Friday, May 30, 2025

MAKALA : MJASIRIAMARI MJANJA ANA TABIA GANI ???

 Kakaa/Dadaa Yangu,

‎ Unajua shida ya wengi?

‎Wengi wanaanza biashara kwa kishindo...

‎Lakini baada ya miezi mitatu,

‎BAM! Kimya kama kaburi la usiku.

‎Wanaanza kuuza nguo,

‎Wanaingiza mzigo wa milioni mbili,

‎Lakini hakuna anayenunua.

‎Wanashindwa kuelewa nini kinakwenda kombo.

‎Wanakata tamaa fasta.

‎Wanarejea kutegemea mshahara.

‎Wengine wanakata tamaa kabisa—wanakufa na ndoto zao.

💔 Na hapa ndipo kuna maumivu makali.

‎Biashara si kupost tu bidhaa kwenye status.

‎Si kutegemea rafiki zako watanunua.

‎Wala si kushusha bei kila siku eti "promo."

‎Ukiwa huna akili ya mjasiriamali mjanja

‎utachezewa kama karata mitaani.

🎯 Ngoja nikufunze kitu.

‎Mjasiriamali mjanja ana akili ya pesa.

‎Anajua kutafuta wateja wake popote.

‎Anajua jinsi ya kuwashawishi bila kusumbua.

‎Anajua kutoa ofa ambayo haiwezi kukataliwa.

‎Anaelewa psychology ya mteja.

‎Na zaidi ya yote, anajua kuji-brand.

‎Na kama hujui hayo yote,

‎Usijidanganye eti “ni mapenzi ya Mungu.”

‎Ni mapenzi ya kukosa maarifa.

⚙️ Sasa suluhisho liko hivi:

‎Ukiamua kuwa mjanja kwenye biashara

‎Lazima ujue kuuza hadithi.

‎Ndiyo, HADITHI!

‎Watu wananunua stori kabla ya bidhaa.

‎Wakiigusa hadithi yako,

‎Wanafika mwisho wa status tayari wamejishawishi.

‎Ukiuza sabuni,

‎Usiuze sabuni uza usafi wa mtoto wako.

‎Ukiuza viatu,

‎Usiuze kiatu uza heshima ya mguu wake kazini.

‎Mjasiriamali mjanja anauza HISIA si bidhaa tu.

🧠 Nikupe hadithi moja ya kweli.

‎Mrembo mmoja anaitwa Amina.

‎Alikuwa anauza mikoba Kariakoo.

‎Alihangaika sana, kila siku status 50, likes 2, wateja 0.

‎Alipojifunza kuuza kwa stori, mambo yalianza kubadilika.

‎Siku moja aliandika:

‎“Mwanamke mmoja alikuja dukani kwangu, akiwa amechoka, alinyamaza muda mrefu...

‎Aliponunua hii handbag,

‎Alisema, ‘Kwa mara ya kwanza najihisi mwanamke kamili.’

‎Niliogopa kusema chochote,

‎Ila moyo wangu ulichanua.

‎Na hapo ndipo nilijua,

‎Siuzi mikoba, nauza imani kwa mwanamke.”

‎Dakika 20 baadaye mikoba 7 iliuzwa.

MAKALA : MJASIRIAMALI MJANJA NA MBUNIFU NI NANI ??

 

Ni yule anayejifunza kila siku.

‎Anayefikiria tofauti.

‎Anayejua kutumia lugha ya wateja.

‎Anayeuza kwa hisia, si bei.

‎Wewe je?

‎Upo kwenye biashara kwa bahati,

‎Au umeamua kuwa MJASIRIAMALI MJANJA?

‎ Kumbuka hii ya mwisho:

‎Wakati wengine wanauza bidhaa,

‎MJANJA ANAUZA STORI INAYOCHOMA MOYO.

‎MUHIMU; Kama bado hujasoma kitabu cha MJASIRIAMALI MJANJA,

‎Ukweli ni kwamba unajipunja,

BOOK 345 --- I CAN , I MUST , I WILL ----THE SPIRIT OF SUCCESS ---BY DR. REGINALD ABRAHAM MENGI---TANZANIA---2018-----( PDF )-----CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716924 136

Thursday, May 22, 2025

KITABU 342 : KITABU CHA HADITHI ----HAIBA NA MBILIKIMO SABA-----IMETOHOLEWA KUTOKA NGANO YA ULAYA NA PILLI DUMEA----1997----( SNOW WHITE AND THE SEVEN DWARFS BY BROTHERS GRIMM )----( PDF )-----KWA WATOTO WA TANZANIA----CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136

MAKALA : MAISHA SI BAHATI NASIBU AU KUBET . NI RAMANNI YA MABADILIKO NA DIRA . NI MAAMUZI NA MAANDALIZI------NA MWL. JAPHET MASATU------TANZANIA -------FRIKA YA MASHARIKI--------CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136

 Kakaa/Dadaa....

‎Unajua shida kubwa inayowakumba wengi?

Wanaamka kila siku…

‎Wanakimbizana kama mchwa waliomwagiwa maji…

‎Lakini hawajui wanakimbilia wapi.

‎Kila siku ni kujituma…

‎Lakini mwisho wa mwezi, mfuko ni kama shimo la panya.

‎Kila mwaka unakatika…

‎Lakini hakuna mabadiliko ya maana.

‎Wengi wako kwenye 'autopilot' ya maisha.

‎Wanajisukuma tu.

‎Wakiamini ipo siku mambo yatajileta.

‎Mambo hayajileti. Wewe ndo lazima uyasogeze.

‎Hii Inatisha Kidogo…

‎Unaamka ukiwa na nguvu.

‎Unaota mafanikio.

‎Lakini kila jioni, unarudi na uchovu tu.

‎No progress.

‎No peace of mind.

‎Unasema utabadilika kesho.

‎Kesho ikifika, unafanya yaleyale.

‎Ni kama umefungwa pingu zisizoonekana.

‎Hii ni hatari sana.

‎Inaua ndoto zako taratibu bila kelele.

‎Alafu unakuja kushangaa:

‎“Mbona maisha yananizunguka?”

‎Ni kwa sababu hakuna mwongozo.

‎Kuna Uongo Mmoja Mkubwa…

‎Eti “kuwa na bidii, utafanikiwa.”

‎Wongo huo.

‎Watu wengi wana bidii kuliko hata gari la kubeba mawe.

‎Lakini wako pale pale.

‎Tatizo si bidii.

‎Tatizo ni kutokuwa na DIRA.

‎Hakuna ramani.

‎Hakuna mwongozo.

‎Na kama hujui unakokwenda…

‎Hutajua hata ukifika.

Sasa Sikiliza Vizuri…

‎Maisha yako yanahitaji mfumo.

‎Mfumo wa kuweka malengo.

‎Kujijua wewe ni nani.

‎Unataka nini.

‎Na kwa nini unakitaka.

‎Halafu?

‎Anza kupanga hatua ndogo ndogo.

‎Kila siku.

‎Kidogo kidogo hadi kikamilike.

‎Na muhimu zaidi, tafuta maarifa ya kweli.

‎Si porojo.

‎Maarifa ya watu waliopitia moto.

‎Walioungua.

‎Wakaamka.

‎Wakasimama tena.

‎Ngoja Nikupe Kisa Cha Huyu Bwana Mdogo Hapa…

‎Kuna Bwana Mdogo mmoja mtaani kwetu Anaitwa Baba T.

‎‎Miaka mitano iliyopita alikuwa anauza vocha na peremende stendi.

‎Maskini alikua anavaa viatu vilivyochanika…

‎Watu walimcheka.

‎Lakini kuna siku moja aliniambia:

‎“Bro, nimeshaamua. Sitaki kufa maskini. Nataka mafanikio ya ukweli.”

‎Akanunua daftari.

‎Akaandika malengo yake.

‎Akasoma vitabu.

‎Akatafuta mentor.

‎Akaanza kuandika kila kitu anachotumia.

‎Leo hii?

‎Ana duka lake la simu.

‎Anauza online.

‎Anatoa ushauri kwa vijana wengine.

‎Na bado ni yule yule – Baba T ila mwenye mwongozo mpya wa maisha.

‎Na Wewe Unaweza Kubadilika Leo…

‎Ukiamua, unaweza.

‎Ukiwa na mwongozo sahihi, maisha yanabadilika.

‎Unapunguza makosa.

‎Unafupisha safari ya mateso.

‎Unapanda ngazi haraka.

‎Chukua hatua.

‎Andika malengo yako.

‎Soma kila siku.

‎Tafuta watu wanaojua kuliko wewe.

‎Achana na kelele za mtaani.

‎Focus.

‎Maisha ni yako.

‎Na hakuna atakayeyaishi kwa niaba yako.

‎Unataka mafanikio ya kweli?

‎Tafuta mwongozo.

‎Fuata mfumo.

‎Jitahidi bila kusahau mwelekeo.

‎Maisha si bahati.

‎Ni maamuzi na maandalizi.

ENDELEA   KUSOMA  HAPA   UTAPATA    RAMANI  YA  MABADILIKO   NA  DIRA    YA  MAISHA  YAKO.