Thursday, May 22, 2025

KITABU 342 : KITABU CHA HADITHI ----HAIBA NA MBILIKIMO SABA-----IMETOHOLEWA KUTOKA NGANO YA ULAYA NA PILLI DUMEA----1997----( SNOW WHITE AND THE SEVEN DWARFS BY BROTHERS GRIMM )----( PDF )-----KWA WATOTO WA TANZANIA----CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136

MAKALA : MAISHA SI BAHATI NASIBU AU KUBET . NI RAMANNI YA MABADILIKO NA DIRA . NI MAAMUZI NA MAANDALIZI------NA MWL. JAPHET MASATU------TANZANIA -------FRIKA YA MASHARIKI--------CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136

 Kakaa/Dadaa....

‎Unajua shida kubwa inayowakumba wengi?

Wanaamka kila siku…

‎Wanakimbizana kama mchwa waliomwagiwa maji…

‎Lakini hawajui wanakimbilia wapi.

‎Kila siku ni kujituma…

‎Lakini mwisho wa mwezi, mfuko ni kama shimo la panya.

‎Kila mwaka unakatika…

‎Lakini hakuna mabadiliko ya maana.

‎Wengi wako kwenye 'autopilot' ya maisha.

‎Wanajisukuma tu.

‎Wakiamini ipo siku mambo yatajileta.

‎Mambo hayajileti. Wewe ndo lazima uyasogeze.

‎Hii Inatisha Kidogo…

‎Unaamka ukiwa na nguvu.

‎Unaota mafanikio.

‎Lakini kila jioni, unarudi na uchovu tu.

‎No progress.

‎No peace of mind.

‎Unasema utabadilika kesho.

‎Kesho ikifika, unafanya yaleyale.

‎Ni kama umefungwa pingu zisizoonekana.

‎Hii ni hatari sana.

‎Inaua ndoto zako taratibu bila kelele.

‎Alafu unakuja kushangaa:

‎“Mbona maisha yananizunguka?”

‎Ni kwa sababu hakuna mwongozo.

‎Kuna Uongo Mmoja Mkubwa…

‎Eti “kuwa na bidii, utafanikiwa.”

‎Wongo huo.

‎Watu wengi wana bidii kuliko hata gari la kubeba mawe.

‎Lakini wako pale pale.

‎Tatizo si bidii.

‎Tatizo ni kutokuwa na DIRA.

‎Hakuna ramani.

‎Hakuna mwongozo.

‎Na kama hujui unakokwenda…

‎Hutajua hata ukifika.

Sasa Sikiliza Vizuri…

‎Maisha yako yanahitaji mfumo.

‎Mfumo wa kuweka malengo.

‎Kujijua wewe ni nani.

‎Unataka nini.

‎Na kwa nini unakitaka.

‎Halafu?

‎Anza kupanga hatua ndogo ndogo.

‎Kila siku.

‎Kidogo kidogo hadi kikamilike.

‎Na muhimu zaidi, tafuta maarifa ya kweli.

‎Si porojo.

‎Maarifa ya watu waliopitia moto.

‎Walioungua.

‎Wakaamka.

‎Wakasimama tena.

‎Ngoja Nikupe Kisa Cha Huyu Bwana Mdogo Hapa…

‎Kuna Bwana Mdogo mmoja mtaani kwetu Anaitwa Baba T.

‎‎Miaka mitano iliyopita alikuwa anauza vocha na peremende stendi.

‎Maskini alikua anavaa viatu vilivyochanika…

‎Watu walimcheka.

‎Lakini kuna siku moja aliniambia:

‎“Bro, nimeshaamua. Sitaki kufa maskini. Nataka mafanikio ya ukweli.”

‎Akanunua daftari.

‎Akaandika malengo yake.

‎Akasoma vitabu.

‎Akatafuta mentor.

‎Akaanza kuandika kila kitu anachotumia.

‎Leo hii?

‎Ana duka lake la simu.

‎Anauza online.

‎Anatoa ushauri kwa vijana wengine.

‎Na bado ni yule yule – Baba T ila mwenye mwongozo mpya wa maisha.

‎Na Wewe Unaweza Kubadilika Leo…

‎Ukiamua, unaweza.

‎Ukiwa na mwongozo sahihi, maisha yanabadilika.

‎Unapunguza makosa.

‎Unafupisha safari ya mateso.

‎Unapanda ngazi haraka.

‎Chukua hatua.

‎Andika malengo yako.

‎Soma kila siku.

‎Tafuta watu wanaojua kuliko wewe.

‎Achana na kelele za mtaani.

‎Focus.

‎Maisha ni yako.

‎Na hakuna atakayeyaishi kwa niaba yako.

‎Unataka mafanikio ya kweli?

‎Tafuta mwongozo.

‎Fuata mfumo.

‎Jitahidi bila kusahau mwelekeo.

‎Maisha si bahati.

‎Ni maamuzi na maandalizi.

ENDELEA   KUSOMA  HAPA   UTAPATA    RAMANI  YA  MABADILIKO   NA  DIRA    YA  MAISHA  YAKO. 

KITABU 53 : WANA WA IBRAHIMU---WAKRISTU NA WAISLAMU---( 03 )---IMANI MBALIMBALI ZA WANA WA IBRAHIMU----FULL NUKU / NOTES----TOLEO LA NANE , 1976----NA H.P. ANGLARS------TANZANIA------( PDF )--------CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136

Sunday, May 18, 2025

KITABU 342 ---ROSA MISTIKA --FULL KITABU---NA E. KEZILAHABI-----( PDF )------CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136

MAKALA : NGUVU YA KUTENDA MIUJIZA NA NDOTO ZAKO UMEIBEBA WEWE MWENYEWE NA SI MTU MWINGINE--------NA MWL. JAPHET MASATU -------CALL / SMS / WHATSAPP + 266 716 924 136

 Kakaa/Dadaa Yangu...

‎Umesahau wewe ni nani.

‎Umesahau kuwa ndani yako kuna nguvu ya kutikisa dunia.

‎Umejikatia tamaa kimya kimya.

‎Kila siku unasema *labda mimi sina bahati.*

‎Umeanza kuamini maisha ni magumu na huwezi kubadilisha chochote.

‎Lakini ukweli ni huu: UNA NGUVU YA MIUJIZA NDANI YAKO  ,  

‎Unaitumia vibaya.

‎Au hujui hata ipo.

‎Ulishawahi kumuona mtu aliyeanzisha biashara kwa buku 5 akafika juu?

‎Ulishawahi kumuona mtu aliyefeli shule lakini leo anaajiri waliopata division one?

‎Ulishawahi kumuona mtu aliyetelekezwa, akasota, lakini leo anajenga nyumba yake?

‎Wote hawa hawakuwa na miujiza ya mbinguni.

‎Walitumia nguvu ya ndani waliyoamka nayo kila siku.

‎Na hiyo nguvu wewe pia unayo.

‎Lakini... unaitumia kuskroll TikTok.

‎Unaitumia kulalamika.

‎Unaitumia kutafuta huruma badala ya suluhisho.

‎Una nguvu lakini hauna mwelekeo.

‎Miujiza sio kupasuliwa mbingu.

‎Sio malaika kushuka.

‎Miujiza ni pale mtu wa kawaida anapoamua kuamka na kuchukua hatua isiyo ya kawaida.

‎Ni pale mtu anapoamua kuamka kabla ya wengine.

‎Kuanza kuandika ndoto zake.

‎Kuanza kusoma vitabu badala ya magazeti ya udaku.

‎Kuanza kuomba kazi kwa bidii badala ya kuomba msaada.

‎Miujiza ni matokeo ya msimamo.

‎Suluhisho Lipo. Na Lipo Ndani Yako.

‎Badilisha namna unavyofikiri.

‎Acha kusema “sina mtaji” sema “naanza na hiki kidogo.”

‎Acha kusema “nimechelewa”  sema “leo ndiyo siku yangu ya kwanza.”

‎Acha kujificha nyuma ya visingizio.

‎Toka uvunguni.

‎Toka kwenye comfort zone ya umaskini wa mawazo.

‎Chukua hatua.

‎Anza leo.

‎Fanya kitu.

‎Kwa sababu NGUVU YA MIUJIZA UMEIBEBEA WEWE MWENYEWE.

‎Bado namkumbuka....

‎Kuna bro mmoja alichoka na maisha.

‎Alikuwa hana kazi. Hana mtaji. Hana cheti.

‎Alikaa chini akaandika: “Mwaka huu lazima niwe mtu mwingine.”

‎Akaanza kuuza karanga mtaani.

‎Akaweka akiba ya mia mia.

‎Alikuwa anasoma vitabu alivyokopeshwa.

‎Alifungua YouTube kujifunza marketing.

‎Miaka mitatu baadaye...

‎Ana biashara ya kuuza nafaka.

‎Ana familia.

‎Ana ndoto mpya kila mwaka.

‎Aliniambia hivi:

‎“Miujiza haikunitokea, niliitengeneza mwenyewe.”

‎Sasa Wewe Una Sababu Gani Ya Kukata Tamaa?

‎Huna sababu.

‎Una kila sababu ya kusimama.

‎Chukua kalamu na kuandika ndoto zako.

‎Zima data saa tatu usiku na kupanga kesho yako.

‎Na anza kutenda miujiza ya kweli kupitia nguvu yako ya ndani.

‎Kumbuka: Miujiza Haiporomoki.

‎Miujiza hutengenezwa.

‎Na hutengenezwa na watu kama wewe.

‎Watu wa kawaida lakini walioamua kuishi maisha ya ajabu.

 

ENDELEA   KUTEMBELEA    BLOG  HII     UTAJIFUNZA  MENGI   "  MAISHA    NA  MAFANIKIO ( LIFE  &   YOU  )  BLOG  "  PENDA    KUNUNUA    VITABU  NA    KUVISOMA   UTAGUNDUA  SIRI  NYINGI   ZA  DUNIA  HII.

KITABU 341--THE AUTO BIOGRAPHY OF MARTIN LUTHER KING , JR----FULL BOOK----1998-----( PDF )------CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136

Friday, May 16, 2025

MAKALA : SHERIA 100 ZA MAISHA NA MAFANIKIO -----NA MWL JAPHET MASATU ---- CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136

Kakaa/Dadaa Yangu...

‎Watu wengi wanakufa maskini si kwa sababu walizaliwa maskini…

‎Wanabaki maskini kwa sababu wanaishi bila sheria.

‎Wanapiga hatua moja mbele… halafu wanarudi tatu nyuma.

‎Siku zinaenda, miaka inasonga… maisha yanabaki pale pale.

‎Unaamka, unaenda kazini… lakini huna cha maana unaweka mezani.

‎Kila ukijaribu kusonga, kuna kitu kinakuvuta nyuma.

‎Unajua ni nini?

‎Huna ramani.

‎Huna sheria.

‎Huna mwelekeo.

‎Na Hapo Ndio Unatupwa Katika Kundi la “Wanaojitahidi Tu”

‎Unahangaika sana, lakini hakuna matokeo.

‎Unasoma vitabu, unaenda semina… lakini maisha yako hayabadiliki.

‎Una marafiki wanafanikiwa, lakini wewe bado unahaha.

‎Una ndoto, lakini hazina miguu.

‎Una malengo, lakini hayatimizwi.

‎Una nia nzuri, lakini hakuna mbinu.

‎Inachosha.

‎Inaumiza.

‎Inavunja moyo.

‎Unaweza ukajiona kama vile maisha yamekuchoka.

‎Kila kitu kinagoma.

‎Kila mtu anakupita.

‎Wewe unabaki unaangalia… ukiwa na maswali kuliko majibu.

‎Na Tatizo Halipo Kwenye Bahati… Lipo Kwenye Mfumo Wako

‎Wengi wanangoja bahati.

‎Wanasema: “Siku moja nitapanda juu.”

‎Hiyo siku haiji.

‎Kwa sababu hawafuati sheria.

‎Sheria za maisha.

‎Sheria za mafanikio.

‎Hakuna mafanikio bila sheria.

‎Kama vile gari halisafiri bila barabara.

‎Kama vile mti hauoti bila mizizi.

‎Maisha yanahitaji misingi.

‎Na misingi hiyo ni sheria.

‎Na sio sheria ngumu.

‎Ni zile rahisi.

‎Zenye mantiki.

‎Zenye mpangilio.

‎Lakini wengi hawajui.

‎Wengine wamewahi kusikia, lakini hawafuati.

‎Na ndio maana maisha yao ni kama gari lililoharibika breki, linaenda tu... bila mwelekeo.

‎Sasa Hii Ndio Dawa – Sheria 100 Za Maisha Ya Mafanikio

‎Nimekuandalia sheria hizi kwa jasho na damu.

‎Zimetoka kwa tajiri aliyewahi kulala kwenye dari la mabati.

‎Zimetoka kwa kijana aliyekua anauza vocha, leo ana kampuni.

‎Zimetoka kwa mwanamke aliyetelekezwa, leo ana biashara tano.

‎Sheria hizi ni silaha.

‎Zikupatie mwelekeo.

‎Zikupatie nguvu ya kupambana.

‎Zikusaidie kuachana na maisha ya mdundo mmoja.

‎Ukitaka kubadilisha maisha yako…

‎Ukitaka kuamka kutoka usingizini...

‎Sheria hizi ni Biblia / Juzuu yako mpya.

‎Sikiliza Story ya Kelvin Kijana Aliyeamua Kubadilika

‎Kelvin alikua anaishi Tandale, kwa mama wa kambo.

‎Alikua anafukuzwa shule kila siku —si kwa sababu ni mjinga, bali hakuwa na sare.

‎Alikua anaota kuwa mtu mkubwa, lakini mtaa ulimcheka.

‎Siku moja akapewa kitabu kidogo tu kilikua na "Sheria 100 Za Maisha Ya Mafanikio"

‎Akakisoma.

‎Akaanza kubadili tabia.

‎Akaanza kuamka mapema.

‎Akaanza kujifunza kila siku.

‎Akaacha kulalamika.

‎Leo Kelvin ni mkurugenzi wa kampuni inayouza bidhaa mitandaoni.

‎Analipa kodi.

‎Anasaidia mama yake.

‎Anafundisha vijana wenzie.

‎Na yeye anasema hivi:

‎"Maisha yanabadilika pale unapofuata sheria za maisha, si pale unapongoja msaada."

‎Sasa Ni Zamu Yako

‎Sheria 100 hizi si hadithi za kuburudisha.

‎Ni mashine ya kukutoa kwenye maisha ya hovyo hovyo.

‎Ni mwelekeo mpya wa mafanikio.

‎Ukiamua kuzifuata, hakuna kitakachokuzuia.

‎Ukiamua kuzipuuza, usilalamike maisha yanapokuchezea.

ENDELEA   KUPERUZI    NA   KUSOMA  BLOG  HII  "  MAISHA    NA   MAFANIKIO  (  AND  LIFE  )   BLOG " 

ILI  UJIFUNZE  SHERIA/  KANUNNI   ZA  KUFANIKIWA  KATIKA  MAISHA    YAKO.