SOMA VITABU KILA SIKU

Friday, May 30, 2025

MAKALA : MJASIRIAMARI MJANJA ANA TABIA GANI ???

 Kakaa/Dadaa Yangu,

‎ Unajua shida ya wengi?

‎Wengi wanaanza biashara kwa kishindo...

‎Lakini baada ya miezi mitatu,

‎BAM! Kimya kama kaburi la usiku.

‎Wanaanza kuuza nguo,

‎Wanaingiza mzigo wa milioni mbili,

‎Lakini hakuna anayenunua.

‎Wanashindwa kuelewa nini kinakwenda kombo.

‎Wanakata tamaa fasta.

‎Wanarejea kutegemea mshahara.

‎Wengine wanakata tamaa kabisa—wanakufa na ndoto zao.

💔 Na hapa ndipo kuna maumivu makali.

‎Biashara si kupost tu bidhaa kwenye status.

‎Si kutegemea rafiki zako watanunua.

‎Wala si kushusha bei kila siku eti "promo."

‎Ukiwa huna akili ya mjasiriamali mjanja

‎utachezewa kama karata mitaani.

🎯 Ngoja nikufunze kitu.

‎Mjasiriamali mjanja ana akili ya pesa.

‎Anajua kutafuta wateja wake popote.

‎Anajua jinsi ya kuwashawishi bila kusumbua.

‎Anajua kutoa ofa ambayo haiwezi kukataliwa.

‎Anaelewa psychology ya mteja.

‎Na zaidi ya yote, anajua kuji-brand.

‎Na kama hujui hayo yote,

‎Usijidanganye eti “ni mapenzi ya Mungu.”

‎Ni mapenzi ya kukosa maarifa.

⚙️ Sasa suluhisho liko hivi:

‎Ukiamua kuwa mjanja kwenye biashara

‎Lazima ujue kuuza hadithi.

‎Ndiyo, HADITHI!

‎Watu wananunua stori kabla ya bidhaa.

‎Wakiigusa hadithi yako,

‎Wanafika mwisho wa status tayari wamejishawishi.

‎Ukiuza sabuni,

‎Usiuze sabuni uza usafi wa mtoto wako.

‎Ukiuza viatu,

‎Usiuze kiatu uza heshima ya mguu wake kazini.

‎Mjasiriamali mjanja anauza HISIA si bidhaa tu.

🧠 Nikupe hadithi moja ya kweli.

‎Mrembo mmoja anaitwa Amina.

‎Alikuwa anauza mikoba Kariakoo.

‎Alihangaika sana, kila siku status 50, likes 2, wateja 0.

‎Alipojifunza kuuza kwa stori, mambo yalianza kubadilika.

‎Siku moja aliandika:

‎“Mwanamke mmoja alikuja dukani kwangu, akiwa amechoka, alinyamaza muda mrefu...

‎Aliponunua hii handbag,

‎Alisema, ‘Kwa mara ya kwanza najihisi mwanamke kamili.’

‎Niliogopa kusema chochote,

‎Ila moyo wangu ulichanua.

‎Na hapo ndipo nilijua,

‎Siuzi mikoba, nauza imani kwa mwanamke.”

‎Dakika 20 baadaye mikoba 7 iliuzwa.

No comments:

Post a Comment