Wakati wa mlipuko kama huu, hakuna anayejua nini kitatokea kesho, na
kadiri mambo yanavyozidi kuwa mabaya, ndivyo watu wanaendelea kutabiri
kwamba mambo yatakuwa mabaya zaidi.
Watu wanatishana na kupeana wasiwasi mkubwa. Wapo wanaosema huu ndiyo
mwisho wa dunia. Kila mtu ana maoni yake. Lakini tunajua kitu kimoja
kuhusu maoni, siyo ukweli.
Hakuna aliyeweza kutabiri ujio au madhara ya mlipuko huu, na hakuna
anayeweza kutabiri kwa uhakika mambo yataendaje. Tunachojua ni kwamba
tutavuka hili, kama ambavyo jamii ya binadamu imevuka mengi siku za
nyuma.
Hivyo wewe kuwa chanzo cha matumaini sahihi kwa wateja wako. Katika
hali ya wasiwasi kama hii, watu wanapenda kuwasikiliza wale wanaoleta
habari njema, lakini siyo habari njema hewa. Bali habari njema sahihi.
Usiwe mtu wa kutoa habari mbaya kwa wateja wako, utawatisha na
kuwafanya waahirishe kununua. Badala yake kuwa mtu wa kutoa habari
njema, mtu wa kuwapa wateja wako moyo na hapo watajisikia vizuri na
kununua. Ukiweza kuwaonesha jinsi kile unachouza kinawasaidia kupunguza
makali ya mlipuko, wateja wanakujali zaidi.
Mfano; biashara za ushauri na mafunzo zinapaswa kuwa
chanzo cha matumaini kwa wateja wake. Kwa kuwaonesha kwamba hili
linaloendelea siyo mwisho wa dunia na mambo yatakwenda vizuri baada ya
hili.
BADILI FIKRA.FIKIRI TOFAUTI .BADILI MAISHA.JITAMBUE .JIFUNZE ELIMU YA SAIKOLOJIA,TEOLOJIA , FEDHA ,UTAMBUZI(SELF HELP EDUCATION),FALSAFA YA MAISHA,MAISHA NA MAFANIKIO,BIASHARA / UJASIRIAMALI.FURAHIA WASAA WAKO NA MAISHA NA MAFANIKIO BLOGU.THIS IS THE COMMUNITY CAPACITY BUILDING BLOG.ENJOY THE BLOG.STRETCH YOUR MIND. YOU CAN CHANGE YOUR LIFE FOR EVER. YOU CAN ACHIEVE EXCELLENCE.YOU CAN MAKE A DIFFERENCE.
Saturday, April 4, 2020
MFANYA BIASHARA / MJASIRIAMALI : JUA THAMANI NA WAELEZE WATEJA WAKO
BIASHARA pekee zitakazovuka kipindi hiki cha Mlipuko wa ugonjwa wa CORONA salama ni
zile ambazo zinatoa thamani kubwa kwa wateja wake na jamii kwa ujumla.
Zile biashara ambazo watu hawawezi kuishi bila ya kuwa na kile
kinachouzwa.
Hivyo huu ni wakati wa wewe kukaa chini na kujiuliza ni thamani gani unayoitoa kwa wateja wako. Huenda umezoea kuuza na kupokea fedha na umesahau thamani ipi unatoa.
Jiulize ni tatizo au hitaji gani la wateja ambalo biashara yako inatoa. Kisha waeleze wateja thamani hiyo vizuri, waoneshe jinsi ambavyo wanaihitaji thamani hii wakati huu wa mlipuko.
Mfano; biashara za huduma za kifedha zinatumia nafasi hii kuonesha jinsi ilivyo salama kutuma na kupokea fedha kwa mtandao na siyo fedha taslimu. Hii ni thamani kubwa ambayo mteja au mfanyabiashara hakuwa anaiona, lakini kwa sasa iko wazi.
Hivyo huu ni wakati wa wewe kukaa chini na kujiuliza ni thamani gani unayoitoa kwa wateja wako. Huenda umezoea kuuza na kupokea fedha na umesahau thamani ipi unatoa.
Jiulize ni tatizo au hitaji gani la wateja ambalo biashara yako inatoa. Kisha waeleze wateja thamani hiyo vizuri, waoneshe jinsi ambavyo wanaihitaji thamani hii wakati huu wa mlipuko.
Mfano; biashara za huduma za kifedha zinatumia nafasi hii kuonesha jinsi ilivyo salama kutuma na kupokea fedha kwa mtandao na siyo fedha taslimu. Hii ni thamani kubwa ambayo mteja au mfanyabiashara hakuwa anaiona, lakini kwa sasa iko wazi.
Tuesday, March 31, 2020
Subscribe to:
Posts (Atom)