MAISHA NA MAFANIKIO (LIFE AND YOU) BLOG
BADILI FIKRA.FIKIRI TOFAUTI .BADILI MAISHA.JITAMBUE .JIFUNZE ELIMU YA SAIKOLOJIA,TEOLOJIA , FEDHA ,UTAMBUZI(SELF HELP EDUCATION),FALSAFA YA MAISHA,MAISHA NA MAFANIKIO,BIASHARA / UJASIRIAMALI.FURAHIA WASAA WAKO NA MAISHA NA MAFANIKIO BLOGU.THIS IS THE COMMUNITY CAPACITY BUILDING BLOG.ENJOY THE BLOG.STRETCH YOUR MIND. YOU CAN CHANGE YOUR LIFE FOR EVER. YOU CAN ACHIEVE EXCELLENCE.YOU CAN MAKE A DIFFERENCE.
Saturday, May 31, 2025
MAKALA : JE, WAJUA KUSUDI LAKO KUWAKO HAPA DUNIANI ?? NDANI YAKO KUNA MOTO WA NDOTO ZAKO UMEFICHWA------NA MWL JAPHET MASATU ------CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136
Rafiki Yangu Mpendwa,
Watu wengi wanamka kila siku…
Wanaoga, wanavaa, wanatoka.
Lakini hawajui kwa nini wanaishi.
Wanapambana… lakini hawajui wanapambana kwa lipi.
Wanaume wanahangaika na mihangaiko,
Wanawake wanahangaika na wanaume.
Kila mtu anakimbia, lakini hakuna anayeuliza:
"Tunakoenda ni wapi?"
Ishu Hii Ndio Inasababisha Maisha Ya Watu Yatupwe Kama Karatasi Iliyotumika.
Unajikuta una miaka 30... lakini unahisi hujaanza kuishi.
Unajiona hufai.
Unachoka bila kazi.
Una usingizi wa saa 10 lakini bado umechoka.
Unapoteza nguvu kwenye mambo yasiyojenga.
Unapata hela unazimaliza bila hata kumbukumbu.
Unapenda unakataliwa.
Unajifunza lakini bado maisha yako yapo vile vile.
Unapambana, lakini unapambana gizani.
Umefungwa kwa minyororo usiyoiona…
Na minyororo hiyo inaitwa: "Kutokujua KUSUDI la maisha yako."
Kujua Kisudi Ni Siri Ya Waliotoka Chini Wakafika Juu.
Wewe si maskini umepoteza mwelekeo tu.
Wewe si mvivu hujagundua unachopaswa kufanya.
Wewe si mshindwa hujajua sababu ya wewe kuwa hai.
Watu wakishajua walichozaliwa kufanya,
wanabadilika kama mwewe aliyefunguliwa.
Wanapaa.
Wanang’ara.
Wanatesa!
Ukweli Ni Huu: Maisha Hayaanzi Kwa Kupata Pesa Yanaanza Kwa Kujielewa.
Na huwezi kujielewa bila MWONGOZO.
Huwezi kufika bila RAMANI.
Huwezi kushinda bila KUJUA UNAPIGANIA NINI.
Ukweli mwingine ni huu:
Watu wengi wameishia kuishi maisha ya kuigiza.
Maisha ya watu wengine.
Wanavaa kama wengine.
Wanakimbia mafanikio ya wengine.
Wanajilinganisha.
Wanashindana.
Lakini ndani yao kuna MOTO UMEFICHWA.
Moto wa ndoto zao.
Moto wa kusudi lao.
Moto wa ukubwa wao halisi.
SULUHISHO?
Chukua MWONGOZO huu: “MWONGOZO WA MAISHA YA MAFANIKIO.”
KWA KUEDELEA KUSOMA VITABU Ndani yake utajifunza:
Jinsi ya kugundua kusudi lako.
Sheria 100 za maisha ya mafanikio.
Jinsi ya kuamka kila asubuhi ukiwa na maana
Jinsi ya kuishi maisha ya tofauti
Jinsi ya kuacha kuigiza na kuanza kuishi maisha yako halisi
Bado namkumbuka Huyu Kijana.
Kuna kijana mmoja alinitafuta.
Alichoka kuishi maisha ya ‘kawaida.’
Alikuwa na degree.
Alikuwa na kazi.
Lakini kila kitu kilionekana kimekosa ladha.
Akaanza kunywa.
Akaanza kuchelewa kazini.
Akaanza kujichukia.
Siku moja akaniambia:
“Bro, naishi kama si mimi.”
Nikampa mwongozo huu.
Akarudi baada ya wiki tatu na macho yenye mwanga.
Sasa ameanzisha kitu chake.
Anaamka kabla ya saa kumi.
Anapata pesa.
Anapendwa.
Anajipenda.
Maana sasa anajua KUSUDI lake.
Uko Tayari Kuamka?
Ama utaendelea kuishi kama ndoto ya mtu mwingine?
Usiishi kama kivuli jifunze kuangaza.
ENDELEA KUSOMA VITABU KILA SIKU ILI UENDELEE KUANGAZA NA KUISHI KUSUDI LAKO
Friday, May 30, 2025
MAKALA : MJASIRIAMARI MJANJA ANA TABIA GANI ???
Kakaa/Dadaa Yangu,
Unajua shida ya wengi?
Wengi wanaanza biashara kwa kishindo...
Lakini baada ya miezi mitatu,
BAM! Kimya kama kaburi la usiku.
Wanaanza kuuza nguo,
Wanaingiza mzigo wa milioni mbili,
Lakini hakuna anayenunua.
Wanashindwa kuelewa nini kinakwenda kombo.
Wanakata tamaa fasta.
Wanarejea kutegemea mshahara.
Wengine wanakata tamaa kabisa—wanakufa na ndoto zao.
Na hapa ndipo kuna maumivu makali.
Biashara si kupost tu bidhaa kwenye status.
Si kutegemea rafiki zako watanunua.
Wala si kushusha bei kila siku eti "promo."
Ukiwa huna akili ya mjasiriamali mjanja
utachezewa kama karata mitaani.
Ngoja nikufunze kitu.
Mjasiriamali mjanja ana akili ya pesa.
Anajua kutafuta wateja wake popote.
Anajua jinsi ya kuwashawishi bila kusumbua.
Anajua kutoa ofa ambayo haiwezi kukataliwa.
Anaelewa psychology ya mteja.
Na zaidi ya yote, anajua kuji-brand.
Na kama hujui hayo yote,
Usijidanganye eti “ni mapenzi ya Mungu.”
Ni mapenzi ya kukosa maarifa.
Sasa suluhisho liko hivi:
Ukiamua kuwa mjanja kwenye biashara
Lazima ujue kuuza hadithi.
Ndiyo, HADITHI!
Watu wananunua stori kabla ya bidhaa.
Wakiigusa hadithi yako,
Wanafika mwisho wa status tayari wamejishawishi.
Ukiuza sabuni,
Usiuze sabuni uza usafi wa mtoto wako.
Ukiuza viatu,
Usiuze kiatu uza heshima ya mguu wake kazini.
Mjasiriamali mjanja anauza HISIA si bidhaa tu.
Nikupe hadithi moja ya kweli.
Mrembo mmoja anaitwa Amina.
Alikuwa anauza mikoba Kariakoo.
Alihangaika sana, kila siku status 50, likes 2, wateja 0.
Alipojifunza kuuza kwa stori, mambo yalianza kubadilika.
Siku moja aliandika:
“Mwanamke mmoja alikuja dukani kwangu, akiwa amechoka, alinyamaza muda mrefu...
Aliponunua hii handbag,
Alisema, ‘Kwa mara ya kwanza najihisi mwanamke kamili.’
Niliogopa kusema chochote,
Ila moyo wangu ulichanua.
Na hapo ndipo nilijua,
Siuzi mikoba, nauza imani kwa mwanamke.”
Dakika 20 baadaye mikoba 7 iliuzwa.
MAKALA : MJASIRIAMALI MJANJA NA MBUNIFU NI NANI ??
Ni yule anayejifunza kila siku.
Anayefikiria tofauti.
Anayejua kutumia lugha ya wateja.
Anayeuza kwa hisia, si bei.
Wewe je?
Upo kwenye biashara kwa bahati,
Au umeamua kuwa MJASIRIAMALI MJANJA?
Kumbuka hii ya mwisho:
Wakati wengine wanauza bidhaa,
MJANJA ANAUZA STORI INAYOCHOMA MOYO.
MUHIMU; Kama bado hujasoma kitabu cha MJASIRIAMALI MJANJA,
Ukweli ni kwamba unajipunja,