BADILI FIKRA.FIKIRI TOFAUTI .BADILI MAISHA.JITAMBUE .JIFUNZE ELIMU YA SAIKOLOJIA,TEOLOJIA , FEDHA ,UTAMBUZI(SELF HELP EDUCATION),FALSAFA YA MAISHA,MAISHA NA MAFANIKIO,BIASHARA / UJASIRIAMALI.FURAHIA WASAA WAKO NA MAISHA NA MAFANIKIO BLOGU.THIS IS THE COMMUNITY CAPACITY BUILDING BLOG.ENJOY THE BLOG.STRETCH YOUR MIND. YOU CAN CHANGE YOUR LIFE FOR EVER. YOU CAN ACHIEVE EXCELLENCE.YOU CAN MAKE A DIFFERENCE. JIFUNZE ---ELIMIKA --CHUKUA HATUA---FANIKIWA
Simu yaweza kumsaidia mtoto kujifunza lakini bado nimuhimu kwa mzazi kuwa makini
Hivi karibuni
imekuwa kawaida sana kumkuta mtoto anatumia simu ya mkononi ya mzazi
wake na mara nyingine wanatumia bila hata kupata ridhaa ya mzazi
mwenyewe.
Baadhi ya watoto huonyesha utaalamu wa hali ya juu katika kufungua kurasa mbalimbali za simu hizo.
Na inadaiwa kuwa kuna watoto ambao huwa wanajifunza mambo mengi kupitia simu za mkononi. Hata
hivyo si wazazi wote ambao hukubali simu zao zitumiwe na watoto, baadhi
huwa wakali na kuweka kila aina ya nywila ingawa wengine huwa hawaoni
shida kuwapatia watoto wao simu punde tu wanaporejea kutoka kwenye
majukumu yao ya kila siku.
Baadhi ya wazazi huwa wanaona kuwa simu ndio njia pekee inayoweza
kuwafanya watoto wao watulie na wao wapate muda wa kupumzika ama hata
kufanya shughuli zao za nyumbani.
Je,kuna faida yeyote endapo mtoto atatumia simu? BBC
imezungumza na baadhi ya wazazi ili kufahamu ni kwa kiasi gani watoto
wao hutumia simu zao na wanawadhibiti vipi vitu anavyoangalia mtoto?
"Kwa
kweli simu yangu hata sina uhuru nayo huwa nikifika tu nyumbani wanangu
huwa wananipokea kwa mbwembwe zote na cha kwanza kubeba ni simu na
nikihitaji lazima niwaombe wao. Simu ikiita utakuta wao ndio
wanapokea,mara nyingi wanaangalia video za kartoon au za watoto wenzao
zilizopo you tube," Mama Brian anaeleza
Baadhi ya watoto hutambua hadi nywila za simu za wazazi wao
Alex Kayetta ambaye ni baba wa mtoto mmoja, anasema simu yake huwa haimiliki punde tu anapofika nyumbani , "Mwanangu
akishashika simu yangu yani kuipata lazima nimbembeleze, na akichukua
mara nyingine huwa lazima nimtafute alipo ,kuna siku nilimkuta amejificha
ndani ya beseni akicheza michezo ya kwenye simu'game' nikampiga
picha".
Freddie Kyara ni mwanasaikolojia kutoka nchini Tanzania
ambaye anaeleza kuwa hali hii huwa inafanana na jinsi mzazi anapokua
kwenye simu muda mrefu na hupoteza fursa ya kuwa karibu jamii na ndivyo
hivyo inavyotokea kwa mtoto.
Na kwa upande wa mtoto kutumia simu huwa kuna madhara pia "Kukua kwa
mtoto kunahitaji awe na mbinu za kijamii, kama vile kucheza na watoto
wenzake na kujifunza mambo mbalimbali kutoka kwa wenzake, lakini siku
hizi unaweza kukuta mtoto anashindwa kucheza na watoto wengine kwa
sababu amezoea yeye rafiki yake ni simu tu.
Ubunifu wa mtoto
unaweza kupungua. Sisi wakati tunakuwa hatukuwa tunajua habari za simu,
ilikuwa ni kucheza mpira na kujishughulisha na shughuli mbalimbali za
nyumbani na hali hiyo ilitufanya tuweze kujenga urafiki na watu na kujua
tabia za watu tofautitofauti.
Mtoto anaweza kujifunza pia kwenye
simu lakini lazima uthibiti uwepo kwa sababu sio kila kilichopo kwenye
simu kina maudhui mazuri kwa watoto na wanapaswa kutengewa muda" Kyara
,mtaalamu wa saikolojia alieleza.
Hata hivyo jumbe mbalimbali zimekuwa zikisambaa kuonya madhara ya
mionzi ya simu kwa watoto wadogo na kudai kuwa umri sahihi wa kupewa
simu ni kuanzia miaka kumi na sita. Jambo ambalo Daktari Fredrick
Mashili anasema madhara ya namna hiyo huwa inategemeana zaidi na umri wa
mtoto japo kwa upande mwingine macho yanaweza kupata shida ingawa
hakuna ushahidi wa kutosha kuthibitisha madhara hayo ya mionzi.
"Kuna
wasiwasi kwamba mtu akianza kutumia simu mapema anaongeza muda wa
kuyashughulisha macho yake katika mionzi kwa muda mrefu zaidi kitu
ambacho si kizuri kwa afya ya macho," Dkt.Mashili alieleza.
Linapokuja swala la fedha, kila mtu ana namba na viwango vyake. Kwa
sababu tunatofautiana ndoto, kazi/biashara, kipato, mitindo ya maisha na
hata mazingira, matokeo yetu ya kifedha hayawezi kulingana.
Hivyo kujipima hatua ulizopiga kifedha kwa kuwatumia wengine ni
kujiumiza na hata kujirudisha nyuma, kwa sababu kuna namba nyingi ambazo
utakuwa huzijui kuhusu wengine. Kwa mfano unaweza kumwona mtu kwa nje
anaonekana kuwa na vitu vinavyoashiria ana fedha nyingi, lakini kumbe
vitu vyote hivyo amepata kwa mkopo ambao ataulipa maisha yake yote. Pia unaweza kumwona mtu ukafikiri hayupo vizuri kifedha kwa mwonekano
wake wa nje, kumbe anafanya uwekezaji ambao baadaye utamwezesha kufikia
uhuru wa kifedha.
Kwa kuwa ni vigumu kupima hatua ulizopiga kifedha kwa kuwatumia watu wengine, unahitaji kujitumia wewe mwenyewe.
Kiasi cha fedha unachotoa kwa wengine bila ya kutegemea kupata
chochote ni kiwango kingine muhimu sana cha kupima afya yako kifedha na
kujua hatua ulizopiga. Kwa kadiri unavyotoa zaidi ndivyo unavyoonesha
kwamba unaitumia fedha na siyo fedha inakutumia wewe.
Unahitaji kuwa na utaratibu wa kutoa fedha kuwasaidia wengine bila ya
kutegemea kulipwa fedha hizo. Kwa sababu tunatoshelezwa zaidi na utoaji
kuliko upokeaji.
Pia unapotoa fedha kwa wengine, unatengeneza pengo ambalo itabidi
lizibwe, hivyo unakuwa umejiweka kwenye nafasi ya kuongeza kipato chako
zaidi.
Hichi ni kiwango kinachoonesha maandalizi yako uliyonayo sasa kwa
upande wa fedha. Kadiri unavyokuwa na akiba kubwa kifedha, ndivyo
unavyoweza kujilinda na dharura mbalimbali zinazoweza kukutokea. Akiba
unayokuwa nayo ndiyo itakukinga usiingie kwenye madeni mabaya pale
unapokutana na changamoto ambazo hukuzitegemea.
Kiwango sahihi cha akiba unayopaswa kuwa nayo ni ile inayoweza
kutosheleza kuendesha maisha yako kwa miezi 6 mpaka mwaka mmoja hata
kama utakuwa huna kipato kabisa katika kipindi hicho.
Kuza kiwango chako cha akiba na hili litakupa pumziko na kukuondolea
wasiwasi kuhusu fedha kitu ambacho kitakuwezesha kufanya mambo yako kwa
utulivu na ufanisi mkubwa.
Kiasi cha fedha unachodaiwa na wengine kutokana na vitu ulivyonunua
bila ya kuwa na fedha ni kipimo cha maamuzi yako ya kifedha kwa siku za
nyuma. Kadiri madeni yako yanavyokuwa makubwa, ndivyo sehemu kubwa ya
kipato chako inavyoelekea kwenye kulipa madeni hayo na wewe kubaki na
kiasi kidogo ambacho hakiwezi kukutosheleza.
Unahitaji kutokuwa na deni binafsi kabisa, na madeni mazuri
unayopaswa kuwa nayo ni yale yanayojilipa yenyewe. Madeni yanayojilipa
yenyewe ni yale ambayo yanazalisha faida na faida hiyo unatumia kulipa
deni. Haya ni madeni ambayo hayakuumizi.
Lakini madeni ambayo unalipa kwa fedha zako unazopata kwenye shughuli
zako binafsi, ni utumwa ambao utakutesa kwa muda mrefu. Kama upo kwenye
madeni ya aina hii kazana kuondoka na usiingie tena ili kuepuka
kujiweka kwenye wakati mgumu kifedha.
Kiwango ambacho umekiwekeza kwenye maeneo ambayo yanazalisha riba au
faida ni kipimo muhimu kwa maandalizi yako ya kifedha ya baadaye. Kama
hapo ulipo hujafanya uwekezaji wote kwa ajili ya baadaye, kama hujawa na
maandalizi ya kukuwezesha kuingiza kipato bila ya wewe kufanya kazi
moja kwa moja, huna maandalizi ya kifedha ya baadaye, na haupo eneo zuri
kifedha.
Unahitaji kufanya uwekezaji kwa ajili ya baadaye, kwa sababu utakuja
wakati ambapo huna uwezo wa kufanya kazi kama unavyofanya sasa, lakini
una mahitaji muhimu kwa maisha yako. Unapokuwa umewekeza na uwekezaji
unazalisha, maisha yako yanakwenda vizuri.
Kiwango sahihi cha uwekezaji unachopaswa kuwa nacho ni kile ambacho
kinazalisha faida au riba ambayo inakuwezesha wewe kuendesha maisha yako
kwa kadiri ya mahitaji yako.
Watu wawili wanaweza kushindwa kwenye kitu kimoja, mmoja akachukulia
kushindwa huko kama kichocheo cha kufanya zaidi na akafanikiwa. Mwingine
anaweza kuchukulia kushindwa huko kama sababu ya kukata tamaa na
kushindwa kabisa.
Tukio ni moja, tafsiri tofauti na matokeo tofauti kabisa. Siyo kinachotokea, bali namna unavyotafsiri kinachotokea ndiyo inaleta madhara kwako. Kwenye Falsafa ya Ustoa pia kuna dhana inayoitwa upili wa udhibiti.
Dhana hii inaeleza kwamba vitu vyote vinavyotokea kwenye maisha yako,
vinagawanyika katika makundi mawili, kundi la kwanza ni vitu unavyoweza
kuviathiri, hivi vipo ndani ya uwezo wako. Kundi la pili ni vitu
usivyoweza kuviathiri, hivi vipo nje ya uwezo wako.
Hivyo unapokutana na chochote na ukajiambia ni kigumu au
kinakushinda, huna haja ya kusumbuka, badala yake jiulize je kipo ndani
ya uwezo wako au nje ya uwezo wako. Kama kipo ndani ya uwezo wako chukua
hatua sahihi, kama kipo nje ya uwezo wako kikubali kama kilivyo au
kipuuze. Hakuna namna bora ya kuendesha maisha yako kama hii, kwa sababu
hakuna chochote kitakachotokea, ambacho kitakuvuruga kabisa.
Ndugu yangu , nikukumbushe tena ya kwamba kama unataka kuitawala dunia,
kuna mtu mmoja unayepaswa kumtawala, na mtu huyo ni wewe mwenyewe.
Hutaweza kujitawala wewe mwenyewe kwa mabavu au nguvu, badala yake
utajitawala kwa kudhibiti mawazo yako na hisia zako.