Katika MAISHA watu hufurahia zaidi
yale waliyokamilisha pekee huku wakiyasahau kabisa yale ambayo hawajayafanya au
kuyakamilisha.
Pia kitendo cha kuyafurahia yale ambayo umeyafanya na
kujiona wewe ni bora zaidi hukufanya uzidi kubweteka na kuachana na yale
unayoyakosea katika maisha.
Hivyo NDUGU yangu MDAU wangu katika maisha haya unatakiwa
kukumbuka ya kwamba yale uliyoyapanga na kuyakamilisha ni jambo jema sana, ila
kama unataka kuwa bora zaidi ya hapo ulipo sasa unatakiwa kushughulika na yale
machache yalikuwa ni vikwazo ambayo yamekufanya ushindwe kufanya vizuri zaidi.
Asante sana kwa kusoma , Ndimi MWL JAPHET MASATU , DAR ES SALAAM, TANZANIA, AFRIKA YA MASHARIKI.
No comments:
Post a Comment