JifunzeUinuke
#BiasharaNiAkiliNaMaarifa
Tuesday, May 13, 2025
KITABU 338 : JIFUNZE BIBLIA TAKATIFU --( 08)----AGANO JIPYA --( 08 )---YESU---NAMNA INJILI ZILIVYOTUNGWA , INJILI ILIVYOANDIKWA NA MATHAYO , MARKO , LUKA , YOHANE , INJILI ZA SINOPTIKI , HABARI ZA UTOTO WA YESU , NDUGU ZA YESU ,NYARAKA KWA WATU WOTE NA UFUNUO , ZABURI , ---FULL NUKUU---NA PADRE J. BOUQUET DEUS CHAUX . M. Afr.----TANZANIA----( PDF )---CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136
Monday, May 12, 2025
KITABU 340 : 101 WAYS TO MAKE MONEY IN AFRICA---FULL BOOK---LUCRATIVE BUSINESS IDEAS , INSPIRING SUCCESS STORIES , AND INTERESTING BUSINESS OPPORTUNITIES FOR FORWARD THINKING ENTREPRENEURS----BY JOHN AUL LWUOHA & HARNET BOKREZION PHD-----FIRST EDITION , NOVEMBER , 2014-----CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136
MAKALA : UMASKINI UNAUTAKA WEWE MWENYEWE , USILALAMIKIE WATU , NDUGU WALA SERIKALI ? ANZA NA BUKU ( TSHS 1000 ) KUWEKA AKIBA .----------CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136
Kaka, dada, hebu tuambiane ukweli…
Umechoka kuishi kwa mlo mmoja?
Au kila mwisho wa mwezi ni stress tupu?
Mishahara inapita kama upepo.
Biashara haieleweki.
Kuna hela, lakini haikai.
Unafanya kazi kama punda, lakini mfuko ni kama gunia la mbolea mashimo kila kona.
Unajituma, lakini mafanikio yako kama ndoto ya mchana.
Kaka, hiyo siyo laana.
Ni mfumo mbovu wa maisha.
Ni kukosa maarifa sahihi.
Tazama wenzako wanaoanza na elfu moja,
Leo wanamiliki vibanda, magari, hadi mashamba.
Wewe bado unatafuta mtu wa kukukopesha buku la kula.
Ni aibu.
Lakini sio kosa lako kabisa.
Ni kwamba wakati unakuwa uliaminishwa kuwa*Ukiwa na hela nyingi, ndo unaweza kuwekeza.*
Na Wewe Ukaamini.
Ulimwengu unabadilika, lakini mtazamo wako umebaki kuwa ule wa miaka ya 70.
Upo kwenye mduara wa mateso pesa inaingia na kutoka bila faida.
Kila mwezi ni kama kuanza maisha upya.
Mpaka lini?
Watu wengi hudhani kwamba ili uanze kujenga utajiri, lazima uwe na mamilioni.
Hapo ndo tunakosea.
Ukweli ni huu:
Hela kidogo ndiyo mwanzo wa hela nyingi.
Tatizo si kwamba huna pesa.
Tatizo ni kwamba hujui namna ya kukitumia kile kidogo ulichonacho.
Huna mfumo.
Huna maarifa.
Unakula mtaji, unaua ndoto zako.
Usingoje mshahara mwingine ukufikishe kwenye msongo tena.
Usingoje upate milioni ndo uanze.
Anza na hiyo buku YAANI TSHS 1000
Buku yako ya leo inaweza kuwa sababu ya uhuru wako wa kesho.
ENDELEA KUSOMA KILA SIKU " MAISHA NA MAFANIKIO BLOG " UTAJIFUNZA MENGI NA SIRI NYINGI ZA MAISHA NA MENGINEYO DUNIANI --- ONGEA NA KOCHA MWL. JAPHET MASATU-----CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136