Monday, December 30, 2019

TOFAUTI KATI YA TAJIRI NA MASIKINI KATIKA KUJIFUNZA NA KUKUA...

MATAJIRI huwa wanajifunza kila siku na kuendelea kukua zaidi. Wanajisomea vitabu na kutafuta maarifa mbalimbali yanayowawezesha kupiga hatua. Wanaamini kuna mengi hawajui hivyo kujifunza zaidi, na hilo linawafanya wafanikiwe.
 
MASIKINI wao hawana muda wa kujifunza, wanaamini tayari wanajua kila kitu. Hawasomi vitabu ila habari za udaku na mitandao ya kijamii ndivyo wanapenda kufuatilia. Kwa njia hii wamekuwa hawajifunzi na hivyo kubaki kwenye umasikini wao.

Wednesday, December 25, 2019

TOFAUTI YA TAJIRI NA MASKINI KATIKA KUDHIBITI FEDHA.


MATAJIRI  wana uwezo wa kudhibiti fedha zao na hivyo kuweza kupiga hatua zaidi. Hawana ulimbukeni kwenye fedha, hawabadili maisha yao kwa sababu wamepata fedha zaidi. Na pale wanapopata fedha zaidi, wanaiwekeza. 

MASKINI  hawawezi kudhibiti fedha zao, wana ulimbukeni mkubwa kwenye fedha. Wakipata fedha zaidi wanabadilika, wanaanza kununua vitu visivyo muhimu mpaka fedha hiyo iishe. Kwa namna hii, wanashindwa kupiga hatua na kila wanapopata fedha zaidi, ndiyo wanapotea zaidi.
Acha ulimbukeni kwenye fedha, jifunze jinsi ya kudhibiti fedha zinazokuja kwako ili uweze kuzitumia kupiga hatua zaidi.