Kuna wakati unakuwa umeshapanga kabisa nini utafanya na kwa wakati
gani. Lakini inapofika muda wa kufanya, mawazo ya kuahirisha yanaanza
kukuingia. Unaanza kuona labda hujawa tayari au ni bora kusubiri.
Ni katika wakati kama huu ndiyo unapaswa kujiambia kauli hii,
NAFANYA SASA HIVI, rudia kauli hiyo mara nyingi uwezavyo na utajikuta
umeanza kufanya. Kila unapofikiria kuahirisha kufanya kitu, jiambie
kauli hiyo kwamba unafanya. Kila unapoanza kujiambia kwambe umechoka,
anza kujiambia kauli hiyo.
Kwa kurudia rudia kujiambia kauli hiyo, unaanza kuiamini na kujiamini wewe mwenyewe na kuanza kufanya.
No comments:
Post a Comment