Wednesday, April 15, 2020

JINSI YA KULIPWA UKIWA NYUMBANI----ONGEA NA KOCHA / COACH MWL JAPHET MASATU

Watu wengi wamezoea biashara ni mpaka utoke nyumbani na kwenda kwenye ofisi au eneo jingine la biashara na ukutane na wateja.

Lakini mapinduzi ya kiteknolojia yameshabadili hilo.
Sasa unaweza kufanya biashara na kulipwa ukiwa nyumbani kwako, bila hata ya kukutana na wateja.
Hii ni kupitia mtandao wa intaneti.
Hatua ya kwanza ya kulipwa mtandaoni, ni kuwa na blog.
Blog ndiyo inakuwa duka lako la mtandaoni, ambapo wale wenye uhitaji wa unachotoa watakuja na kukutana na wewe.
Baada ya hapo, kuna namna ya kuwapa thamani zaidi na wao wakakulipa.

 HUHITAJI   MTAJI  ILI  KUANZA .
Uzuri ni kwamba, kuigiza kipato mtandaoni kwa kutumia blog huhitaji kuwa na mtaji wowote wa kuanzia, kama unaweza kusoma hapa, basi kifaa hicho hicho unachotumia kusoma ndiyo unaweza kukitumia kuendesha blog yao.
Kama unatumia kompyuta hiyo hiyo inakutosha kufanya biashara hii. Na hata kama unatumia simu pekee, inakutosha sana kuweza kufanya biashara hii.
Unachohitaji kuwa nacho ni kitu kinachoongeza thamani kwenye maisha ya wengine na utayari wa kutoa thamani hiyo halafu kuwa na njia bora ya kulipwa na baada ya hapo kuweka kazi hasa.

JE , WAHITAJI   KUWA   NA   BLOG    YAKO  ???  WASILIANA  NA   KOCHA   MWL  JAPHET  MASATU   ------ 0716 924136 /   0755 400128 / 0688  361 539

Monday, April 13, 2020

FURSA 35 ZA BIASHARA KATIKA SEKTA YA UTUNZAJI WA MAZINGIRA ------FURSA AFRIKA MASHARIKI BLOG

VIPAUMBELE VYAKO NI VIPI ? KAMA UNATAKA KITU KIFANYIKE , MPE MTU ALIYE BIZE

Huwa tunajidanganya kwamba hatuna muda wa kufanya vitu kwa sababu tupo bize.

Ila ukweli ni kwamba, kama kuna kitu unataka kufanya, basi utakifanya vizuri ukiwa bize kuliko ukiwa hauko bize.
Angalia, kipindi kama hiki ambapo watu wengi hawana kazi nyingi za kufanya, ungetegemea uwe ndiyo watu wangeutumia muda huu vizuri kusoma na kujifunza.


Lakini waangalie watu wanafanya nini, kufuatilia habari na mitandao siku nzima.


Hali hii inasababishwa na kukosa vipaumbele.
Unapokuwa bize unajiwekea vipaumbele na kukazana kuvifikia.
Lakini unapokuwa haupo bize, unakosa vipaumbele, hivyo hata kitu kidogo kinakushinda kufanya.