Mwanamke kuwa na kazi
au biashara ya kufanya na ikamwingizia kipato ni kitu cha muhimu sana,
maana dunia ya sasa hivi tunaishi Kwa kutegemeana. Na wanawake tuna
fursa nyingi sana za kujiongeza kiuchumi kama mtu ukiwa na bidii,
uvumilivu na kutogopa vikwazo.
Nitakwenda kuorodhesha biashara au
miradi ambayo mwanamke unaweza kuifanya , kitu cha muhimu ni anza mradi
kutokana na mtaji na ujuzi ulionao na uwe unakipenda hicho kitu kutoka
moyoni;
1. Bakery: hii ni bishara ya kutengeneza na kuuza
vitafunwa inapata kasi sababu watu wengi hawapendi kununua vitafunio
mitaani, hata kama huna mtaji wa kufungua bakery unaweza kupika
vitafunwa mbalimbali nyumbani Kwa order au ku supply kwa wenye maduka au
migahawa.
2. Shule za chekechea, ni biashara nzuri Kama ukipata
eneo zuri na ukatoa huduma nzuri, na walimu wakiwa wana ujuzi wa
kutosha. Pia kama wewe ni mwalimu unaweza kuanzisha shule yako mwenyewe
kutokana na mtaji wako.
3. Event management and catering , siku
hizi sherehe ni nyingi sana na watu wawataki kuangaika na mambo ya
chakula, mc, mapambo, usafiri nk, wana kodi kampuni ya watu Kwa ajili
hiyo.
4.Ufundishaji wa ujuzi mbalimbali, wanawake wengi wana
penda kujifunza mambo mbalimbali ili watumie huo ujuzi kwenye
ujasiriamali, iwe ni kupika vyakula, utengenezaji wa sabuni, mapambo,
kilimo nk. Ukiwa na ujuzi wowote utumie kufundisha wengine na ujipatie
kipato.
5.Maduka ya urembo na kuuza nguo za wanawake, hii ni
biashara nzuri sababu supply ni kubwa mfano Dar kariakoo kuna maduka
mengi tu ya jumla unaweza kupata bidhaa, na wanaume wengi wanafanya
Biashara hii Ila ikifanywa na mwanamke ni bora zaidi unajua kabisa vitu
gani wanawake wanapenda.
6.Insurance, consultancy companies: Kama
una elimu, uzoefu na mtaji wa kutosha unaweza kuanzisha kampuni yako ya
bima au kotoa ushauri mbalimbali au watu kukupa kazi zao uwafanyie na
unaweza kufungua kampuni mbalimbali.
7.Biashara ya chakula,
unaweza kuanzisha hotel au kimgahawa na ukapika vyakula, muhimu uweze
kuandaa chakula vizuri, na kuandaa mazingira masafi na huduma ziwe
nzuri.
8.Biashara ya kuuza maua na miche, hii ni biashara unaweza
kuanza bila mtaji au mtaji kidogo sana, kama una maua yakate na uoteshe
mengi zaidi katika vifuko, pia miche ya miti au matunda unaweza
kuetengeneza kitalu, unaweza kupata maua Kwa watu hata kununua bei sio
ghali. Tafuta eneo zuri la kuuzia hata kwako muhimu ni kujitangaza.
9.Biashara ya vinywaji; soma zaidi hapa
10.Biashara ya mapambo ya nyumba
Miradi
iko mengi sana na bidii yako ya kufanya utafiti na kujifunza wengine
wanafanya nini. Pia kumbuka biashara yoyote mwanamke unaweza kufanya na
suala la mtaji sio tatizo sana mikopo ipo mradi utafute yenye masharti
nafuu.
Kwa ushauri wa BIASHARA / UJASIRIAMALI na MAISHA wasiliana nami WhatsApp 0716924136 / + 255 755 400 128 / + 255 688 361 539 / + 255 629 748 937
KOCHA MWL JAPHET MASATU
BADILI FIKRA.FIKIRI TOFAUTI .BADILI MAISHA.JITAMBUE .JIFUNZE ELIMU YA SAIKOLOJIA,TEOLOJIA , FEDHA ,UTAMBUZI(SELF HELP EDUCATION),FALSAFA YA MAISHA,MAISHA NA MAFANIKIO,BIASHARA / UJASIRIAMALI.FURAHIA WASAA WAKO NA MAISHA NA MAFANIKIO BLOGU.THIS IS THE COMMUNITY CAPACITY BUILDING BLOG.ENJOY THE BLOG.STRETCH YOUR MIND. YOU CAN CHANGE YOUR LIFE FOR EVER. YOU CAN ACHIEVE EXCELLENCE.YOU CAN MAKE A DIFFERENCE.
Wednesday, May 20, 2020
Thursday, May 14, 2020
MTAJI NI MDOGO ? --JINSI YA KUKABILIANA NA USHINDANI WA BEI .
Zifuatazo ni hatua za kuchukua ili kukabiliana na ushindani wa bei pale unapofanya biashara kwa mtaji mdogo.
(01 ). CHEZA MCHEZO WAKO MWENYEWE.
Kama
unataka kupata ushindi kwenye eneo lolote la maisha yako, basi unapaswa
kucheza mchezo wako mwenyewe. Hii ina maana kwamba unapaswa kutengeneza
mchezo wako, kujiwekea sheria zako mwenyewe, kisha kucheza mchezo huo.
Ukiingia kucheza mchezo wa wengine, ambao wameutengeneza wao na kuweka
sheria zao, huwezi kushinda, maana wao ndiyo wanaoujua mchezo huo kuliko
wewe.
Hivyo
pia ndivyo ilivyo kwenye biashara, haijalishi unafanya biashara gani,
unapaswa kucheza mchezo wako mwenyewe. Hapa unapaswa kupanga ni aina
gani ya biashara unaifanya na utaifanya kwa njia zipi. Tengeneza njia
zako mwenyewe, ambazo zinatumia uwezo ulio ndani yako na aina ya wateja
unaowalenga, kwa kile unachouza. Jiwekee sheria zako mwenyewe na kisha
endesha biashara yako kwa sheria hizo.
Chagua
kufanya biashara ya tofauti, ambapo sheria yako kuu kwenye ushindani
siyo bei, bali utofauti. Usishindane kwa kupunguza bei, bali shindana
kwa kutoa kitu ambacho biashara nyingine hazitoi. Kwa maneno mengine,
usikazane kuwa bora zaidi ya wengine, bali kazana kuwa tofauti na
wengine.
Hakikisha
kuna kitu ambacho wateja wanakipata kwenye biashara yako, ambacho
hawawezi kukipata kwenye biashara nyingine yoyote. Inaweza kuwa aina ya
bidhaa unazouza, inaweza kuwa aina ya huduma wanayoipata. Ni lazima uwe
na kitu ambacho wateja wanakipata kwako tu na hawawezi kukipata kwa
wafanyabiashara wengine.
Kama
kwenye biashara unayoifanya huwezi kutengeneza kitu cha aina hiyo,
ushindani wa bei hauwezi kukuacha salama. Usitegemee utoe kile ambacho
kinaweza kupatikana kwa wengine, halafu wateja waje kununua kwako kwa
bei juu wakati wanaweza kupata kwingine kwa bei ya chini.
Kumbuka
ubinafsi ni asili yetu binadamu, huwa tunaangalia maslahi yetu kwanza
kabla ya kitu kingine. Hivyo hakikisha kwenye biashara yako kuna kitu
unachowapa wateja wako, kinachowanufaisha na hawawezi kukipata sehemu
nyingine. Kwa kuwa na kitu hicho, watakuwa tayari kuja kununua kwako kwa
bei ya juu kuliko kwenda kwa wengine wanaouza kwa bei ya chini.
( 02 ). ANZA NA WATEJA SAHIHI.
Kuna
wateja ambao wanachoangalia ni bei tu, na wapo wateja ambao
wanachoangalia ni thamani wanayoipata. Ni vigumu sana kumshawishi mteja
anayeangalia bei rahisi kuona thamani.
Hivyo
kabla hujaweka nguvu zako kwenye ushawishi au mengine yoyote, anza na
wateja sahihi. Jua kwanza kinachomsukuma mteja kununua ni bei au
thamani.
Kama
kinachomsukuma mteja kununua ni bei peke yake, usipoteze hata muda
wako, kwa sababu atakwenda kule ambapo anapata kwa bei ya chini. Lakini
unapokutana na mteja ambaye anaangalia thamani anayoipata, hapo una
nafasi ya kumshawishi kulipa zaidi ili apate thamani zaidi.
Wateja
wa thamani siyo wengi, lakini wale wachache unaowapata watakufanya
ufurahie kuifanya biashara yako, maana huwa ni waelewa na hawakusumbui
sana.
Wateja
wa bei rahisi huwa ni wengi, lakini pia ni wasumbufu. Unaweza
kuwapunguzia bei na bado wakaona umenufaika zaidi na hivyo kutaka zaidi
kutoka kwako.
Kwa
biashara unayofanya, chagua aina ya wateja unaotaka kwenda nao, kisha
tafuta aina hiyo ya wateja. Wanapokuja wateja wanaoangalia bei tu,
waeleze thamani unayotoa na kama bado wanasisitiza kwenye bei, unaweza
kuwaelekeza wapi pa kupata kwa bei wanayotaka wao, lakini pia waoneshe
nini watakosa kwa kuangalia bei pekee.
( 03 ). KUWA KARIBU ZAIDI NA WATEJA WAKO.
Biashara
ndogo huwa zinazishinda biashara kubwa kwenye eneo hili, uwezo wa kuwa
karibu na wateja. Biashara kubwa zinahudumia watu wengi, hivyo huwa
hazihangaiki na mteja mmoja mmoja, hivyo mteja hawezi kupata upekee
kwenye biashara kubwa.
Ila
kwenye biashara ndogo, kwa sababu wateja ni wachache, ni rahisi kumpa
kila mteja upekee anaostahili. Ni rahisi kumjua kila mteja na matakwa
yake, hivyo wajibu ni kumtimizia mteja yale anayotaka kwa namna yake
mwenyewe.
Kosa
kubwa ambali wafanyabiashara wengi wadogo huwa wanafanya ni kufanya
biashara zao ndogo kama vile ni biashara kubwa, kitu ambacho
kinawagharimu sana.
Kuwa
karibu zaidi na wateja wako, wasiliana nao mara kwa mara, jua matukio
mbalimbali kwenye maisha yao, mfano siku zao za kuzaliwa, watu wao wa
karibu na kadhalika. Kisha watumie salamu au jumbe mbalimbali katika
siku zao hizo muhimu.
Tumia
kila fursa kuwapa wateja wako upekee, uwafanye wajisikie vizuri
wanapokuja kwenye biashara yako ambapo wanalipa zaidi kuliko
wanavyojisikia wanapokwenda kwenye biashara kubwa ambapo wanalipa
kidogo.
( 04 ). WAFUATE WATEJA KULE WALIPO.
Njia
nyingine ya kuongeza thamani kwa wateja wako ili wawe tayari kulipa
zaidi kwako ni kuwafuata kule walipo. Sasa hivi watu hawana muda, hivyo
wanapenda sana pale biashara inapowafuata wao kule walipo. Lakini pia
uaminifu umekuwa mdogo, hivyo watu wengi huhofia kuagiza vitu ambavyo
hawajaviona.
Wewe
kwa kuwa na biashara ndogo, una nafasi ya kujenga uaminifu na wateja
wako na kisha kuwafanya waweze kuagiza kile unachouza popote walipo na
wakapelekewa. Hii inawafanya wateja wawe tayari kulipa zaidi, kwa sababu
imewapunguzia usumbufu na upotevu wa muda kutoka walipo na kwenda
kutafuta wanachotaka.
Biashara ndogo inaweza kuwafikia wateja kule walipo kwa ufanisi zaidi kuliko biashara kubwa, hivyo tumia vizuri nafasi hiyo.
( 05 ) WEKEZA ZAIDI KWENYE BIASHARA YAKO.
Unapomtaka
mteja alipie zaidi kile anachonunua kwako, ambacho anaweza kukipata kwa
bei ya chini sehemu nyingine, lazima utengeneze mazingira ambayo
yatamfanya mteja aone anastahili kulipa zaidi. Mfano ukinunua soda ya
cocacola kwenye duka la mtaani utalipa shilingi mia tano, lakini soda
hiyo hiyo ukiinunua hotelini utalipa shilingi elfu mbili. Ukiwa hotelini
hutalalamika kwa nini uuziwe soda ya mia tano kwa shilingi elfu mbili,
kwa sababu kuna mazingira yanayokufanya uone kulipa elfu mbili ni
halali. Unakuwa umekaa eneo zuri na tulivu, unahudumiwa na watu
wanaokujali na kadhalika.
Hivyo
pia ndivyo unavyopaswa kufanya kwenye biashara yako, fanya uwekezaji
unaoipa biashara yako thamani zaidi kuliko washindani wako. Kuna kitu
kidogo sana unaweza kukifanya kwenye eneo lako la biashara na
likawafanya watu waipe thamani kubwa. Kitu hicho ni mwonekano wa eneo la
biashara, linapaswa kuwa safi na lililopangiliwa vizuri. Mtu akifika
kwenye eneo hilo anaona utofauti mkubwa, na ndani yake anakuwa tayari
kulipa zaidi.
Wewe
mwenyewe ni shahidi, huenda umewahi kufika kwenye eneo la biashara, na
kwa jinsi lilivyo na mwonekano mzuri, ukajua utatozwa gharama kubwa,
lakini ulipotozwa gharama za kawaida ukashangaa. Hiyo ndiyo hali
unayopaswa kuileta kwenye biashara yako pia, kufanya uwekezaji
unaowaandaa wateja kuwa tayari kulipa zaidi.
Mwonekano
na mpangilio wa eneo la biashara, vifaa unavyotumia na huduma unayowapa
wateja wako vinapaswa kuwa vya viwango vya juu sana kiasi cha mteja
kuona kama anakuibia pale unapomtajia bei. Na kumbuka hapa utakuwa
unawalenga wateja sahihi na siyo wale wanaoangalia bei ya chini pekee.
Rafiki,
hizo ndizo hatua tano za kuchukua ili kuweza kukabiliana na ushindani
wa bei pale unapofanya biashara kwa mtaji kidogo. Kama ulivyoona, kuna
mengi ya kufanya kuliko kuingia kwenye ushindani wa moja kwa moja kwenye
bei, ambao utakuumiza sana.
Nimalizie
kwa kukuambia hili rafiki yangu, kama upo kwenye biashara ambayo kitu
pekee unachoweza kujitofautisha nacho ni kupunguza bei, basi upo kwenye
biashara ambayo siyo sahihi. Kwa sababu kuna wengine wapo tayari
kupunguza bei zaidi yako, na wakiwa na mtaji mkubwa kuliko wewe,
watapata faida kwa kuuza kwa wengi zaidi kuliko wewe unayeuza kwa
wachache.
Hivyo
fanyia kazi haya matano uliyojifunza, na mengine yanayoendana na hayo,
lakini siyo kupunguza bei. Na kama biashara haina namna nyingine bali
bei basi achana nayo na nenda kwenye biashara sahihi, ambapo unaweza
kutengeneza mchezo wako mwenyewe na kuucheza vizuri.
JIUNGE NA DARASA ONLINE KWA KULIPIA ADA YA MWEZI , MWAKA---UJIFUNZE KWA UNDANI NA MAPANA--ELIMU YA BIASHARA & UJASIRIAMALI--- NA UCHUKUE HATUA --UTAFANIKIWA
SEE YOU AT THE TOP
Ndimi rafiki yako KOCHA / MWL. JAPHET MASATU , BLOGGER
Kwa maelekezo zaidi tuwasiliane kwa ;--
SIMU / MESEJI / ( WhatsApp + 255 716 924136 ) / +255 755 400128 / + 255 688 361 539 / + 255 629 748 937
JIUNGE NA DARASA ONLINE KWA KULIPIA ADA YA MWEZI , MWAKA---UJIFUNZE KWA UNDANI NA MAPANA--ELIMU YA BIASHARA & UJASIRIAMALI--- NA UCHUKUE HATUA --UTAFANIKIWA
SEE YOU AT THE TOP
Ndimi rafiki yako KOCHA / MWL. JAPHET MASATU , BLOGGER
Kwa maelekezo zaidi tuwasiliane kwa ;--
SIMU / MESEJI / ( WhatsApp + 255 716 924136 ) / +255 755 400128 / + 255 688 361 539 / + 255 629 748 937
Saturday, April 25, 2020
Friday, April 24, 2020
Saturday, April 18, 2020
UJASIRIAMAARIFA , BIDHAA 10 ZA KIDIJITALI UNAZOWEZA KUUZA MTANDAONI NA KUINGIZA KIPATO.
Kuna bidhaa nyingi za kidijitali unazoweza kuuza mtandaoni na ukaingiza kupato kwa muda mrefu.
1. Vitabu
2. Makala
3. Picha
4. Michoro
5. Muziki
6. Ushauri
7. Kozi
8. Ukocha
9. Blog
10. Matangazo.
Tumia mtandao wa intaneti kwa manufaa, jua jinsi ya kuingiza kipato mtandaoni kwa kutumia blog.
Thursday, April 16, 2020
UJASIRIAMAARIFA , LIPWA KWA MAARIFA NA TAARIFA ULIZONAZO.
Tunaishi kwenye zama za TAARIFA na / MAARIFA ,Hivyo mwenye maarifa na taarifa zenye manufaa makubwa kwa wengine, ndiyo wanaonufaika sana.Na hapo kuna aina mpya ya ujasiriamali ambao unahusisha maarifa, ambao tunauita UJASIRIAMAARIFA.Kupitia ujasiriamali huu, unaweka maarifa na taarifa ulizonazo kwenye kifurushi ambacho wengine wanaweza kununua kama nakala ngumu (HARDCOPY ) au tete.( SOFTCOPY )
Unaweza kujifunza kwa kina kuhusu ujasiriamaarifa katika Mada ya JINSI YA KUTENGENEZA FEDHA MTANDAONI KWA KUTUMIA BLOG. Una maarifa na taarifa nyingi, anza kuziuza sasa .
WASILIANA NA KOCHA MWL JAPHET MASATU AKUTENGEHEZEE BLOG YAKO LEO NA UJUE JINSI YA KUFANYA HIVYO. ----- Call / SMS / WhatsApp / +255 716924136 / + 255 755 400128 / + 255 688361539
Subscribe to:
Posts (Atom)