BADILI FIKRA.FIKIRI TOFAUTI .BADILI MAISHA.JITAMBUE .JIFUNZE ELIMU YA SAIKOLOJIA,TEOLOJIA , FEDHA ,UTAMBUZI(SELF HELP EDUCATION),FALSAFA YA MAISHA,MAISHA NA MAFANIKIO,BIASHARA / UJASIRIAMALI.FURAHIA WASAA WAKO NA MAISHA NA MAFANIKIO BLOGU.THIS IS THE COMMUNITY CAPACITY BUILDING BLOG.ENJOY THE BLOG.STRETCH YOUR MIND. YOU CAN CHANGE YOUR LIFE FOR EVER. YOU CAN ACHIEVE EXCELLENCE.YOU CAN MAKE A DIFFERENCE. JIFUNZE ---ELIMIKA --CHUKUA HATUA---FANIKIWA
Saturday, August 31, 2019
Friday, August 30, 2019
Saturday, August 24, 2019
Sunday, August 18, 2019
HAKUNA ANAYEKOSEA KWA MAKUSUDI.
Upo
msingi wa ustoa ambao utakuwezesha kuishi maisha yako kwa utulivu bila
ya kujali wengine wanasema au kufanya nini. Moja ya vitu ambavyo
vinatusumbua sana zama hizi ni mambo ambayo wengine wanasema au
wanafanya. Huwa tunayaruhusu yatuumize, tukiamini kwamba watu hao
wanafanya mambo hayo kwa makusudi ili kutuumiza.
Lakini
wastoa wanatuambia kwamba, watu wanaofanya mambo ambayo yanatuumiza,
hawafanyi hivyo kwa makusudi, bali wanafanya hivyo kwa sababu hawajui
kulicho sahihi kufanya. Hivyo hupaswi kuumia kwa sababu yao, badala yake
unapaswa kuwaonea huruma na kuona kama kuna namna unaweza kumsaidia ili
asiendelee kukosea.
Mfano
mzuri ni pale mtoto mdogo anapokupiga kofi, je utarejesha kwa kumpiga
kofi pia? Je utakasirika? Je utamnunia? Je utasema amekudharau? Majibu
hapo ni hapana. Lakini vipi mtu mzima mwenzako akikupiga kofi? Hapo
mambo yanabadilika, unaona amekudharau, utataka kulipiza, utakasirika na
hata kumnunia. Lakini kama utachukulia mtu huyo amekupiga kofi kwa
kutokujua au kwa bahati mbaya, hutapata hisia hizo.
Hivyo
cha kujifunza hapa, tusikimbilie kuhukumu pale watu wanapofanya vitu
kwamba ni vibaya au wamedhamiria kutuumiza. Badala yake tuchukulie
kwamba watu hao hawajui wanachofanya au wamefanya kwa bahati mbaya, na
hilo litatuzuia sisi kuumia.
Mfano
mzuri ni kwenye wizi au utapeli, mtu akikuibia, badala ya kuumia,
unapaswa kumwonea huruma, kwa sababu kwanza hajui njia sahihi ya
kutengeneza kipato ambayo itampa maisha ya utulivu na pili, kwa tabia
yake hiyo, ataishia jela au kaburini, maana ataiba akamatwe na wananchi
wenye hasira kali hadi kufa, au apelekwe polisi na baadaye kufungwa.
Unaona jinsi ambavyo unaondoka kwenye upande wa lawama na kuwa upande wa
utulivu!
CHAGUA SHUJAA WA MAISHA YAKO.
Wastoa
wamekuwa wanaelewa umuhimu wa kuwa na mashujaa, watu ambao tunayapima
maisha yetu kupitia wao. Lakini hili ni eneo ambalo limekuwa na
changamoto kubwa sana zama hizi, kwa sababu kumekuwa na mashujaa wengi
feki. Siku hizi watu wanaoweza kutengeneza umaarufu rahisi kupitia
mitandao ya kijamii, sanaa, michezo au siasa ndiyo wanaonekana mashujaa
kwa wengi. Na wengi wanawafuata watu hao, lakini hakuna wanachojifunza
kwa sababu mwisho wa siku umaarufu wa watu hao huanguka, kwa sababu
haujajengwa kwenye misingi sahihi.
Ni
muhimu uchague mashujaa sahihi wa maisha yako, kutokana na misingi
wanayoiishi au waliyoiishi ambayo unaweza kujijengea kwenye maisha yako
na ukaweza kupiga hatua pia. Kadiri unavyojifunza falsafa hii na
kujifunza wengine walioiishi falsafa hii, utavutiwa na maisha ya baadhi
ya wanafalsafa na kuwachagua kuwa mashujaa wako.
Subscribe to:
Comments (Atom)