Saturday, May 31, 2025

MAFUNDISHO YA USHONAJI : SOMO : VIPIMO VYA ZIADA VYA OFFSHOULDER MOYO----FULL NUKUU---KWA WANAFUNZI WA USHONAJI -----TANZANIA----( PDF )-------CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136

MAKALA : JE, WAJUA KUSUDI LAKO KUWAKO HAPA DUNIANI ?? NDANI YAKO KUNA MOTO WA NDOTO ZAKO UMEFICHWA------NA MWL JAPHET MASATU ------CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136

 Rafiki Yangu Mpendwa,

‎Watu wengi wanamka kila siku…

‎Wanaoga, wanavaa, wanatoka.

‎Lakini hawajui kwa nini wanaishi.

‎Wanapambana… lakini hawajui wanapambana kwa lipi.

‎Wanaume wanahangaika na mihangaiko,

‎Wanawake wanahangaika na wanaume.

‎Kila mtu anakimbia, lakini hakuna anayeuliza:

‎"Tunakoenda ni wapi?"

‎Ishu Hii Ndio Inasababisha Maisha Ya Watu Yatupwe Kama Karatasi Iliyotumika.

‎Unajikuta una miaka 30... lakini unahisi hujaanza kuishi.

‎Unajiona hufai.

‎Unachoka bila kazi.

‎Una usingizi wa saa 10 lakini bado umechoka.

‎Unapoteza nguvu kwenye mambo yasiyojenga.

‎Unapata hela unazimaliza bila hata kumbukumbu.

‎Unapenda unakataliwa.

‎Unajifunza lakini bado maisha yako yapo vile vile.

‎Unapambana, lakini unapambana gizani.

‎Umefungwa kwa minyororo usiyoiona…

‎Na minyororo hiyo inaitwa: "Kutokujua KUSUDI la maisha yako."

‎Kujua Kisudi Ni Siri Ya Waliotoka Chini Wakafika Juu.

‎Wewe si maskini umepoteza mwelekeo tu.

‎Wewe si mvivu hujagundua unachopaswa kufanya.

‎Wewe si mshindwa hujajua sababu ya wewe kuwa hai.

‎Watu wakishajua walichozaliwa kufanya,

‎wanabadilika kama mwewe aliyefunguliwa.

‎Wanapaa.

‎Wanang’ara.

‎Wanatesa!

‎Ukweli Ni Huu: Maisha Hayaanzi Kwa Kupata Pesa Yanaanza Kwa Kujielewa.

‎Na huwezi kujielewa bila MWONGOZO.

‎Huwezi kufika bila RAMANI.

‎Huwezi kushinda bila KUJUA UNAPIGANIA NINI.

‎Ukweli mwingine ni huu:

‎Watu wengi wameishia kuishi maisha ya kuigiza.

‎Maisha ya watu wengine.

‎Wanavaa kama wengine.

‎Wanakimbia mafanikio ya wengine.

‎Wanajilinganisha.

‎Wanashindana.

‎Lakini ndani yao kuna MOTO UMEFICHWA.

‎Moto wa ndoto zao.

‎Moto wa kusudi lao.

‎Moto wa ukubwa wao halisi.

‎SULUHISHO?

‎Chukua MWONGOZO huu: “MWONGOZO WA MAISHA YA MAFANIKIO.”

‎KWA   KUEDELEA    KUSOMA    VITABU  Ndani yake utajifunza:

✅ Jinsi ya kugundua kusudi lako.

‎Sheria 100 za maisha ya mafanikio.

✅ Jinsi ya kuamka kila asubuhi ukiwa na maana

✅ Jinsi ya kuishi maisha ya tofauti

✅ Jinsi ya kuacha kuigiza na kuanza kuishi maisha yako halisi

‎Bado namkumbuka Huyu Kijana.

‎Kuna kijana mmoja alinitafuta.

‎Alichoka kuishi maisha ya ‘kawaida.’

‎Alikuwa na degree.

‎Alikuwa na kazi.

‎Lakini kila kitu kilionekana kimekosa ladha.

‎Akaanza kunywa.

‎Akaanza kuchelewa kazini.

‎Akaanza kujichukia.

‎Siku moja akaniambia:

‎“Bro, naishi kama si mimi.”

‎Nikampa mwongozo huu.

‎Akarudi baada ya wiki tatu na macho yenye mwanga.

‎Sasa ameanzisha kitu chake.

‎Anaamka kabla ya saa kumi.

‎Anapata pesa.

‎Anapendwa.

‎Anajipenda.

‎Maana sasa anajua KUSUDI lake.

‎Uko Tayari Kuamka?

‎Ama utaendelea kuishi kama ndoto ya mtu mwingine?

👉 Usiishi kama kivuli jifunze kuangaza.

ENDELEA   KUSOMA   VITABU    KILA  SIKU  ILI  UENDELEE  KUANGAZA  NA    KUISHI  KUSUDI  LAKO

Friday, May 30, 2025

MAKALA : MJASIRIAMARI MJANJA ANA TABIA GANI ???

 Kakaa/Dadaa Yangu,

‎ Unajua shida ya wengi?

‎Wengi wanaanza biashara kwa kishindo...

‎Lakini baada ya miezi mitatu,

‎BAM! Kimya kama kaburi la usiku.

‎Wanaanza kuuza nguo,

‎Wanaingiza mzigo wa milioni mbili,

‎Lakini hakuna anayenunua.

‎Wanashindwa kuelewa nini kinakwenda kombo.

‎Wanakata tamaa fasta.

‎Wanarejea kutegemea mshahara.

‎Wengine wanakata tamaa kabisa—wanakufa na ndoto zao.

💔 Na hapa ndipo kuna maumivu makali.

‎Biashara si kupost tu bidhaa kwenye status.

‎Si kutegemea rafiki zako watanunua.

‎Wala si kushusha bei kila siku eti "promo."

‎Ukiwa huna akili ya mjasiriamali mjanja

‎utachezewa kama karata mitaani.

🎯 Ngoja nikufunze kitu.

‎Mjasiriamali mjanja ana akili ya pesa.

‎Anajua kutafuta wateja wake popote.

‎Anajua jinsi ya kuwashawishi bila kusumbua.

‎Anajua kutoa ofa ambayo haiwezi kukataliwa.

‎Anaelewa psychology ya mteja.

‎Na zaidi ya yote, anajua kuji-brand.

‎Na kama hujui hayo yote,

‎Usijidanganye eti “ni mapenzi ya Mungu.”

‎Ni mapenzi ya kukosa maarifa.

⚙️ Sasa suluhisho liko hivi:

‎Ukiamua kuwa mjanja kwenye biashara

‎Lazima ujue kuuza hadithi.

‎Ndiyo, HADITHI!

‎Watu wananunua stori kabla ya bidhaa.

‎Wakiigusa hadithi yako,

‎Wanafika mwisho wa status tayari wamejishawishi.

‎Ukiuza sabuni,

‎Usiuze sabuni uza usafi wa mtoto wako.

‎Ukiuza viatu,

‎Usiuze kiatu uza heshima ya mguu wake kazini.

‎Mjasiriamali mjanja anauza HISIA si bidhaa tu.

🧠 Nikupe hadithi moja ya kweli.

‎Mrembo mmoja anaitwa Amina.

‎Alikuwa anauza mikoba Kariakoo.

‎Alihangaika sana, kila siku status 50, likes 2, wateja 0.

‎Alipojifunza kuuza kwa stori, mambo yalianza kubadilika.

‎Siku moja aliandika:

‎“Mwanamke mmoja alikuja dukani kwangu, akiwa amechoka, alinyamaza muda mrefu...

‎Aliponunua hii handbag,

‎Alisema, ‘Kwa mara ya kwanza najihisi mwanamke kamili.’

‎Niliogopa kusema chochote,

‎Ila moyo wangu ulichanua.

‎Na hapo ndipo nilijua,

‎Siuzi mikoba, nauza imani kwa mwanamke.”

‎Dakika 20 baadaye mikoba 7 iliuzwa.

MAKALA : MJASIRIAMALI MJANJA NA MBUNIFU NI NANI ??

 

Ni yule anayejifunza kila siku.

‎Anayefikiria tofauti.

‎Anayejua kutumia lugha ya wateja.

‎Anayeuza kwa hisia, si bei.

‎Wewe je?

‎Upo kwenye biashara kwa bahati,

‎Au umeamua kuwa MJASIRIAMALI MJANJA?

‎ Kumbuka hii ya mwisho:

‎Wakati wengine wanauza bidhaa,

‎MJANJA ANAUZA STORI INAYOCHOMA MOYO.

‎MUHIMU; Kama bado hujasoma kitabu cha MJASIRIAMALI MJANJA,

‎Ukweli ni kwamba unajipunja,

BOOK 345 --- I CAN , I MUST , I WILL ----THE SPIRIT OF SUCCESS ---BY DR. REGINALD ABRAHAM MENGI---TANZANIA---2018-----( PDF )-----CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716924 136