Watu wengi huwa wanauanza mwaka kwa
matumaini makubwa, wanaweka malengo makubwa lakini huwa hayamalizi
mwezi, wanaachana nayo na kurudi kwenye maisha ya kawaida.
Unapofika mwezi disemba ni wakati mzuri
wa kuutafakari mwaka unaokwenda kuumaliza, kuangalia yale malengo na
mipango uliyojiwekea na pia kuangalia kwa kiasi gani umeweza kutekeleza.
Kwa yale malengo uliyoachana nayo, jua tatizo ni nini, uliyaweka vibaya au uvivu na uzembe wako ndiyo umekufanya uachane nayo?
Angalia pia fursa mbalimbali ulizokutana nazo kwenye mwaka wako mzima, zile ulizofanyia kazi na zile zilizokupita.
Kwa kuutafakari mwaka unaokwenda kuumaliza, utaweza kuona wapi umefanya vizuri, wapi umekosea na marekebisho yapi ya kufanya.
HERI YA X--MASS NA MWAKA MPYA.
No comments:
Post a Comment