Sisi binadamu ni wabaya sana kwenye kujisimamia wenyewe, huwa
tunajionea sana huruma na ni rahisi sana kujidanganya. Unaweza kuwa na
orodha yako ya siku, umepanga mambo yako matano muhimu na hata kujiwekea
ukomo. Lakini katikati ya siku yako ukawa hujisikii kuendelea na yale
uliyopanga, ni rahisi kujihalalishia kwamba labda umechoka au ni kitu
hakiwezekani.
Lakini unapokuwa na mtu wa pembeni, mtu ambaye jukumu lake ni
kuhakikisha umekamilisha uliyopanga na hapokei sababu bali matokeo,
utalazimika kufanya kile ulichopanga kufanya.
Tafuta mtu wa karibu kwako, ambaye hakuonei huruma kisha mtake
akusimamie kwa karibu ili utimize unachotaka. Kama huwezi kupata mtu wa
karibu basi kuwa na kocha au menta ambaye atakusimamia kwa karibu.
No comments:
Post a Comment