Tuesday, September 13, 2016

LIGI YA MABINGWA ULAYA KUANZA KUTIMUA VUMBI LEO



ligi ya mabingwa ulaya kuanza kutimua vumbi leo

13  septemba  2106


Image copyright Google Image caption Nembo ya ligi ya mabingwa ulaya 

Michuano ya ligi ya mabingwa barani ulaya inaanza kutimua vumbi leo kwa jumla ya viwanja vinane kuwaka moto.

Katika kundi A miamba wa soka la Ufaransa, Paris St Germaine watakua nyumbani kuwaalika Arsenal toka England, huku Basel wakichuana na Ludo Razgrad. 

Michezo ya kundi B Wareno wa Benfica watashuka katika dimba lao la Estádio da Luz kuwakabili Besiktas toka uturuki, Dynamo Kiev nao watapambana na Napoli.

Fc Barcelona watashuka dimbani Camp Nou kukipiga na Celtic,matajiri wa Manchester City wataanza kusaka heshima kwenye michuano hiyo kwa kucheza Wajerumani wa Borussia Monchengladbach.

Michezo ya kundi D Bayern Munich watakua nyumbani kucheza na Fc Rostov huku Waholanzi wa PSV Eindhoven wakicheza na Atletico Madrid.

BBC  SWAHILI

No comments:

Post a Comment