wateja. Kwenye biashara kuna aina mbili za wateja, ambao ni wateja wa zamani na wateja wapya.
Kwa jinsi hali ilivyo huku mitaani kwetu, ni kwamba wafanyabiashara wengi wanajali zaidi wateja mpya.
Mteja
mpya anaonyeshwa kila aina ya upendo kiasi cha kumkatishatamaa mteja wa
zamani endapo ikitokea wote wawili wakawepo pamoja eneo la biashara.
Hali
hii ya kutengwa kama mteja wa zamani imenitokea mara nyingi na
kunifanya niamini kwamba kadiri unavyozidi kununua bidhaa mara nyingi
kutoka kwa mfanyabiashara fulani ndivyo anavyoacha kukujali.
Kiashiria
mojawapo ni wakati mwingine mteja wa zamani anapouziwa vitu kwa bei
tofauti na Yule mteja mpya. Yaani ni ajabu wateja wapya wanapunguziwa
wakati wale wa zamani wanaonunua vitu mara kwa mara wanapandishiwa bei.
Wakati
mwingine baadhi ya wafanyabiashara wanakupunja wewe mteja wao wa zamani
kupitia vipimo hasa kwa bidhaa kama sukari, nyama, mchele n.k.
Ukweli
ni kwamba, mteja wa zamani ni LULU. Unapashwa kumtengenezea mazingira
rafiki kwa kuhakikisha unampatia unafuu kadiri mtakavyozidi kukaa pamoja
kibiashara. Ikiwa utazidi kumjali na yeye atazidi kuwa na sababu ya
kuendelea kuwa mteja wako daima.
Kwanini mteja wa zamani?
Ukizidi
kuwajali wateja wa zamani inakusaidia wewe kupata wateja wapya kwa
gharama kidogo sana; kuliko ambavyo ungewatafuta wewe mwenyewe moja kwa
moja.
Mteja
wa zamani ni mtaji mkubwa” endapo utakaanaye vizuri, na hii nikutokana
na ukweli kwamba, anaouwezo wa kukuletea wateja wapya kila mara.
Mteja wa zamani ni rahisi kumtunza kuliko kupata mteja mpya.
Sisi
wataalamu wa masuala ya masoko tunasema kuwa gharama za kumpata mteja
mpya ni mara saba zaidi ya gharama za kukaa na mteja wako wa zamani.
Mteja
wa zamani tayari anakufahamu kwahiyo, akiambiwa juu ya mali mpya hana
mud sana wa kuhoji kwasababu tayari anakuamini na hivyo ataweza kuitikia
haraka.
Uzoefu wangu unaonyesha kuwa inachukua muda na nguvu nyingi kumshawishi mteja mpya kukubali bidhaa yako kuliko wa mteja zamani.
Tayari
wewe unafahamu vizuri tabia na mahitaji ya wateja wako wa zamani,
kwahiyo inakuwa rahisi kujua namna nzuri ya kutengeneza mkakati wa
kuongeza mauzo yako bila kusahau kuwapa kilicho bora.
Nifanye nini kukuza uhusiano na wateja wangu wa zamani?
Unachotakiwa
kufanya ni kujifunza jinsi ya kujenga na kuimalisha mahusiano na watu
hasa wale wanaokuja kununua bidhaa na huduma mbalimbali kutoka kwako.
Ni
muhimu sana kujenga mahusiano ya karibu na kila mteja mpya wakiwemo
wale walioletwa na mteja wako wa zamani, lakini jenga uhusiano na kila
mmoja peke yake siyo kama kikundi.
Katika mchakato wa kujenga uhusiano na wateja fanya yafuatayo;
Badili tabia yako juu ya mahusiano: Tabia
yako ya mahusiano na watu wengine ni muhimu sana. Usidhani suala zima
la kujali watu litatokea tu siku moja, lazima uzame ndani kwenye tabia
yako kwanza.
Andaa orodha ya majina na namba za simu:
Jiwekee utaratibu wa kuwa na orodha ya majina pamoja na namba zao za
simu. Ukiwa na orodha ya majina ni rahisi kuwa na kumbukumbu ya nani
kanunua nini na kiasi gani mwaka mwezi au mwaka huu.
Inapofika
sikukuu maalum kama Krismas hawa ndio wa kuwapa kipaumbele unapotuma
salam za pongezi. Sijui wewe kama uliwahi kumtumia mtu heri ya krismas
kwasababu tu ni mteja wako mzuri..kama hujafanya hivyo basi jitafakari
na uchukue hatua.
Toa elimu juu ya bidhaa/huduma: Hakikisha
wateja wako wanapata elimu bora juu ya matumizi sahihi ya bidhaa zako,
ili waweze siyo tu kununua bali kueneza habari njema kwa wateja wengine.
Kadiri utakavyozidi kuwaelimisha ndivyo utakavyozidi kuzalisha wateja
wengi ambao ni waaminifu.
Shirikiana nao shughuli za kijamii:
Jaribu kuwa nao karibu kwenye shughuli za kijamii; kama ni kuchangia
harusi fanya hivyo, hawa ndio unatakiwa kuwachangia, kama ni misiba hawa
unalazimika kuwatembelea na kuwafariji.
Kwahiyo, kupitia mahusiano yako na wateja, unajikuta umejenga kundi kubwa la marafiki na ndugu mlioshibana.
Bahati mbaya sana wengi tunashiriki zaidi shughuli za kijamii kwa watu ambao hawana uhusiano wowote na biashara zetu.
Unahitaji
kuwaongeza kwenye orodha wateja wako, ili linapofika suala zima la
kushirikiana katika shughuli za kijamii, nao wawe ni sehemu ya watu
unaowakumbuka.
Toa tuzo kwa wateja:
Kama unachukua kumbukumbu za wateja vizuri ni rahisi kwako kuona nani
amechukua pesa zake kwa wingi kwa katika kipindi cha mwezi, robo, nusu
mwaka au mwaka mzima.
Hapa
utakuwa na nafasi ya kujua ni nani umpe tuzo. Tuzo hiyo siyo lazima
uwambie, unaweza ukatafuta utaratibu wa kumpongeza au kumpa tuzo.
Mafano;
kutoa mwaliko wa chakula cha jioni au kinywaji nyumbani au hoterini;
unaweza kutuma salam za pongezi mfano kupata mtoto, kumaliza shule kwa
watoto n.k.
Wewe
uliye na biashara yoyote tambua kuwa unahitaji kuendelea kujifunza
mpaka ufike sehemu uone kwamba wateja ndio ndugu namba moja.
KWA KUJIFUNZA KWA MAPANA NA MAREFU JIUNGE NA " DARASA ONLINE " KWA KUWA MWANACHAMA.
Tuwasiliane kwa WhatsApp + 255 716924136 / + 255 755 400128 + 255 688 361 539
Ndimi RAFIKI NA KOCHA MWL. JAPHET MASATU ,
DAR ES SALAAM , TANZANIA.
CHUMA ULETE YA CHUNGU
ReplyDeleteKwanza CHUMA ulete Ni nini?
Ni dawa ambayo utengenezwa kwa mkusanyiko wa utaratibu Fulani unaofanyika kwa pamoja kwa mlengo wa uvutaji au uvunaji wa fedha kutoka sehemu tofauti au mbalimbali.
(Kwa uhitaji wa NDAGU AU JIHNI WA MALI AU FEDHA NA KINGA YA MWILI NA MALI KWA UJUMLA NIPIGIE SIMU MOJA KWA MOJA DOKTA MDIRO +255 742162843 KWA MAELEKEZO HATA KAMA UKIWA MBALI MALIPO NI BAADA YA MAFANIKIO).
CHUMA ulete katika utengenezwaji hutumika jini anayeitwa GHUUL ambae uleta au uvuta fedha kimazingala kutoka sehemu mbalimbali kwa utaratibu maalumu. CHUMA ulete zipo Aina nyingi Ila leo nitazungumzia CHUMA ulete mdogo ya CHUNGU.
Chuma uleteee ndogo ya chungu ambayoo inaluka na kwenda kukusanya pesa sehemu mbali mbali inavuta pesa ndanii .
Hii chakula chake ni udi tuu na unaweza kunuwiza ukachagua ukaomba ikuletee pesa za aina gani wewe utachaguwa kama unavyoona hapo kwenye picha hii ni chuma uleteee ndogo mtu yeyotee anaweza kutengenezewa hata kama huna biashala pia hata Kama upo mbali kikubwa tu uwe na uwezo wa kutunza sili. Vile vileee hii inadumu miaka 5 itakubidii uludi kuja kutengeneza upya kafara ya damu ya kuku mwekunduu inatakiwa kila baada ya miezi 3.
Tafuta chungu kama icho kwenye picha fanya duwa maalumu ambayo nitakupatia na tafuta udi Aina ya sain frola, metrofrolla au metromillan na kitambaa cheupe pia chumba kisafi kwa ajili ya ibada hiyo.
Kumbuka hii ni chuma uleteee ndogo ya chungu hutakiwi kutoaa sili ya jini huyu na ufalume wa jini huyu maana utavunja miiko na maagano ya Jambo Hilo.
Angalizo Piga simu kuepuka MATAPELI pia kwa maelekezo zaidi husifanye jambo hili bila maelekezo KAMILI.
DOKTA MDIRO
Call/whatsup +255 742162843