NYUMBA ZA KUPANGISHA
KUJENGA NYUMBA ZA KUPANGISHA ni njia mojawapo unayoweza kuitumia katika KUWEKEZA. Utafiti niliowahi kufanya kwa kuchunguza matajiri ninaowafahamu ni kwamba kila mmoja anamiliki wastani wa nyumba tano. Moja kati ya hizo , anaishi yeye mwenyewe na nne ANAPANGISHA.
FAIDA ya KUWEKEZA kwenye nyumba ni kwamba , NYUMBA ZINA TABIA YA KUPANDA THAMANI pia KODI ZA NYUMBA zina tabia ya KUPANDA.
KUMBUKA pia ukiwa na HATI YA NYUMBA yaweza kutumika kama DHAMANA YA MKOPO.
MAPATO YA KODI YA PANGO ni ya uhakika. Hivyo humsaidia MTU asikwame hata kama BIASHARA zake zitayumba , na hivyo hawawezi KUKOSA FEDHA ZA CHAKULA NA MATUMIZI MENGINEYO.
SUALA LA KUWEKEZA linatakiwa lifanywe kwa Umakini Mkubwa na kupata USHAURI WA WATAALAMU WA MBINU ZA UWEKEZAJI.
UKIWA NA FEDHA ZA ZIADA TAFUTA NAMNA YA KUZIWEKEZA ILI UPATE FAIDA ZAIDI.
Asante kwa kusoma makala hii ! Mungu Akubariki !!
No comments:
Post a Comment