Kaka, dada, hebu tuambiane ukweli…
Umechoka kuishi kwa mlo mmoja?
Au kila mwisho wa mwezi ni stress tupu?
Mishahara inapita kama upepo.
Biashara haieleweki.
Kuna hela, lakini haikai.
Unafanya kazi kama punda, lakini mfuko ni kama gunia la mbolea mashimo kila kona.
Unajituma, lakini mafanikio yako kama ndoto ya mchana.
Kaka, hiyo siyo laana.
Ni mfumo mbovu wa maisha.
Ni kukosa maarifa sahihi.
Tazama wenzako wanaoanza na elfu moja,
Leo wanamiliki vibanda, magari, hadi mashamba.
Wewe bado unatafuta mtu wa kukukopesha buku la kula.
Ni aibu.
Lakini sio kosa lako kabisa.
Ni kwamba wakati unakuwa uliaminishwa kuwa*Ukiwa na hela nyingi, ndo unaweza kuwekeza.*
Na Wewe Ukaamini.
Ulimwengu unabadilika, lakini mtazamo wako umebaki kuwa ule wa miaka ya 70.
Upo kwenye mduara wa mateso pesa inaingia na kutoka bila faida.
Kila mwezi ni kama kuanza maisha upya.
Mpaka lini?
Watu wengi hudhani kwamba ili uanze kujenga utajiri, lazima uwe na mamilioni.
Hapo ndo tunakosea.
Ukweli ni huu:
Hela kidogo ndiyo mwanzo wa hela nyingi.
Tatizo si kwamba huna pesa.
Tatizo ni kwamba hujui namna ya kukitumia kile kidogo ulichonacho.
Huna mfumo.
Huna maarifa.
Unakula mtaji, unaua ndoto zako.
Usingoje mshahara mwingine ukufikishe kwenye msongo tena.
Usingoje upate milioni ndo uanze.
Anza na hiyo buku YAANI TSHS 1000
Buku yako ya leo inaweza kuwa sababu ya uhuru wako wa kesho.
ENDELEA KUSOMA KILA SIKU " MAISHA NA MAFANIKIO BLOG " UTAJIFUNZA MENGI NA SIRI NYINGI ZA MAISHA NA MENGINEYO DUNIANI --- ONGEA NA KOCHA MWL. JAPHET MASATU-----CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136