KUNUNUA HISA
Kununua Hisa ni njia nyingine ya KUWEKEZA. Faida ya kununua HISA ni kwamba thamani ya FEDHA zako katika HISA hukua kutokana na ukuaji wa FAIDA YA KAMPUNI.
Kwa mfano, umenunua HISA 1,000 za kampuni fulani kwa bei ya Tshs 300 kwa HISA utalipa TShs 300,000/= thamani ya HISA zako zile zile zikipanda mara mbili ukiziuza utapata TShs 600,000 /= .
FAIDA nyingine ya kuwekeza katika HISA ni kupata GAWIO. Makampuni mengi hutengeneza mahesabu kila baada ya miezi 3 na kutoa GAWIO kwa wenye HISA.
HASARA ya kuwekeza katika HISA kuna wakati makampuni hupata HASARA na hivyo kutotoa GAWIO na HISA zinaweza kushuka thamani.
No comments:
Post a Comment