USTOA ni falsafa ya matendo, ni falsafa ambayo imelenga kumwezesha
mtu kuwa na maisha bora, kwa kufikiri sahihi na kuchukua hatua sahihi
kwenye maisha yake. Falsafa ya ustoa siyo kama falsafa nyingine za
kubishana na kutaka kuonekana unajua zaidi, badala yake ni falsafa ya
kufikiri sahihi na kuchukua hatua sahihi. Falsafa ya ustoa inalenga
kudhibiti hisia zetu na kuishi kulingana na asili. Kwa njia hiyo,
tunakuwa na maisha bora wakati wote.
Falsafa ya ustoa ilianzishwa na Zeno wa Citium miaka ya 301 K.K na
baadaye kupokelewa na kukuzwa na wanafalsafa Cato, Seneca, Epictetus na
Marcus Aurelius. Hawa wote ni wanafalsafa walioishi zaidi ya miaka 2000
iliyopita, wakati wa utawala wa Roma.
No comments:
Post a Comment