Kabla hujaweka malengo yoyote, anza
kwanza na vipaumbele. Watu wengi wanakosea kwenye kuweka malengo kwa
sababu hawajui na pia hawana vipaumbele kwenye maisha yao. Hilo
linawapelekea kuweka malengo ambayo hata hawajui wanayafikiaje, kwa
sababu yanakuwa hayaendani na hayajapangiliwa vizuri.
Chagua vipaumbele vichache kwa mwaka
unaofuata, angalia yale maeneo ambayo ni ya muhimu zaidi kwenye maisha
yako, ambayo ukiyasimamia vizuri na kuyafanyia kazi, utaweza kupata
matokeo bora sana kwenye maisha yako.
Kwa kujua vipaumbele vyako, utaweza kuweka malengo ambayo ni sahihi kwako na yanafikika.
HERI YA X--MASS NA MWAKA MPYA.
No comments:
Post a Comment