Saturday, August 1, 2026

MUNGU HAKUKAMILISHA DUNIA: KWANINI ALIMPA MWANADAMU KIPAJI CHA UBUNIFU ??? -----NA MWL / KOCHA / COACH JAPHET MASATU-----CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136 / + 255 755 400 128

MUNGU  alitupatia  DUNIA  hii  ikiwa  haiko   kamili  ili  nasi   tushiriki  katika  UUMBAJI ( UBUNIFU ).MUNGU  alifanya  MITI  lakini  hakufanya  VITI , KABATI ,  MEZA , n.k. MUNGU  alitengeneza  ARDHI  na   MADINI  lakini  hakufanya  MAGARI , VIOO , MABATI , n,k, MUNGU hakufanya vyote  hivyo  akijua SISI  ametuumba  tukiwa  na   KIPAJI   CHA  UBUNIFU.

TUNAPOBUNI  kitu  chenye   kusaidia  binadamu   tunapata  MAFANIKIO. CHA   AJABU  SISI  TUMEKUWA  SIYO   WABUNIFU , TUNALALAMIKA  UMASKINI   NA  KUWA  OMBA   OMBA. 

 (  BY  MWL / KOCHA /  COACH   / MWANDISHI /  BLOGGER  , MOTIVATIONAL /  PUBLIC  SPEAKER    JAPHET    MASATU-----CALL /  SMS /  WHATSAPP   + 266  716  924136  /    +  255 755  400 128



1 comment:

  1. Mungu aliumba dunia na kuiweka ikiwa na rasilimali nyingi, lakini hakufanya kila kitu ambacho mwanadamu anakitumia leo. Alituumba tukiwa na akili, hekima na kipaji cha ubunifu ili tushiriki katika kuendeleza dunia kwa kutumia rasilimali alizotupa.

    Kwa mfano, Mungu aliumba miti, lakini hakutengeneza viti, meza, makabati wala milango. Alimpa mwanadamu uwezo wa kutumia miti hiyo kutengeneza vitu vinavyorahisisha maisha.

    Vilevile, Mungu aliumba ardhi yenye madini kama chuma, shaba, alumini na mchanga wa kutengenezea kioo, lakini hakutengeneza magari, mabati, vioo, ndege, kompyuta au simu. Hivyo, mwanadamu hutumia akili na ubunifu aliopewa na Mungu kubadilisha malighafi hizo kuwa bidhaa zenye manufaa.

    Kwa hiyo, ubunifu, utafiti na maendeleo ya sayansi na teknolojia vinaweza kuonekana kama sehemu ya kutumia vipaji ambavyo Mungu amewapa wanadamu. Tunapobuni, kugundua na kutengeneza vitu vinavyowanufaisha watu, tunatumia vipawa na uwezo tuliopewa, huku tukitambua kwamba chanzo cha malighafi, maisha na uwezo wa kufikiri ni Mungu.

    Hivyo basi, Mungu hakufanya kila kitu moja kwa moja, bali alimuumba mwanadamu akiwa na uwezo wa kufikiri, kubuni na kuendeleza uumbaji wake kwa matumizi yenye manufaa kwa jamii.

    ReplyDelete