Sunday, January 6, 2019

CHUKUA HATUA ZENYE UFANISI ILI KUVUTIA UTAJIRI.

Kama pale ulipo sasa hapakuridhishi, kama unataka kupiga hatua zaidi kwenye maisha yako na kwa kile unachofanya, unapaswa kukua zaidi ya pale ulipo sasa. Unapaswa kuijaza ile sehemu uliyopo sasa kiasi kwamba hakuna tena nafasi kwa ajili yako na hivyo inakubidi ukue zaidi.
 
Chochote unachofanya sasa kifanye kwa viwango vya juu sana kuliko ilivyozoeleka. Na unapofanya kwa viwango vya juu, mfumo wa fikra unaoendesha dunia utakupeleka kwenye hatua za juu kuliko hapo ulipo sasa.
 
Kila siku fanya kile unachopaswa kufanya bila ya kuahirisha, na kifanye kwa ufanisi mzuri. Usifanye kitu chochote kwa haraka au njia ya mkato. Mafanikio kwenye maisha ni kufanya vitu kwa ufanisi wa hali ya juu.
 
Kwa kila hatua unayochukua, kuwa na picha ya matokeo unayotaka kupata na fikiria picha hiyo mara zote. Hili litaweka fikra zako kwenye kile unachofanya na utaweza kupata matokeo bora.

INGIA KWENYE BIASHARA SAHIHI KWAKO ILI KUVUTIA UTAJIRI.

Biashara au kazi yoyote inayo uwezo wa kutengeneza utajiri mkubwa kwa mtu yeyote. Lakini siyo kila aina ya biashara au kazi itaweza kutengeneza utajiri kwako.
 
Utapata utajiri na kufanikiwa kwa kuingia kwenye kazi au biashara ambayo inaendana na wewe. Biashara ambayo inatumia vipaji na uwezo mkubwa uliopo ndani yako.
 
Utafanikiwa zaidi kwa kufanya kile unachopenda na unachojali, kwa sababu utafanya kwa kupenda na siyo kufanya kama kazi.
 
Jua kipi unapenda na kujali na jua vipaji na uwezo mkubwa uliopo ndani yako kisha chagua kazi au biashara inayoendana na vitu hivyo. Hii ndiyo itakayokuletea utajiri mkubwa.

MWONEKANO WA UKUAJI KATIKA KUVUTIA UTAJIRI.

 
Kwa kazi au biashara unayoifanya, usifanye kwa mazoea au kufanya vile vile kila wakati. Badala yake fanya kwa ukuaji kila siku. Kila siku kazana kupiga hatua kubwa zaidi ya ulizopiga siku zilizopita.
 
Ni mwonekano huu wa ukuaji ndiyo unaowavutia watu kwako. Watu wanapenda kujihusisha na wale ambao wanakua zaidi, wanatoa thamani kubwa zaidi kila siku.
 
Mazoea yanaharibu na kuua kabisa kile ambacho kipo ndani ya mtu. Lakini ukuaji unakuza zaidi kile ambacho kipo ndani ya mtu.

UKUAJI BINAFSI KATIKA KUVUTIA UTAJIRI.

 
Ili kuvutia utajiri kupitia kile unachofanya na ili kuziona fursa mpya kila mara, lazima wewe binafsi uwe unakua. Kwa chochote unachofanya sasa, hata kama ni kidogo kiasi gani, unapaswa kukua zaidi ya kitu hicho.
 
Hata kama upo kwenye kazi au biashara ambayo ni ndogo, ifanye kama kubwa na tekeleza majukumu yako kwa ukubwa. Tekeleza majukumu yako kwa ufanisi wa hali ya juu na wahudumie watu kwa namna ambayo inaongeza thamani kubwa kwao.

SAYANSI / KANUNI YA KUPATA UTAJIRI


1. Kuna mfumo wa kufikiri ambao kutoka ndani yake vitu vyote vinatengenezwa na ambao kwa uhalisia wake unaruhusu, kupenyeza na kuujaza ulimwengu wote.
 
2. Fikra kwenye mfumo huu inazalisha ile taswira inayotengenezwa na fikra.
 
3. Mtu anaweza kutengeneza vitu kwenye fikra zake na kwa kuziweka kwenye mfumo huu wa kufikiri kile anachofikiri kinaumbwa.
 
4. Ili kufanya hivi, mtu anapaswa kuondoka kwenye fikra za ushindani na kwenda kwenye fikra za ubunifu. Vinginevyo hataweza kuendana na mfumo wa fikra ambao mara zote upo kwenye hali ya ubunifu na siyo ushindani.
 
5. Mtu yeyote anaweza kuendana na mfumo huu wa fikra kwa kuwa mtu wa shukrani kwa baraka ambazo amezipata. Shukrani inaunganisha fikra za mtu na mfumo wa fikra unaoendesha ulimwengu.
 
6. Mtu lazima atengeneze picha ya kifikra ya vitu anataka kuwa navyo na kuifikiria picha hii mara zote huku akiwa na imani kwamba ataipata na kushukuru kwamba mfumo wa fikra unamwandalia mazingira ya kupata kile anachotaka. Tumia muda wako wa mapumziko kufikiria picha ya utajiri unaotaka kuwa nao na mfumo wa fikra utaipanga dunia kwa namna ambayo itakuletea kile unachotaka.
 
7. Mfumo wa kufikiri unafanya kazi kupitia njia za asili za ukuaji na za kijamii. Kila ambacho kinafikiriwa kwa muda mrefu kwa imani na bila ya shaka, ndiyo kinacholetwa kwenye uhalisia.
 
8. Ili kupokea kile ambacho mtu anataka, lazima mtu achukue hatua kwa namna fulani ambayo inamwezesha kujaza pale alipo sasa. Lazima afanye zaidi, lazima atoe thamani kubwa kwa wengine kuliko thamani anayopokea na lazima akue zaidi na akuze zaidi kile anachofanya.

Friday, January 4, 2019

TUMIA KAULI HII KILA SIKU , " MIMI NI TAJIRI MAFUNZONI " NA EPUKA KAULI HII , " MIMI NI MASKINI " AU " SISI NI WATU MASKINI "

Ndugu yangu, mdau  wangu  kama kuna kitu kimoja unachopaswa kukikataa kwa mwaka 2019 basi ni kukiri umasikini. Usikiri kwa kinywa chako kwamba wewe ni mtu masikini au mtu mnyonge, utaendelea kubaki kwenye hali hiyo.
Hata kama huna fedha, usijiite masikini, badala yake jiite tajiri mafunzoni. Tumia kauli chanya kuhusu fedha na utajiri na hilo litakaribisha fedha kwako zaidi na zaidi.

EPUKA KAULI HII MWAKA MPYA 2019 , " KAZI YA FEDHA NI MATUMIZI / KUTANUA / PONDA MALI KUFA KWAJA " ILI UWE NA MAFANIKIO MAKUBWA KIFEDHA KWAKO.

Hivi ndivyo wengi wanavyotengeneza mahusiano yao na fedha, wakizipata watazitumia mpaka ziishe ndiyo waweze kutulia.
Hupaswi kutumia kila fedha unayoipata mpaka iishe, na kwa hakika unapaswa kuweka akiba na kuwekeza kabla hata hujaanza kutumia fedha uliyonayo.
Acha kujiambia kazi ya fedha ni matumizi, au kutumia kauli kama tumia fedha ikuzoee. Kila fedha unayopata weka fungu fulani pembeni kwa ajili ya akiba na uwekezaji kabla hujaanza kutumia.