Mipango ni rahisi sana, kila mtu anapanga na msimamishe mtu yeyote
njiani na muulize mipango yake ni ipi, atakupa mipango mizuri sana.
Pamoja na kila mtu kuwa na mipango mizuri, ni wachache sana ambao
wanaweza kufanyia kazi mipango hiyo na ikawa uhalisia kwenye maisha yao.
Wengi wamekuwa wanabaki na mipango tu, lakini haiwi uhalisia.
Kinachowazuia wengi kutekeleza mipango waliyonayo ni tabia ya
kuahirisha mambo. Hii ni tabia ambayo ni asili yetu sisi binadamu, huwa
hatupendi kufanya chochote ambacho kinatuumiza au kinataka tuweke kazi.
Huwa tunapenda kutumia muda wetu kwa vitu visivyo na maana. Kwa muda
ule ule na kwa nguvu zile zile, huwa tunaona ni bora kutumia kufanya
vitu ambavyo vitatupa raha ya muda mfupi, kuliko kufanya vitu ambavyo
havina raha ya muda mfupi lakini kwa muda mrefu vina maana.
Kinachowatofautisha wale wanaopata mafanikio makubwa kwenye maisha
yao na wale wanaoshindwa siyo bahati wala akili wala fursa.
Kinachowatofautisha ni namba wanavyoweza kuishinda tabia ya kuahirisha
mambo.
Wanaofanikiwa na wanaoshindwa wote wanakuwa kwenye mazingira
sana, wanakutana na fursa sawa, lakini wale wanaoshindwa huwa wanasubiri
wakati wanaofanikiwa wanachukua hatua.
BADILI FIKRA.FIKIRI TOFAUTI .BADILI MAISHA.JITAMBUE .JIFUNZE ELIMU YA SAIKOLOJIA,TEOLOJIA , FEDHA ,UTAMBUZI(SELF HELP EDUCATION),FALSAFA YA MAISHA,MAISHA NA MAFANIKIO,BIASHARA / UJASIRIAMALI.FURAHIA WASAA WAKO NA MAISHA NA MAFANIKIO BLOGU.THIS IS THE COMMUNITY CAPACITY BUILDING BLOG.ENJOY THE BLOG.STRETCH YOUR MIND. YOU CAN CHANGE YOUR LIFE FOR EVER. YOU CAN ACHIEVE EXCELLENCE.YOU CAN MAKE A DIFFERENCE. JIFUNZE ---ELIMIKA --CHUKUA HATUA---FANIKIWA
Friday, November 30, 2018
FANYA BIASHARA HIZI UTAPIGA PESA SANA. UTAFANIKIWA SANA.
1.
USAFIRI.
Moja ya biashara ambayo inaaminika hasa kwa bara la afrika ikiwa utaifanya kwa utulivu na ukafata misingi yake ni biashara ya usafiri. Hapa unaweza ukawa na kampuni yako ya kusafirishia abiria kutoka sehemu moja na kwenda nyingine.
Kwa sasa hitaji la usafiri bado ni kubwa, kama si mjini hata kijijini. Watu wanataka kusafiri kila siku na kwa bahati mbaya wengi hawana uwezo huo wa kumiliki vyombo vya usafiri. Hii ni mojawapo ya biashara ya kuifikiria kuifanya kama unaweza, kwani itakupa mafanikio sana.
2. AFYA.
Kama pia utajikita na kufanya biashara inayohususha mambo ya afya, basi upo uwezekano mkubwa zaidi wa wewe kufanikiwa sana. Huduma za afya katika maeneo mengi bado hazijafikiwa kisawasawa na zinahitajika kweli.
Hivyo kwa kufanya biashara hii, kama ukifungua hospitali au zahati au duka la dawa, utapata pesa na hapo pia utakuwa imeisaidia jamii. Kikubwa kubali kuzunguka kuangalia ni wapi ambapo ukifanya huduma au biashara hii wewe itakulipa.
3. CHAKULA.
Hakuna mtu asiyekula, hiyo ikiwa na maana ukianzisha biashara ya vyakula na ukaifanya kwa ufanisi mkubwa utafanikiwa. Hapa unaweza ukauza chakula, lakini si maanishi uje na picha ile ya mama ntilie ‘pasee.’
Ukiamua kuja na biashara ya kuuza chakula ifanye kwa ukisasa zaidi. Zipo sehemu bado nyingi zinazohitaji huduma hii ya chakula safi, mazingira safi, lakini hawaipati kwa uhakika kwahiyo unatakiwa ujue jinsi ya kuanza ili uanze kupiga pesa.
4. VIWANDA VIDOGO VIDOGO.
Huwezi kuendelelea sana kama utaendelea kuwa mlanguzi wa biashara za watu wengine. Changamsha akili na anza mchakato wa kuweka viwanda vidogo vidogo ambavyo vitasaidia wewe kuweza kukupa kipato kikubwa.
Uzuri wakuwa na kiwanda kidogo wewe ndio unakuwa mzalishaji wa kwanza kwa hiyo ni lazima utapata faida kubwa sana. Hapa unaweza ukatengeneza kiwanda chako cha kutengeneza juisi au unga wa sembe na lishe, uamuzi ni wako.
Moja ya biashara ambayo inaaminika hasa kwa bara la afrika ikiwa utaifanya kwa utulivu na ukafata misingi yake ni biashara ya usafiri. Hapa unaweza ukawa na kampuni yako ya kusafirishia abiria kutoka sehemu moja na kwenda nyingine.
Kwa sasa hitaji la usafiri bado ni kubwa, kama si mjini hata kijijini. Watu wanataka kusafiri kila siku na kwa bahati mbaya wengi hawana uwezo huo wa kumiliki vyombo vya usafiri. Hii ni mojawapo ya biashara ya kuifikiria kuifanya kama unaweza, kwani itakupa mafanikio sana.
2. AFYA.
Kama pia utajikita na kufanya biashara inayohususha mambo ya afya, basi upo uwezekano mkubwa zaidi wa wewe kufanikiwa sana. Huduma za afya katika maeneo mengi bado hazijafikiwa kisawasawa na zinahitajika kweli.
Hivyo kwa kufanya biashara hii, kama ukifungua hospitali au zahati au duka la dawa, utapata pesa na hapo pia utakuwa imeisaidia jamii. Kikubwa kubali kuzunguka kuangalia ni wapi ambapo ukifanya huduma au biashara hii wewe itakulipa.
3. CHAKULA.
Hakuna mtu asiyekula, hiyo ikiwa na maana ukianzisha biashara ya vyakula na ukaifanya kwa ufanisi mkubwa utafanikiwa. Hapa unaweza ukauza chakula, lakini si maanishi uje na picha ile ya mama ntilie ‘pasee.’
Ukiamua kuja na biashara ya kuuza chakula ifanye kwa ukisasa zaidi. Zipo sehemu bado nyingi zinazohitaji huduma hii ya chakula safi, mazingira safi, lakini hawaipati kwa uhakika kwahiyo unatakiwa ujue jinsi ya kuanza ili uanze kupiga pesa.
4. VIWANDA VIDOGO VIDOGO.
Huwezi kuendelelea sana kama utaendelea kuwa mlanguzi wa biashara za watu wengine. Changamsha akili na anza mchakato wa kuweka viwanda vidogo vidogo ambavyo vitasaidia wewe kuweza kukupa kipato kikubwa.
Uzuri wakuwa na kiwanda kidogo wewe ndio unakuwa mzalishaji wa kwanza kwa hiyo ni lazima utapata faida kubwa sana. Hapa unaweza ukatengeneza kiwanda chako cha kutengeneza juisi au unga wa sembe na lishe, uamuzi ni wako.
Thursday, November 22, 2018
KILA MTU NA HAMSINI ZAKE. HAKUNA ANAYEJALI SANA MAISHA YA WENGINE.
Maisha
ya sasa hivi naweza kusema yamekuwa ni kama ya kuishi kisiwani, watu wamekuwa
hawajali sana watu wengine kwa kiasi kikubwa, ukilinganisha na zamani. Kwa sasa
ukipata changamoto kubwa wewe jua hiyo ni changamoto yako tu, inabidi ukomae
nayo hadi utoke.
Kutokana na hili kuendelea kudumu kunafanya maisha yanazidi kuendelea kuwa magumu sana hadi watu wanakosa msaada ambao ungeweza kuwasaidia. Ubinafsi ambao wengi wanao imekuwa ni kichocheo kikubwa sana cha ugumu wa maisha.
Kutokana na hili kuendelea kudumu kunafanya maisha yanazidi kuendelea kuwa magumu sana hadi watu wanakosa msaada ambao ungeweza kuwasaidia. Ubinafsi ambao wengi wanao imekuwa ni kichocheo kikubwa sana cha ugumu wa maisha.
KUTEGEMEA CHANZO KIMOJA CHA MAPATO , HUPELEKEA MAISHA KUWA MAGUMU SANA !
Kutokana
na maisha kubadilika na gharama za maisha kupanda karibu kila siku, suala la kutegemea
kipato kimoja, ni moja ya chanzo cha maisha kuwa magumu. Watu wengi wanategemea
kipato kimoja, zaidi kwa wengi ikiwa ni ajira.
Kwa bahati mbaya kipato kimoja hakiwezi kukidhi mahitaji yote hata iweje. Sasa kwa sababu hiyo ya maisha kupanda mara kwa mara, ni lazima tu ugumu wa maisha uonekane. Hata siku moja usitegemee maisha yako yakawa rahisi kama bado una kipato kimoja.
Kwa bahati mbaya kipato kimoja hakiwezi kukidhi mahitaji yote hata iweje. Sasa kwa sababu hiyo ya maisha kupanda mara kwa mara, ni lazima tu ugumu wa maisha uonekane. Hata siku moja usitegemee maisha yako yakawa rahisi kama bado una kipato kimoja.
Saturday, November 17, 2018
TABIA YA FEDHA. FEDHA NI ZAO LA HAMASA.
FEDHA ni kama
mchumba mwenye wivu, mchumba ambaye anataka muda wote uwe naye, muda
wote umfikirie yeye tu. Na mchumba huyu akigundua humfikirii na kumjali
yeye anaondoka na kwenda kutafuta wengine wanaomjali na kumfikiria.
Hivi ndivyo fedha zilivyo, kama huna muda nazo hazitakuwa na muda na wewe. kama huzijali na kuzifikiria muda wote zitaenda kwa wale wanaojali na kuzifikiria.
Fedha ni zao la hamasa, chochote ambacho kinakuhamasisha, kile unachopenda kweli, kila ambacho unakifanya muda wote bila ya kuchoka, ndiyo kitu kitakachokuletea kipato kikubwa sana.
Hivyo rafiki, unapofikiria kuhusu fedha, anza kufikiria nini kinakupa hamasa sana, nini unapenda kufanya sasa kisha weka maisha yako yote kwenye kufanya hicho, na fedha hazitakuwa tatizo kubwa kwako.
Tatizo kubwa kwenye hili ni watu huwa wanakosa uvumilivu, wakiona kile wanachofanya kinachelewa kuwaletea matokeo wanayopata, na kuona wengine wakifurahia matunda ya vile wanavyofanya, wanajidanganya kule ndiyo kwenye fedha, wanaacha wanachofanya na kwenda kufanya vitu vingine. Wanahangaika sana, na hawapati fedha walizofikiria kupata. Na hata wakizipata, bado maisha yao yanakuwa na utupu fulani, kwa sababu kile wanachofanya siyo kinachowahamasisha zaidi.
Hivi ndivyo fedha zilivyo, kama huna muda nazo hazitakuwa na muda na wewe. kama huzijali na kuzifikiria muda wote zitaenda kwa wale wanaojali na kuzifikiria.
Fedha ni zao la hamasa, chochote ambacho kinakuhamasisha, kile unachopenda kweli, kila ambacho unakifanya muda wote bila ya kuchoka, ndiyo kitu kitakachokuletea kipato kikubwa sana.
Hivyo rafiki, unapofikiria kuhusu fedha, anza kufikiria nini kinakupa hamasa sana, nini unapenda kufanya sasa kisha weka maisha yako yote kwenye kufanya hicho, na fedha hazitakuwa tatizo kubwa kwako.
Tatizo kubwa kwenye hili ni watu huwa wanakosa uvumilivu, wakiona kile wanachofanya kinachelewa kuwaletea matokeo wanayopata, na kuona wengine wakifurahia matunda ya vile wanavyofanya, wanajidanganya kule ndiyo kwenye fedha, wanaacha wanachofanya na kwenda kufanya vitu vingine. Wanahangaika sana, na hawapati fedha walizofikiria kupata. Na hata wakizipata, bado maisha yao yanakuwa na utupu fulani, kwa sababu kile wanachofanya siyo kinachowahamasisha zaidi.
Friday, November 16, 2018
HUDHURIA SEMINA AU WARSHA MBALIMBALI ZA KIBIASHARA UJIFUNZE MBINU MPYA ZA KIMAUZO. DUNIA INABADILIKA KILA SIKU. ACHANA NA MBINU ZA KIZAMANI ZA KIMAUZO.
Inapotokea mbinu zako za kimauzo zimepitwa na wakati huwezi kuendelea
kuwapata wateja wengi. Hapa ndipo maana kampuni kubwa zikaja na kitengo
cha huduma kwa wateja ili kila siku kuweza kumudu kuboresha huduma ili
kuleta mafanikio. Kama kila wakati utaendelea kuwa na mbinu zile zile za kimauzo pasipo kuzibadilisha na kutegemea
muujiza utakaokupa wateja wengi, naomba nikwambie kwenye hilo jambo
lisahau kabisa. Ni muhimu ukabadilika kwanza wewe na wasaidizi wako.
NINI UFANYE ???
Kila mara pata mafunzo ya jinsi ya kuboresha huduma kwa wateja na unaweza kuyapata kupitia semina au warsha mbalimbali za kibiashara. Pia jenga urafiki na wateja ili wakusaidie kupata wateja wengine zaidi na zaidi ili kufikia mafanikio.
Ndimi Mwl Japhet Masatu, Dar es salaam , Tanzania, Afrika Ya Mashariki.
EMAIL: japhetmasatu@gmail.com
Call: + 255 716 924136 ( WhatsApp ) , + 255 755 400128
Kila mara pata mafunzo ya jinsi ya kuboresha huduma kwa wateja na unaweza kuyapata kupitia semina au warsha mbalimbali za kibiashara. Pia jenga urafiki na wateja ili wakusaidie kupata wateja wengine zaidi na zaidi ili kufikia mafanikio.
Ndimi Mwl Japhet Masatu, Dar es salaam , Tanzania, Afrika Ya Mashariki.
EMAIL: japhetmasatu@gmail.com
Call: + 255 716 924136 ( WhatsApp ) , + 255 755 400128
HUDUMA MBOVU, HUPOTEZA SANA WATEJA.
Huwezi
kukwepa kukosa wateja kama una huduma mbovu kwa wateja wako. Unaweza usiwe
wewe, hapa wanaweza wakawa ni wasaidizi au wafanyakazi wako ndio wanaokuharibia pasipo wewe kujua kitu
chochote na ukaona uko sawa.
Wengi kwa kushindwa kujua kwamba wanahuduma mbovu ndio wanajikuta ni chanzo cha kuanza kupoteza wateja wengi tena bila kujua. Huduma yako mbovu inaweza ikawa kwenye bidhaa au mazingira au hata jinsi ya kuwahudumia wateja na wakaridhika.
NINI UFANYE ?
Hapa kuwa makini sana na mazingira yote yanayoweza kupelekea huduma mbovu ikatolewa, kama wafanyakzi wako, mazingira na bidhaa unazozitoa. Vitu hivyo unatakiwa kuvihakiki mara kwa mara ili visiwe chanzo cha huduma ya hovyo kwako na kupelekea kukosa wateja.
Na Mwl Japhet Masatu , Dar es salaam , Tanzania, Afrika Ya Mashariki
+255 716 924136 ( WhatsApp ) , +255 755 400128
EMAIL: japhetmasatu@gmail.com
Wengi kwa kushindwa kujua kwamba wanahuduma mbovu ndio wanajikuta ni chanzo cha kuanza kupoteza wateja wengi tena bila kujua. Huduma yako mbovu inaweza ikawa kwenye bidhaa au mazingira au hata jinsi ya kuwahudumia wateja na wakaridhika.
NINI UFANYE ?
Hapa kuwa makini sana na mazingira yote yanayoweza kupelekea huduma mbovu ikatolewa, kama wafanyakzi wako, mazingira na bidhaa unazozitoa. Vitu hivyo unatakiwa kuvihakiki mara kwa mara ili visiwe chanzo cha huduma ya hovyo kwako na kupelekea kukosa wateja.
Na Mwl Japhet Masatu , Dar es salaam , Tanzania, Afrika Ya Mashariki
+255 716 924136 ( WhatsApp ) , +255 755 400128
EMAIL: japhetmasatu@gmail.com
Subscribe to:
Posts (Atom)