Sunday, September 2, 2018

FANYA MAAMUZI KWA WAKATI.

Fanya maamuzi wakati unapokutana na hitaji la kufanya maamuzi. Usijiambie wacha nifikiri nitaamua baadaye. Kama kitu ni muhimu fanya maamuzi sasa, au hutayafanya kabisa. Maamuzi yanayosogezwa mbele ni maamuzi ambayo yamekuwa hayafanywi.

Usiogope kukosea pale unapochagua kufanya maamuzi. Ni bora ufanye maamuzi ukosee, kwa sababu utarekebisha makosa yako, kuliko kutokufanya maamuzi kabisa.


Na  Mwl  Japhet  Masatu , Dar  es  salaam , Tanzania,  Afrika Ya  Mashariki  /+ 255 755 400 128 / + 255 716 924136(WhatsApp ).  EMAIL: japhetmasatu@gmail.com

USIKIMBIZANE NA VITU VYA KUPITA . WEWE KAZANA NA AMBAVYO SIYO VYA KUPITA.

Weka nguvu zako kwenye vitu ambavyo havitabadilika. Watu wengi huwa wanakazana kukimbizana na vitu vinavyopita, fursa mpya, fasheni na habari mpya ya mjini. Wewe kazana na vile ambavyo siyo vya kupita, na biashara yako itakuwa imara. Achana na vitu ambavyo watu wanataka sasa, kazana na vitu ambavyo watu wataendelea kuhitaji miaka kumi ijayo.



Na  Mwl  Japhet  Masatu , Dar  es  salaam , Tanzania,  Afrika Ya  Mashariki  /+ 255 755 400 128 / + 255 716 924136(WhatsApp ).  EMAIL: japhetmasatu@gmail.com