KATIKA MAZINGIRA YA SOKO HURIA , FAIDA inayopatikana katika BIASHARA inatakiwa kuwa " TUZO tu ya uendeshaji wa BIASHARA katika njia inayokubalika.. " Kwa wale wanaopenda kukwepa KULIPA KODI , WAEPUKE HISIA MBAYA dhidi ya KODI , NA KUIFIKIRIA KODI kama matumizi ya lazima ya biashara , , tunayopaswa KULIPA kwa lengo la KUSAIDIA JAMII tunayofanya nayo BIASHARA ZETU. HATUPASWI KUFICHA FAIDA YETU KICHOYO ETI ISIKATWE KODI !!
FAIDA YA KWELI katika BIASHARA ni ile inayotokana na Ongezeko la MAUZO pamoja na UPUNGUZAJI WA GHARAMA ZA UZALISHAJI , SIYO KWA KUUZA BIDHAA KWA BEI YA JUU.
SIRI YA MAFANIKIO IKO KWENYE KUPATA HESHIMA KUTOKA KWA WATEJA WAKO PAMOJA WALE UNAOWAONGOZA. WATEJA wako wanapaswa kuridhika kuwa PESA wanayolipa inalingana na thamani halisi ya bidhaa au huduma wanazopata toka kwako .
No comments:
Post a Comment