Wednesday, May 20, 2020

MIRADI 10 INAYOWEZA KUENDESHWA NA WANAWAKE

Mwanamke kuwa na kazi au biashara ya kufanya na ikamwingizia kipato ni kitu cha muhimu sana, maana dunia ya sasa hivi tunaishi Kwa kutegemeana. Na wanawake tuna fursa nyingi sana za kujiongeza kiuchumi kama mtu ukiwa na bidii, uvumilivu na kutogopa vikwazo.
Nitakwenda kuorodhesha biashara au miradi ambayo mwanamke unaweza kuifanya , kitu cha muhimu ni anza mradi kutokana na mtaji na ujuzi ulionao na uwe unakipenda hicho kitu kutoka moyoni;

1. Bakery: hii ni bishara ya kutengeneza na kuuza vitafunwa inapata kasi sababu watu wengi hawapendi kununua vitafunio mitaani, hata kama huna mtaji wa kufungua bakery unaweza kupika vitafunwa mbalimbali nyumbani Kwa order au ku supply kwa wenye maduka au migahawa.

2. Shule za chekechea, ni biashara nzuri Kama ukipata eneo zuri na ukatoa huduma nzuri, na walimu wakiwa wana ujuzi wa kutosha. Pia kama wewe ni mwalimu unaweza kuanzisha shule yako mwenyewe kutokana na mtaji wako.

3. Event management and catering , siku hizi sherehe ni nyingi sana na watu wawataki kuangaika na mambo ya chakula, mc, mapambo, usafiri nk, wana kodi kampuni ya watu Kwa ajili hiyo.

4.Ufundishaji wa ujuzi mbalimbali, wanawake wengi wana penda kujifunza mambo mbalimbali ili watumie huo ujuzi kwenye ujasiriamali, iwe ni kupika vyakula, utengenezaji wa sabuni, mapambo, kilimo nk. Ukiwa na ujuzi wowote utumie kufundisha wengine na ujipatie kipato.

5.Maduka ya urembo na kuuza nguo za wanawake, hii ni biashara nzuri sababu supply ni kubwa mfano Dar kariakoo kuna maduka mengi tu ya jumla unaweza kupata bidhaa, na wanaume wengi wanafanya Biashara hii Ila ikifanywa na mwanamke ni bora zaidi unajua kabisa vitu gani wanawake wanapenda.

6.Insurance, consultancy companies: Kama una elimu, uzoefu na mtaji wa kutosha unaweza kuanzisha kampuni yako ya bima au kotoa ushauri mbalimbali au watu kukupa kazi zao uwafanyie na unaweza kufungua kampuni mbalimbali.

7.Biashara ya chakula, unaweza kuanzisha hotel au kimgahawa na ukapika vyakula, muhimu uweze kuandaa chakula vizuri, na kuandaa mazingira masafi na huduma ziwe nzuri.

8.Biashara ya kuuza maua na miche, hii ni biashara unaweza kuanza bila mtaji au mtaji kidogo sana, kama una maua yakate na uoteshe mengi zaidi katika vifuko, pia miche ya miti au matunda unaweza kuetengeneza kitalu, unaweza kupata maua Kwa watu hata kununua bei sio ghali. Tafuta eneo zuri la kuuzia hata kwako muhimu ni kujitangaza.

9.Biashara ya vinywaji; soma zaidi hapa

10.Biashara ya mapambo ya nyumba

Miradi iko mengi sana na bidii yako ya kufanya utafiti na kujifunza wengine wanafanya nini. Pia kumbuka biashara yoyote mwanamke unaweza kufanya na suala la mtaji sio tatizo sana mikopo ipo mradi utafute yenye masharti nafuu.


Kwa ushauri wa  BIASHARA / UJASIRIAMALI na MAISHA  wasiliana nami WhatsApp 0716924136  /   + 255 755 400 128 /  + 255 688 361 539  /  + 255 629 748 937
KOCHA MWL JAPHET MASATU

Thursday, May 14, 2020

MTAJI NI MDOGO ? --JINSI YA KUKABILIANA NA USHINDANI WA BEI .

Zifuatazo ni hatua za kuchukua ili kukabiliana na ushindani wa bei pale unapofanya biashara kwa mtaji mdogo.
 (01 ). CHEZA  MCHEZO  WAKO  MWENYEWE.
Kama unataka kupata ushindi kwenye eneo lolote la maisha yako, basi unapaswa kucheza mchezo wako mwenyewe. Hii ina maana kwamba unapaswa kutengeneza mchezo wako, kujiwekea sheria zako mwenyewe, kisha kucheza mchezo huo. Ukiingia kucheza mchezo wa wengine, ambao wameutengeneza wao na kuweka sheria zao, huwezi kushinda, maana wao ndiyo wanaoujua mchezo huo kuliko wewe.
Hivyo pia ndivyo ilivyo kwenye biashara, haijalishi unafanya biashara gani, unapaswa kucheza mchezo wako mwenyewe. Hapa unapaswa kupanga ni aina gani ya biashara unaifanya na utaifanya kwa njia zipi. Tengeneza njia zako mwenyewe, ambazo zinatumia uwezo ulio ndani yako na aina ya wateja unaowalenga, kwa kile unachouza. Jiwekee sheria zako mwenyewe na kisha endesha biashara yako kwa sheria hizo.
Chagua kufanya biashara ya tofauti, ambapo sheria yako kuu kwenye ushindani siyo bei, bali utofauti. Usishindane kwa kupunguza bei, bali shindana kwa kutoa kitu ambacho biashara nyingine hazitoi. Kwa maneno mengine, usikazane kuwa bora zaidi ya wengine, bali kazana kuwa tofauti na wengine.
Hakikisha kuna kitu ambacho wateja wanakipata kwenye biashara yako, ambacho hawawezi kukipata kwenye biashara nyingine yoyote. Inaweza kuwa aina ya bidhaa unazouza, inaweza kuwa aina ya huduma wanayoipata. Ni lazima uwe na kitu ambacho wateja wanakipata kwako tu na hawawezi kukipata kwa wafanyabiashara wengine.
Kama kwenye biashara unayoifanya huwezi kutengeneza kitu cha aina hiyo, ushindani wa bei hauwezi kukuacha salama. Usitegemee utoe kile ambacho kinaweza kupatikana kwa wengine, halafu wateja waje kununua kwako kwa bei juu wakati wanaweza kupata kwingine kwa bei ya chini.
Kumbuka ubinafsi ni asili yetu binadamu, huwa tunaangalia maslahi yetu kwanza kabla ya kitu kingine. Hivyo hakikisha kwenye biashara yako kuna kitu unachowapa wateja wako, kinachowanufaisha na hawawezi kukipata sehemu nyingine. Kwa kuwa na kitu hicho, watakuwa tayari kuja kununua kwako kwa bei ya juu kuliko kwenda kwa wengine wanaouza kwa bei ya chini.
 ( 02 ). ANZA  NA  WATEJA  SAHIHI.
Kuna wateja ambao wanachoangalia ni bei tu, na wapo wateja ambao wanachoangalia ni thamani wanayoipata. Ni vigumu sana kumshawishi mteja anayeangalia bei rahisi kuona thamani.
Hivyo kabla hujaweka nguvu zako kwenye ushawishi au mengine yoyote, anza na wateja sahihi. Jua kwanza kinachomsukuma mteja kununua ni bei au thamani.
Kama kinachomsukuma mteja kununua ni bei peke yake, usipoteze hata muda wako, kwa sababu atakwenda kule ambapo anapata kwa bei ya chini. Lakini unapokutana na mteja ambaye anaangalia thamani anayoipata, hapo una nafasi ya kumshawishi kulipa zaidi ili apate thamani zaidi.
Wateja wa thamani siyo wengi, lakini wale wachache unaowapata watakufanya ufurahie kuifanya biashara yako, maana huwa ni waelewa na hawakusumbui sana.
Wateja wa bei rahisi huwa ni wengi, lakini pia ni wasumbufu. Unaweza kuwapunguzia bei na bado wakaona umenufaika zaidi na hivyo kutaka zaidi kutoka kwako.
Kwa biashara unayofanya, chagua aina ya wateja unaotaka kwenda nao, kisha tafuta aina hiyo ya wateja. Wanapokuja wateja wanaoangalia bei tu, waeleze thamani unayotoa na kama bado wanasisitiza kwenye bei, unaweza kuwaelekeza wapi pa kupata kwa bei wanayotaka wao, lakini pia waoneshe nini watakosa kwa kuangalia bei pekee.
 ( 03 ). KUWA  KARIBU   ZAIDI  NA  WATEJA WAKO.
Biashara ndogo huwa zinazishinda biashara kubwa kwenye eneo hili, uwezo wa kuwa karibu na wateja. Biashara kubwa zinahudumia watu wengi, hivyo huwa hazihangaiki na mteja mmoja mmoja, hivyo mteja hawezi kupata upekee kwenye biashara kubwa.
Ila kwenye biashara ndogo, kwa sababu wateja ni wachache, ni rahisi kumpa kila mteja upekee anaostahili. Ni rahisi kumjua kila mteja na matakwa yake, hivyo wajibu ni kumtimizia mteja yale anayotaka kwa namna yake mwenyewe.
Kosa kubwa ambali wafanyabiashara wengi wadogo huwa wanafanya ni kufanya biashara zao ndogo kama vile ni biashara kubwa, kitu ambacho kinawagharimu sana.
Kuwa karibu zaidi na wateja wako, wasiliana nao mara kwa mara, jua matukio mbalimbali kwenye maisha yao, mfano siku zao za kuzaliwa, watu wao wa karibu na kadhalika. Kisha watumie salamu au jumbe mbalimbali katika siku zao hizo muhimu.
Tumia kila fursa kuwapa wateja wako upekee, uwafanye wajisikie vizuri wanapokuja kwenye biashara yako ambapo wanalipa zaidi kuliko wanavyojisikia wanapokwenda kwenye biashara kubwa ambapo wanalipa kidogo.
 ( 04 ).  WAFUATE  WATEJA  KULE  WALIPO.
Njia nyingine ya kuongeza thamani kwa wateja wako ili wawe tayari kulipa zaidi kwako ni kuwafuata kule walipo. Sasa hivi watu hawana muda, hivyo wanapenda sana pale biashara inapowafuata wao kule walipo. Lakini pia uaminifu umekuwa mdogo, hivyo watu wengi huhofia kuagiza vitu ambavyo hawajaviona.
Wewe kwa kuwa na biashara ndogo, una nafasi ya kujenga uaminifu na wateja wako na kisha kuwafanya waweze kuagiza kile unachouza popote walipo na wakapelekewa. Hii inawafanya wateja wawe tayari kulipa zaidi, kwa sababu imewapunguzia usumbufu na upotevu wa muda kutoka walipo na kwenda kutafuta wanachotaka.
Biashara ndogo inaweza kuwafikia wateja kule walipo kwa ufanisi zaidi kuliko biashara kubwa, hivyo tumia vizuri nafasi hiyo.
 ( 05 ) WEKEZA  ZAIDI  KWENYE  BIASHARA  YAKO.
Unapomtaka mteja alipie zaidi kile anachonunua kwako, ambacho anaweza kukipata kwa bei ya chini sehemu nyingine, lazima utengeneze mazingira ambayo yatamfanya mteja aone anastahili kulipa zaidi. Mfano ukinunua soda ya cocacola kwenye duka la mtaani utalipa shilingi mia tano, lakini soda hiyo hiyo ukiinunua hotelini utalipa shilingi elfu mbili. Ukiwa hotelini hutalalamika kwa nini uuziwe soda ya mia tano kwa shilingi elfu mbili, kwa sababu kuna mazingira yanayokufanya uone kulipa elfu mbili ni halali. Unakuwa umekaa eneo zuri na tulivu, unahudumiwa na watu wanaokujali na kadhalika.
Hivyo pia ndivyo unavyopaswa kufanya kwenye biashara yako, fanya uwekezaji unaoipa biashara yako thamani zaidi kuliko washindani wako. Kuna kitu kidogo sana unaweza kukifanya kwenye eneo lako la biashara na likawafanya watu waipe thamani kubwa. Kitu hicho ni mwonekano wa eneo la biashara, linapaswa kuwa safi na lililopangiliwa vizuri. Mtu akifika kwenye eneo hilo anaona utofauti mkubwa, na ndani yake anakuwa tayari kulipa zaidi.
Wewe mwenyewe ni shahidi, huenda umewahi kufika kwenye eneo la biashara, na kwa jinsi lilivyo na mwonekano mzuri, ukajua utatozwa gharama kubwa, lakini ulipotozwa gharama za kawaida ukashangaa. Hiyo ndiyo hali unayopaswa kuileta kwenye biashara yako pia, kufanya uwekezaji unaowaandaa wateja kuwa tayari kulipa zaidi.
Mwonekano na mpangilio wa eneo la biashara, vifaa unavyotumia na huduma unayowapa wateja wako vinapaswa kuwa vya viwango vya juu sana kiasi cha mteja kuona kama anakuibia pale unapomtajia bei. Na kumbuka hapa utakuwa unawalenga wateja sahihi na siyo wale wanaoangalia bei ya chini pekee.
Rafiki, hizo ndizo hatua tano za kuchukua ili kuweza kukabiliana na ushindani wa bei pale unapofanya biashara kwa mtaji kidogo. Kama ulivyoona, kuna mengi ya kufanya kuliko kuingia kwenye ushindani wa moja kwa moja kwenye bei, ambao utakuumiza sana.
Nimalizie kwa kukuambia hili rafiki yangu, kama upo kwenye biashara ambayo kitu pekee unachoweza kujitofautisha nacho ni kupunguza bei, basi upo kwenye biashara ambayo siyo sahihi. Kwa sababu kuna wengine wapo tayari kupunguza bei zaidi yako, na wakiwa na mtaji mkubwa kuliko wewe, watapata faida kwa kuuza kwa wengi zaidi kuliko wewe unayeuza kwa wachache.
Hivyo fanyia kazi haya matano uliyojifunza, na mengine yanayoendana na hayo, lakini siyo kupunguza bei. Na kama biashara haina namna nyingine bali bei basi achana nayo na nenda kwenye biashara sahihi, ambapo unaweza kutengeneza mchezo wako mwenyewe na kuucheza vizuri.

JIUNGE  NA  DARASA  ONLINE  KWA  KULIPIA   ADA  YA  MWEZI , MWAKA---UJIFUNZE KWA  UNDANI  NA  MAPANA--ELIMU  YA  BIASHARA &  UJASIRIAMALI--- NA  UCHUKUE  HATUA --UTAFANIKIWA

SEE  YOU  AT  THE    TOP
Ndimi  rafiki   yako KOCHA /   MWL.  JAPHET   MASATU , BLOGGER
Kwa   maelekezo   zaidi  tuwasiliane  kwa ;--
SIMU / MESEJI / ( WhatsApp  + 255 716 924136 )    /    +255 755 400128  /  + 255 688  361  539 /  + 255 629 748  937

Saturday, April 18, 2020

UJASIRIAMAARIFA , BIDHAA 10 ZA KIDIJITALI UNAZOWEZA KUUZA MTANDAONI NA KUINGIZA KIPATO.

Kuna bidhaa nyingi za kidijitali unazoweza kuuza mtandaoni na ukaingiza kupato kwa muda mrefu. 

1. Vitabu

2. Makala

3. Picha

4. Michoro

5. Muziki

6. Ushauri

7. Kozi

8. Ukocha

9. Blog

10. Matangazo.

Tumia mtandao wa intaneti kwa manufaa, jua jinsi ya kuingiza kipato mtandaoni kwa kutumia blog.

Thursday, April 16, 2020

UJASIRIAMAARIFA , LIPWA KWA MAARIFA NA TAARIFA ULIZONAZO.

Tunaishi kwenye zama za  TAARIFA  na  / MAARIFA ,Hivyo mwenye maarifa na taarifa zenye manufaa makubwa kwa wengine, ndiyo wanaonufaika sana.Na hapo kuna aina mpya ya ujasiriamali ambao unahusisha maarifa, ambao tunauita UJASIRIAMAARIFA.Kupitia ujasiriamali huu, unaweka maarifa na taarifa ulizonazo kwenye kifurushi ambacho wengine wanaweza kununua kama nakala ngumu (HARDCOPY ) au tete.( SOFTCOPY )

Unaweza kujifunza kwa kina kuhusu ujasiriamaarifa katika   Mada  ya  JINSI YA KUTENGENEZA FEDHA MTANDAONI KWA KUTUMIA BLOG.  Una maarifa na taarifa nyingi, anza kuziuza sasa .

 WASILIANA  NA  KOCHA  MWL  JAPHET MASATU AKUTENGEHEZEE  BLOG  YAKO LEO NA  UJUE  JINSI YA  KUFANYA  HIVYO. ----- Call / SMS / WhatsApp / +255 716924136 /  + 255 755 400128  / + 255 688361539

UZALISHAJI NI SANAA--JINASUE KUTOKA KWENYE MAARIFA YA KAWAIDA----NS DR. KZUO INAMORI---- ( PDF )