Friday, December 25, 2015

JE , WAJUA UNAELEKEA WAPI NDUGU YANGU ?



Katika   tembea  tembea  yangu     huku   uswahilini   kwetu   MWANANYAMALA B  KWA  MAMA  ZAKARIA , KATA  YA  MAKUMBUSHO , jijini  DAR  ES  SALAAM  , TANZANIA  niliwaona  WANAUME    kadhaa    wakifanya   KAZI     katika  kitu  kilichoonekana  kuwa   ni  Msingi  wa  nyumba   kubwa   ambapo   WANAUME   hawa    walikuwa   wakifanya  kazi  ya    KUPANGA  MATOFALI .
     Nilijaribu     kumwuliza mmoja   wa  WANAUME  hao : “  UNAFANYA   NINI ?”  Alijibu :    KWANI    HUONI ?   NAPANGA   MATOFALI .   Niliuliza    swali  hilo   hilo   kwa   MWANAUME  mwingine   :  “ MIMI  ?  AHAA , NAFANYA  KAZI   HAPA  KUJITAFUTIA  RIZIKI.”
  Mtu   wa  tatu   naye   alinijibu :  “ KWA  NINI , BWANA , NASAIDIA   KUJENGA   OFISI  NZURI   KATIKA  JIJI   LETU.”  Yupi   kati   ya   wanume   hawa   unadhani   anaelekea   kuwa   na   maisha   ya   hali   ya  juu ?
    Kabla   hujayafanya  maisha    yako   kuwa   ya  MALENGO   na   FURAHA , lazima  ujue   JAMBO   fulani   kuhusu   wewe   mwenyewe , kwamba   KWA  NINI  UWE   NA  UFANYE   KAMA   UNAVYOFANYA.  Ni  kitu   gani  hasa   kinachokufanya  uwe   tofauti   na  wakati  mwingine  MCHOYO , pengine   kuwa   mtu   mzuri  na   anayekubalika ?  ILI   MRADI  TU  , KWA  NINI  UWE   ULIVYO ?
    MWANASAIKOLOJIA  mmoja   maarufu  amekadiria   kwamba  ni  asilimia   ndogo  sana  ya  watu   ulimwenguni   wana  MALENGO  yao , Waliosalia   WANABURUZWA TU !  kama    ALICE   akiwa   nchi  ya  ajabu .
     NIFUATE    BARABARA  IPI ?    ALICE  alimwuliza   PAKA  CHESHIRE.
  “ INATEGEMEANA  NA  UNAKOKWENDA ,  PAKA  alijibu.
  “ LAKINI , “ALICE  ALISEMA , “ SIJUI   NINAKOTAKA  KWENDA.”
Ndipo   PAKA  akasema:    HAKUNA  TATIZO  KWA  NJIA  YOYOTE  UTAKAYOFUATA.”
ANGALIZO:  Ni  jambo  muhimu sana  kuwa    kila  mmoja   asitofautiane   na  njia  ya   MAISHA    anayofuata. Kusita   kutoa  uamuzi ,  kukosa  FURAHA    na  KUTORIDHIKA  ulimwenguni , kwa  kiasi  kikubwa   husababishwa   na  kukosa  MALENGO.
  Unataka  MAFANIKIO , kila  mmoja   anataka   MAFANIKIO. Kila  mtu   huelewa   MAFANIKIO  kama   kitu  ambacho  ni  tofauti  kwa  wengine   ina   maana    KUPATA  FEDHA  NYINGI  SANA. KWA   MIMI  ina   maana   MJI  wenye   MKE  aliyeridhika  na  MTOTO   mwenye   FURAHA ,  pamoja  na  FEDHA  ZA  KUTOSHA   zinazoweza   KUNIPATIA   MAHITAJI  MUHIMU.
    Umekwishapiga  PICHA   kichwani  mwako   kuhusu   maana   ya   MAFANIKIO  kwako.  MAFANIKIO    katika   MAISHA  hutokea   tu  baada  ya    kuweka   MALENGO   katika   MAISHA  ambayo   unayajenga. Wakati   umejiwekea    MWELEKEO   wako ,  MAISHA  YANA   MAANA. HUCHUKUA  UMUHIMU  MPYA. Hujisikii  tu  kuwa  MAISHA  ni  majaribio  yasiyo  na    maana  na  vikwazo  vyenye   kiasi  kidogo  cha  FURAHA  kilichotupwa  kwako    kukuzuia  KUJINYONGA.
   WANASAYANSI   wametangaza  kuwa  mwili  wa  binadamu   una   mabilioni  ya  chembecheme  ambazo  zinaishi   katika  mambo   matatu:--

    (a).  Kemikali  iliyo  katika   Chakula    unachokula.
    (b).Homoni  zilizopo  katika   mfereji  wa  damu.
    {c).  Ujumbe  wa   fahamu   unaotuma  wewe   mwenyewe.

SIRI   YA  MAFANIKIO  IPO  HAPA NDUGUN YANGU : Unapotuma  ujumbe  wako  kupitia  kituo  cha   kurushia   MATANGAZO---UBONGO  --  ndipo   unapohuishwa , unatiwa   NGUVU. Kama  wewe  ni  mtu    unayependa  kusema :     SIWEZI , SIWEZI , “  ndipo  WAZO  hilo   linasafirishwa    kwenye   chembechembe  katika  mwili  wako   na    zinaambizana  kuwa :     HATUWEZI , BOSI  AMESEMA   HATUWEZI , HIVYO   HATUWEZI . TUPO  CHINI  YA   MAMLAKA  YAKE .” 
  Kama  una  mtazamo   mbaya  kuhusu  MAISHA ,  chembechembe  zako  nazo   huwa   na    mwelekeo  huo. Mara   unapofikiria  vinginevyo , unashangaa  kwa  nini  NGUVU  zako   zimeongezeka  ghafla.

    WANASAYANSI     wamefanya   UTAFITI   wa   kutosha  kuhusu   jinsi   mwanadamu  alivyo  na  jinsi   alivyoumbwa .  Matokeo  ya  ucunguzi   wao   kuhusu  sababu    za   TABIA  YA  MWANADAMU   yanafurahisha  sana.
  UGUNDUZI   wao  ni  kuwa   NGUVU  ambayo    huzunguka   katika   mawimbi   yaendayo  kasi ,  hutokea  mwilini. MAISHA  yote   ni  NGUVU   na   unaweza    kuilekeza    NGUVU  kwenye     mwili   wako  kama  unavyopenda.  Ni  juu  yako   kuyafanya  MAISHA   yawe   kama  unvyopenda  kwa  sababu  WEWE  NDIYE  MWAMUZI   WA  MWISHO   NA  DEREVA  WA  ROHO  YAKO.


  Makala  hii  imeandikwa  na  MWL.  JAPHET   MASATU,  anapatikana  kwa   Call /WhatsApp + 255 716 924136 /  + 255 755 400  128,  EMAIL:  japhetmasatu@yahoo.co.m.  Ni   mwanafunzi  wa  CHUO  KIKUU  HURIA , TANZANIA, KINONDONI , DAR  ES  SALAAM ,2015.
 

 



No comments:

Post a Comment